Midnight
JF-Expert Member
- Apr 24, 2021
- 229
- 681
Mungu ibariki Afrika.
Heshima kwenu ndugu zangu katika Jamii forum, washiriki katika Jamii forum page Facebook, Telegram na search engine zote zenye unapata kuunganishwa na nyuzi zote makini kutoka JF.
Kwanza kabisa napenda kuupongeza uongozi wa JF kwa kuleta mabadiliko na elimu pana miongoni mwa Watanzania na Wana East Africa kwa ujumla wake. Pongezi nyingi sana kwenu nyote kwa kazi nzuri.
Acha niende moja kwa moja kwenye lengo langu kuu la kuanzisha nyuzi hii, huku likiwa sehemu ya jibu langu kama nilivyomwahidi mwanafamilia mwenzetu mmoja hapa ndani.
Kama ungepata nafasi ya kutembelea Marekani na ukapewa kazi ya kutembelea statues zote zilizopo USA ndani ya mwezi mmoja sijuia kama ungezimaliza. Hadi kufikia mwaka 2011 nchini Marekani kulikuwa na sanamu zaidi ya 5193 zilizosimikwa katika kona na maeneo mbali mbali ya kihistoria na makazi ya watu.
Tunaendelea...... Kuanzia vita za wenyewe kwa wenye, ukombozi hadi vita vya vietnam, michezo, ubunifu na viongozi, utumwa, na yote unayoyajua wewe kuhusu America yapo katika hali ya sanamu zilizo tengenezwa vyema kukumbushia matukio na kumbukumbu husika.
September 11 Wamarekani hawaikumbuki kwa maneno tu, Bali pale palipokuwa na majengo pacha yaliyoshambuliwa kuna statue na vipande vya vyuma vya majengo yale ambavyo vitatunzwa na kuwepo pale pale hadi kizazi chako cha tano.
Tukiangalia mfano huo mdogo tu wa Marekani jinsi wanavyo tunza kumbukumbu zao kwa njia ya sanamu hizo huku sisi tukiziona kama ibada na upotoshaji kiimani. Na wakati huo huo huko zilikoanzia hizi dini tunazozifuata ndipo penye mamia ama maelfu ya sanamu, mfano Roma Italia kuna mamia ya dazani za masanamu ambapo ukiachana na vile watanzania wengi mnaamini ovyo kuhusiana na maana halisi za sanamu ukweli ni kuwa kuna umuhimu sana kujua nini tunapaswa kufanya na nini hatupaswi. Tunaweka sanamu ya Steven Kanumba kwaajiri ya kumbukumbu ya ubora wake au tunamwabudu?
Watoto wetu wanapaswa kujifunza historia na matukio muhimu ya nchi zetu kupitia vitu vinavyoonekana kwa macho, vitu ambavyo vitaleta nguvu, wivu wa kujaribu, hamasa na uzarendo kwa nchi yetu pale kijana anapokaa chini ya sanamu ya Edward Sokoine na kusoma historia yake huku moyoni akijengwa hamasa na utayari wa kulitumikia taifa lake na siku moja na yeye picha yake isimame katika uwanja wa mashujaa milele huku ikitunzwa na kutembelewa na vizazi na vizazi.
Pia sioni kama kuna wajasiliamali dhabiti hapa Tanzania. Kama wapo basi waunge mkono wazo langu kisha Katika kuisaidia serikali Katika majukumu muhimu ya kutunza na kuhifadhi utajiri wa Tanzania 🇹🇿 watengeneze japo vituo mbali mbali ndani ya miji mikubwa hapa nchini, vituo ambavyo kutakuwa na statues za watanzania wenzetu walioipeperusha vyema bendera yetu tukufu.
Hata mjenge statue ya nembo yetu adhimu ya bibi na bwana na mkionyesha vyema yale maneno tukufu ya kuiheshimisha nchi yetu nasi tutafunga safari na kuja kuchangia fedha hapo na kupiga picha kisha kupost na wageni watatuuliza hapo ni wapi, tutaeajibu ni Tanzania 🇹🇿 nchi ya ardhi ya mlima kilimanjaro.
Niseme ukweli tu kwamba utajiri wa Tanzania 🇹🇿 Sio Simba, Nyati na twiga pekee, Sio mlima kilimanjaro, ziwa Victoria au mbuga maarufu ya Serengeti na wala sio uzuri wa visiwa vya zanzibar na harufu ya karafuu bali ni mimi na wewe, viumbe pekee wenye jukumu la kuilinda na kuitunza Tanzania, kulinda vilivyokuwepo na tulivyovipoteza.
Hakuna tena mtu kama mzee King Majuto popote pale duniani, hayopo tena Mtu kama Mzee Jengua, Steven Kanumba, Mwalimu Nyerere, John Pombe Magufuri , na wengine wengi ambao majina yao na mchango wao kwa taifa ni mkubwa mno.
Tuache chuki na wivu tuanze sasa kujenga statues za watanzania wenzetu walioipeperusha vyema bendera yetu tukufu na kuiheshimisha na watoto wetu watapata kujifunza kupitia kumbukumbu hizo.
Ahsanteni sana.
Heshima kwenu ndugu zangu katika Jamii forum, washiriki katika Jamii forum page Facebook, Telegram na search engine zote zenye unapata kuunganishwa na nyuzi zote makini kutoka JF.
Kwanza kabisa napenda kuupongeza uongozi wa JF kwa kuleta mabadiliko na elimu pana miongoni mwa Watanzania na Wana East Africa kwa ujumla wake. Pongezi nyingi sana kwenu nyote kwa kazi nzuri.
Acha niende moja kwa moja kwenye lengo langu kuu la kuanzisha nyuzi hii, huku likiwa sehemu ya jibu langu kama nilivyomwahidi mwanafamilia mwenzetu mmoja hapa ndani.
Kama ungepata nafasi ya kutembelea Marekani na ukapewa kazi ya kutembelea statues zote zilizopo USA ndani ya mwezi mmoja sijuia kama ungezimaliza. Hadi kufikia mwaka 2011 nchini Marekani kulikuwa na sanamu zaidi ya 5193 zilizosimikwa katika kona na maeneo mbali mbali ya kihistoria na makazi ya watu.
Tunaendelea...... Kuanzia vita za wenyewe kwa wenye, ukombozi hadi vita vya vietnam, michezo, ubunifu na viongozi, utumwa, na yote unayoyajua wewe kuhusu America yapo katika hali ya sanamu zilizo tengenezwa vyema kukumbushia matukio na kumbukumbu husika.
September 11 Wamarekani hawaikumbuki kwa maneno tu, Bali pale palipokuwa na majengo pacha yaliyoshambuliwa kuna statue na vipande vya vyuma vya majengo yale ambavyo vitatunzwa na kuwepo pale pale hadi kizazi chako cha tano.
Tukiangalia mfano huo mdogo tu wa Marekani jinsi wanavyo tunza kumbukumbu zao kwa njia ya sanamu hizo huku sisi tukiziona kama ibada na upotoshaji kiimani. Na wakati huo huo huko zilikoanzia hizi dini tunazozifuata ndipo penye mamia ama maelfu ya sanamu, mfano Roma Italia kuna mamia ya dazani za masanamu ambapo ukiachana na vile watanzania wengi mnaamini ovyo kuhusiana na maana halisi za sanamu ukweli ni kuwa kuna umuhimu sana kujua nini tunapaswa kufanya na nini hatupaswi. Tunaweka sanamu ya Steven Kanumba kwaajiri ya kumbukumbu ya ubora wake au tunamwabudu?
Watoto wetu wanapaswa kujifunza historia na matukio muhimu ya nchi zetu kupitia vitu vinavyoonekana kwa macho, vitu ambavyo vitaleta nguvu, wivu wa kujaribu, hamasa na uzarendo kwa nchi yetu pale kijana anapokaa chini ya sanamu ya Edward Sokoine na kusoma historia yake huku moyoni akijengwa hamasa na utayari wa kulitumikia taifa lake na siku moja na yeye picha yake isimame katika uwanja wa mashujaa milele huku ikitunzwa na kutembelewa na vizazi na vizazi.
Pia sioni kama kuna wajasiliamali dhabiti hapa Tanzania. Kama wapo basi waunge mkono wazo langu kisha Katika kuisaidia serikali Katika majukumu muhimu ya kutunza na kuhifadhi utajiri wa Tanzania 🇹🇿 watengeneze japo vituo mbali mbali ndani ya miji mikubwa hapa nchini, vituo ambavyo kutakuwa na statues za watanzania wenzetu walioipeperusha vyema bendera yetu tukufu.
Hata mjenge statue ya nembo yetu adhimu ya bibi na bwana na mkionyesha vyema yale maneno tukufu ya kuiheshimisha nchi yetu nasi tutafunga safari na kuja kuchangia fedha hapo na kupiga picha kisha kupost na wageni watatuuliza hapo ni wapi, tutaeajibu ni Tanzania 🇹🇿 nchi ya ardhi ya mlima kilimanjaro.
Niseme ukweli tu kwamba utajiri wa Tanzania 🇹🇿 Sio Simba, Nyati na twiga pekee, Sio mlima kilimanjaro, ziwa Victoria au mbuga maarufu ya Serengeti na wala sio uzuri wa visiwa vya zanzibar na harufu ya karafuu bali ni mimi na wewe, viumbe pekee wenye jukumu la kuilinda na kuitunza Tanzania, kulinda vilivyokuwepo na tulivyovipoteza.
Hakuna tena mtu kama mzee King Majuto popote pale duniani, hayopo tena Mtu kama Mzee Jengua, Steven Kanumba, Mwalimu Nyerere, John Pombe Magufuri , na wengine wengi ambao majina yao na mchango wao kwa taifa ni mkubwa mno.
Tuache chuki na wivu tuanze sasa kujenga statues za watanzania wenzetu walioipeperusha vyema bendera yetu tukufu na kuiheshimisha na watoto wetu watapata kujifunza kupitia kumbukumbu hizo.
Ahsanteni sana.