Uholanzi kusitisha matumizi ya chanjo ya AstraZeneca

Uholanzi kusitisha matumizi ya chanjo ya AstraZeneca

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191

chanjo

Uholanzi nayo imeamua kusitisha matumizi ya chanjo ya corona ya Oxford-AstraZeneca kwa kuhofia kuwa na madhara.
Serikali ya Uholanzi imeamua kuchukua hatua hiyo mpaka Machi 29 ili kuchukua tahadhari.

Awali Jamuhuri ya Ireland ilichukua uamuzi huohuo kwa kuhofia hatari ya watu kuganda damu baada ya kupata chanjo hiyo nchini Norway.
Lakini Shirika la Afya Duniani (WHO) hakuna uhusiano wowote baina ya chanjo hiyo na hatari ya watu kuganda damu.

Shirika la madawa la Muungano wa Ulaya(EMA) lilisema awali kwamba hakuna dalili kwamba chanjo hiyo inasababisha kugada kwa damu mwilini, likiongeza kuwa ni "faida ambayo zinaendelea kuwa kubwa kuliko hatari zake.

Denmark, Norway, Bulgaria, Iceland na Thailand pia wamesitisha matumizi ya chanjo ya AstraZeneca.
 
Zimewafanya kitu mbaya.cha ajabu WHO wamejikausha Kama hawaoni vile.na bado zinaendelea kuzalishwa.
 
Aisee warudi tu maabara kwanza hakuna haraka ya kuleta chanjo ambayo inamadhara zaidi ya hiyo covid yenyewe
 
Back
Top Bottom