Uhuru Kenyatta asema atafungua kikao cha Bunge hata bila ya uwepo wa wabunge wa NASA leo

Uhuru Kenyatta asema atafungua kikao cha Bunge hata bila ya uwepo wa wabunge wa NASA leo

Kunguru Mjanja

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2012
Posts
2,046
Reaction score
3,971
Rais Uhuru Kenyatta ameukashifu mrengo wa NASA kwa kutishia kutohudhuria kikao cha pamoja cha bunge la taifa na lile la seneti leo. Rais anasema uwezo wa kiidadi ulio nao mrengo wa Jubilee kwenye mabunge yote unauwezesha kupitisha miswada na hivyo atatoa hotuba yake ilivyopangwa.

Kinara mwenza wa NASA Moses Wetangula hata hivyo anasema kikao hicho kinafaa kuahirishwa hadi rais atakayechaguliwa kwenye marudio ya uchaguzi aapishwe na kwa sasa Rais hana mamlaka ya kufungua bunge. Pia Moses Wetangula amesema wataohudhuria wataadhibiwa.

 
Siasa za ke na tz bure kabisa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Psalm 133:1[emoji768] "Behold, how good and how pleasant it is for brethren to dwell together in unity."
 
Chadema na UKAWA wana support wrong team. Inaonekana NASA ndio pacha wao.
 
Kenyatta mihemko mingi hata wananchi wanashidwa kumuelewa,mara anasema hiki mara kesho hiki je sibora akatulia na demokrasia ikachukua mkondo wake. (SURA MBILI USO MMOJA)
 
yaani hiyo uchaguzi ingefanyika tu huu mvutano ukwishe mara moja...wameanza kuleta siasa kama zile za kule kwa sizonje..
 
Naona mvutano wa kikatiba hapo, ni dhahili kuwa kwenye katiba hakuna kifungu kinachoongea juu ya ufunguzi wa bunge endapo uchaguzi utabatilishwa!

Ndo maana uhuru anasema atafanya hivi, nasa nao wanasema watafanya vile!
 
Back
Top Bottom