Wakuu,
COVID-19 ilisambazwa kwa makusudi duniani ili kusababisha migogoro kati ya mtu na mtu, jamii kwa jamii, taifa kwa taifa, mataifa kwa mataifa kisha uhai na mauti. COVID-19 haina rafiki awe mweupe, mweusi, mwekundu, mrefu, mfupi, msomi, maamuma, tajiri au maskini wote wako sawa mbele ya kirusi hicho chenye uwezo wa kujenga chuki ndani ya mtu dhidi ya mwingine bila sababu za msingi ila ubinafsi tupu ndio lengo lake halisi.
Maadui ni rahisi sana kuchonganisha kati ya mtu na mtu , taifa kwa taifa kupitia athari za ugonjwa wa COVID-19 kwa hiyo unapochngamana na mtu, jamii, au taifa jitahidi kutunza siri za ndani ya chumba chako unacholala zisiende nje hata kama humo ulimo kuna fukuto, ukikurupuka kwa ulimbukeni wa kuchukua mfumo wa maisha wa Magharibi kwamba wewe ni mwanahakati wa kupigania haki, atakaye kupongeza ndiye atakuja kukutweza na hautaamini kitakachotokea.
Nafikiri kama kuna watu wana rangi ya bluu inawezekana wakawa na roho ya pekee lakini sio hawa walio juu ya uso wa dunia tunayoishi wanadamu wote tukionekana kwa macho na kugusika kwa kushika.
Bado athari zake zitakuja kusababisha vurugu kubwa sana Ulaya, Marekani na kwa sehemu Afrika kisha baadhi ya maeneo ya nchi husika kutamani kujitenga na kujitawala wenyewe.
Huko mbeleni watu, jamii, nchi na mataifa ambayo yaliungana kwa nia njema hapo kabla wataingiwa na kirusi kisichoonekana kwenye fikra zao na kufanya mtengamano wao kuwa tete; baadhi watatengana kwa uhakika ikiwemo USA ambayo state zake tatu zitasababisha mtikisiko usiotarajiwa katika taifa hilo kubwa