Uhuru unapopotea, motisha ya asili ya kulisha tumbo huanza kufifia

Uhuru unapopotea, motisha ya asili ya kulisha tumbo huanza kufifia

Lior

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2018
Posts
1,617
Reaction score
3,697
Tukio hili lilitokea katika hekalu la Kombaru huko Karnataka, India.

Chui alikuwa akimfukuza mbwa, mbwa aliingia chooni kupitia dirisha, Choo kilikuwa kimefungwa kwa nje. Chui aliingia baada ya mbwa na wote wawili wakanaswa mle chooni; Mbwa alipomwona chui, aliogopa na kukaa kimya kwenye kona. Hakuthubutu hata kubweka.

Screenshot_20240329-192843~2.png

Ingawa chui alikuwa na njaa na kumfukuza mbwa, hakumla mbwa.
Angeweza kumla mbwa, lakini wanyama wawili walikuwa pamoja katika pembe tofauti kwa karibu saa kumi na mbili. Wakati wa saa hizi kumi na mbili, chui pia alikuwa mtulivu. Idara ya misitu ilimkaribia chui huyo na kumkamata.

Sasa swali ni je, kwa nini chui mwenye njaa hakumrarua mbwa wakati iliwezekana kirahisi?

Watafiti wa wanyamapori walijibu swali hili: kulingana na wao, wanyama wa mwitu ni sensitive sana kwenye uhuru wao.
Mara tu wanapotambua kwamba uhuru wao umepokonywa kutoka kwao, wanaweza kuhisi maumivu makali sana, kiasi kwamba wanaweza kusahau njaa yao.
Motisha yako ya asili ya kulisha tumbo lako huanza kufifia.

Uhuru na furaha vimeunganishwa. Uhuru wa kufikiri, kutenda, na kuishi jinsi tunavyotaka.
 
Ndugu si useme tu ulichokuwa unataka kusema kwa CCM sijui inafanya raia wakose furaha sijui kwasababu sijui hawapo huru sijui nini na nini, si useme mzee.
 
Thanks mods.
Ndugu si useme tu ulichokuwa unataka kusema kwa CCM sijui inafanya raia wakose furaha sijui kwasababu sijui hawapo huru sijui nini na nini, si useme mzee.
Hayo ni mawazo yako mkuu tusilishane maneno.
 
Back
Top Bottom