Uhalisia wa GPA na uwezo wa mtu kiakili

Dogo Tundu

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2009
Posts
448
Reaction score
189
Kwanza mi nikiri kuwa GPA ni kipimo cha kisayansi juu ya uwezo wa mtu darasani (but not applicable in practical life) hapa namaanisha hakuna mahusiano ya moja kwa moja kati ya GPA kubwa na mafanikio ya kimaisha.

Sasa kuna watu bila ku consider mazingira ya mtu alipokuwa chuo, moja kwa moja wanamjaji uwezo wake wa akili na GPA, masalani yule aliyepata GPA ndogo huchukuliwa kama kilaza asiyeweza fanya chochote kwenye ulimwengu huu.

Kilichonishangaza ni matokeo ya juzi ya watahiniwa wa nafasi mbalimbali za kazi TPDC, kuna watu wane score mpaka zero, imagine!

Kwa wasiofahamu TPDC huitwa kwenye usaili wenye 1st na 2nd upper class tu. Wenye 2nd lower kushuka chini hawatakiwi kwenye hili shirika letu la umma.

What a discrimination!
Sasa swali langu how come mtu awe na hizo sifa za kitaaluma anashindwa kupata japo 1%. Ni aibu kwa mtu kuamini GPA ndo zinafanya kazi, huku wenye GPA kubwa wakiwatia aibu wenzao kwa kushindwa kujibu hata swali moja.

Kwa mfano nafasi niliyofanya written interview mimi mtu wa mwisho ana 8, imagine. Ifike wakati wa watanzania kuacha kubaguana sisi kwa sisi, tutakuwa tunaliangamiza taifa letu.
Mimi sina hizo GPA zao walizotaka but nadhani walini shotlist kutoka na Masters yangu, na nimeshika nafasi ya pili kati ya mamia tuliofanya hiyo written interview.

Naamini walitakiwa kuwa fair kwa kuita wote walioomba kwenye written then from there wangepata right candidates for oral interview.
 
Kwanza wewe una gpa ya ngapi au classs gani?alafu tuingie kwenye maada
 

Unakosea sana unapohusisha swala la GPA na ubaguzi. Mbona wanafunzi waliomaliza kidato cha sita wanapokuwa wanaomba vyuo huwa wanachaguliwa kwa kungalia ufaulu wao wa kidato cha sita?

Mbona hapo huwa huoni kama ni ubaguzi. Kwanini sasa inapokuja kwenye swala la kazi wanapohitaji watu wenye ufaulu wa juu zaidi mnakimbilia kusema ni ubaguzi?

Jamani watanzania wenzangu embu tuache visingizio dhaifu. Kwa mfano juzi tu watu wa PWC wamekuja chuoni kwetu kuhitaji wanafunzi wa mwaka wa mwisho kutoka kozi mbalimbali lakini kwa kigezo cha kuwa na upper second.je hapo utasema wanabagua? La hasha.

Ni wazi kwamba hapo watamchukua hata mtoto wa masikini ikimradi anauwezo mkubwa.
Najua utaweza kusema kuwa uwezo wa mtu sio GPA.

But swali litakuja palepale kuwa kama ww umekaa chuo miaka yote na ukakosa kuwa nidhamu ya kukusaidia kufanya vizuri je watakuamini vipi kuwa wakikuweka kwenye taasisi yao utafanya vizuri?
 
You have approached a sensitive matter from a wrong corner. Your arguments appear in red, my responses in blue. Twende kazi......

1. Sasa kuna watu bila ku consider mazingira ya mtu alipokuwa chuo, moja kwa moja wanamjaji uwezo wake wa akili na GPA, masalani yule aliyepata GPA ndogo huchukuliwa kama kilaza asiyeweza fanya chochote kwenye ulimwengu huu. Huoni una ji contradict na hapa Kwanza mi nikiri kuwa GPA ni kipimo cha kisayansi juu ya uwezo wa mtu darasani

2. Kilichonishangaza ni matokeo ya juzi ya watahiniwa wa nafasi mbalimbali za kazi TPDC, kuna watu wane score mpaka zero, imagine!, Sasa swali langu how come mtu awe na hizo sifa za kitaaluma anashindwa kupata japo 1%. Couldnt it be interpreted kwamba wenye lower second na pass wangepata sifuri kabisa? What is the basis for your perspectives? Tutajua baadaye.....lets continue

3. What a discrimination! Naamini walitakiwa kuwa fair kwa kuita wote walioomba kwenye written then from there wangepata right candidates for oral interview

How do you define discrimination? simply because you did not work hard enough to get the GPA as you have declared, you want rewards that those who worked hard disserve be treated as discrimination? When you say kuita wote walioomba, do you know how many they are? Are you aware that job applicants lost their lives in Nigeria as a result of implementing the suggestions you are making? No wonder you got GPA ndogo!
 
BRN haishii tu secondary na primary hata vyuo vikuu kwa ku consider GPA imekuwa tatizo katika nchi hii.Ufanisi hautokani na GPA bali jitihada na content aliyonayo mtu.
 
si kweli hata kidogo kuwa GPA ni kipimo cha kisayansi kujua akili ya mtu
 
Nahisi alitaka kututaarifu kwamba ana master degree na written interview alikuwa wa pili
 
si kweli hata kidogo kuwa GPA ni kipimo cha kisayansi kujua akili ya mtu

huenda watu wanachanganya na kipimo cha kisayansi kinachopima IQ = Intelligence Quotient ya mtu.

Sijui kama watu wameshatafiti kulinganisha tofauti ya uwezo kwa mfano wa mtu mwenye GPA kwa mfano 3.9 kutoka UDSM na yule atokae UDOM and so on kwa course ilele?
 
Kwa kitanzania sidhan kama GPA inaangaliwa sana and also at the end of the day people they do work inorder to get profits that's it!
 
kimtazamo gpa ni kipimo cha uelewa wa mwanafunzi darasani ila ktk suala la ajira ni vizuri content ya mtu ikaangaliwa kwani hizi gpa sa hv znanunuliwa tu!
Nawasilisha!

hiyo ni njia mojawapo ya kuchuja. Kwa mfano zimetangazwa nafasi 5 wakajitokeza waombaji 500 utawapataje hao wa5?
 

Asante mkuu kwa kunikejeli juu ya GPA yangu ndogo, hongera wewe mwenye GPA kubwa.

Kwenye ulimwengu huu watu hupitia mambo mengi ikiwemo changamoto mbalimbali za maisha, nadhani wewe hayajakukuta bado, omba yasikutembelee.

Hoja yangu ya msingi ilikuwa wapo wazembe na walistahili hizo GPA ndogo na wapo wenye uwezo pia bidii wanayo.

Kulingana na changamoto za kimaisha wapo walioshindwa kufikia malengo si kwa kuwa hawana uwezo bali mazingira yake ya kujisomea yalichangia kupata class ndogo. Dhambi iko wapi mtu kama huyo naye kupata fursa ya kufanya interview? Ili kupima uwezo wake?

Mtu kama huyu hastahili kuajiriwa?
Huoni tunapoteza vipaji kwa kuwa na ubaguzi wa namna hiyo?
What if viongozi wetu nawe tungesema lazima wawe na GPA kubwa?

Je ni kipimo sahihi kubaki tu kwenye GPA kubwa kupata talented person kwenye ajira na hasa kwenye mashirika yetu ya umma?

Je ni kweli wenye GPA kubwa wamekuwa na ufanisi mkubwa makazini?

Kwa leo ni hayo tu mkuu.
 
Utaratibu wa kumpima mtu kwa kutumia GPA ni wa kitaalam (nadhani), ni kweli mpango unaweza kuwa na changamoto zake, la msingi na ninalokiri (kwa uzoefu), wapo waliopata GPA kubwa kwenye utendaji(application) kwenye field maeneo yao ya kazi wakawa vilaza,na wapo walopata GPA ndogo wakatisha kwenye utendajii, baada ya kipimo hicho tuongeze kipimo cha uwezo wa mhusika kiutendaji pia, " it might bring us to give right persons right positions", au..?
 
GPA bado Ndio kipimo halisi cha kuanzia ili kujua uwezo wa mtu. Wengi wenu mnacheza tu vyuoni then mnakuja babwaja mitandaoni .someni acheni kelele.
 

kweli kabisa
 

Attachments

  • 1397967852180.jpg
    3.7 KB · Views: 813

Wenye akili wawe vio
 

Lengo la kwanza la kutumia GPA ni ku discriminate.

Baada ya hapo ndipo kingine kinaweza kufanyika. So far hakuna njia nyingine ya kupata right candidates katika positions mbalimbali zaidi ya kuanza na GPA.

Kama nataka kukuunga mkono ni kutoa ushauri kwamba to be fair bora kuanza na Oral wote (utapata candidates for paper), Then paper (utapata waliofaulu) of course baada ya hapa comes a subjective selection basing on both GPA and Expressive skills of candidates
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…