Uhuru Kenyatta barabarani bila ulinzi

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Sera za maridhiano hupelekea hali za kuaminiana kama hizi:

Uhuru Kenyatta Caught Off guard in Traffic.

Sera za kinunda nunda hupelekea yale ya kuombeana vifo, kuoteana vifo nk kama tunayoyashudia makwetu leo.

Niseme kabla ya kuhitimisha Lumumba buku 7 mafanikio kama hayo hayawuhusu hivyo nyie na midomo yenu michafu ya matusi vitu kabila hii achaneni navyo tu.
 
Picture and source please
 

Kitu gani unatuaminisha kuwa hana ulinzi..?? Ukute hayo magari yote pembeni yake ni secret service... Wabongo bwana...🙆🙆🙆
 
Naona bado sana uelewa wako wa maswala ya usalama uko chini ya kiwango!!
 
Nasubiria Jiwe aukache ulinzi akiongozana na Mbowe mahala fulani
 
Ngoja na sisi tuweke mazingira soon tutafanya hii.
 
Naona bado sana uelewa wako wa maswala ya usalama uko chini ya kiwango!!

Wewe mwenye uelewa na mambo ya usalama jiwe anaweza hata kufanya igizo kama hilo kama wewe waliona igizo?

Yote unavyoona na Uhuru yanatokana na jitihada kubwa ambayo kawekeza kwenye maridhiano.

Kwa mburula kama wewe ni muhimu kutambua kuwa theme ya uzi ni umuhimu wa maridhiano lakini hebu wewe ona uliowekwa nda - nje ya mada. Ndiyo maana nililazimika kuitisha nota bene Lumumba buku 7 watupishe. Haya hawayawezi.
 
Hamna kuridhiana na upinzani uchwara wa tz. Kama wamramua kucheza gemu JPM anacheza nao hivyo hivyo wanavyotaka wao.
Ni afadhari uridhiane na nzi kuliko ufipa.
 
Hamna kuridhiana na upinzani uchwara wa tz. Kama wamramua kucheza gemu JPM anacheza nao hivyo hivyo wanavyotaka wao.
Ni afadhari uridhiane na nzi kuliko ufipa.

Hivi hata hujihurumii achilia mbali kumhurumia huyo jiwe? Starehe gani anayo kwa mtaji kama huu?

 
Hivi hata hujihurumii achilia mbali kumhurumia huyo jiwe? Starehe gani anayo kwa mtaji kama huu?

Aisee, ujinga ulioubeba ni mzigo wako mwenyewe. Usitafute huruma. Unajua walikuwapo kina nani ktk huo msafara na walikuwa na shughuli gani?
Ujinga wako komaa nao mkuu mpaka ufike nao unakoenda ila hamna wa kukusaidia kuubeba hata utafute huruma namna gani. Zigo lako hilo mwenyewe.
 

Wasalimu Lumumba buku 7. Lugha za matusi peleka huko huko.

Kwa nota bene zote zile umefuata nini huku. Wa kutukanana naye umemkosa. Matusi peleka huko huko yatakusaidia.
 
Wasalimu Lumumba buku 7. Lugha za matusi peleka huko huko.

Kwa zile nota bene zote zile umefuata nini huku. Wa kutukanana naye umemkosa. Matusi peleka huko huko yatakusaidia.
Ujinga sio tusi.
Elimika mkuu.
Ningesema WEWE NI PUMBAVU, hapa sasa ningekuwa nimekutukana.
 
Unamaanisha Kenya ni shwari kuliko Tanzania?,_wale mabaunsa msafara wa Mbowe wa kazi gani?, Ulinzi wa Mkuu wa nchi ni jukumu letu sote hasa tunapotekeleza mipango mikubwa kwa Taifa udhibiti wa wizi wa madini, umeme, maji, maliasili, SGR, Strigers Gorge , ndege, hii mirafi ni tishio kwa mabeberu na mawakala wao. Hivyo ulinzi wa Rais ni Ulinzi wa Taifa. Take time to learn, take time to grow
 
Ujinga sio tusi.
Elimika mkuu.
Ningesema WEWE NI PUMBAVU, hapa sasa ningekuwa nimekutukana.

Umeshindwa kuona theme ndani ya bandiko lile na hata kusoma kilichomo kwenye ile link. Haiyumkiniki wewe ni maimuna.

Kwa akili yako ndogo umejiambia kuwa hoja inayoongelewa ati kuwa Uhuru hana ulinzi. Kina Nyerere walionekana hadharani na baiskeli, kina Salim waziri mkuu walionekana hadharani kwa miguu nk dalili ya hali nzuri ya utangamano nchini.

Ya Kenya dalili hizo ziko katika maridhiano wewe unasema ukaridhiane na nzi. Haiyumkiniki wewe ni nzi. Nzi kwa nzi mtashindwa vipi kuridhiana? Karaga baho!
 

Asiyejua maana haambiwi maana.

Soma uelewe. Kama hujaelewa soma tena kuelewa, kama bado soma tena kuelewa, nk nk umaimuna kuondokana nao yataka jitihada.

Utakapoelewa utaona nguvu ya maridhiano na faida yake. Ukiona bado hujaelewa soma tena mkuu. Hali mashakula kuidhinishwa kuelewa usisikitike sana watatafutwa wasukuma watafsiri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…