Pre GE2025 Uhuru wa Habari: Gazeti la Nipashe Februari 8 kuhusu ARV kuanza kuuzwa halikufika mtaani, kama walikuwa na ushahidi shida ilikuwa wapi?

Pre GE2025 Uhuru wa Habari: Gazeti la Nipashe Februari 8 kuhusu ARV kuanza kuuzwa halikufika mtaani, kama walikuwa na ushahidi shida ilikuwa wapi?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Asubuhi ya Jumamosi Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa aliweka pandiko kwenye account yake ya Insta iliweka lebo kwenye gazeti la Nipashe "SIO KWELI (MISINFORMATION)" na kuongeza maelezo kuwa; PUUZENI UPOTOSHAJI HUU WA TAARIFA ZA DAWA ZA KUFUBAZA VIRUSI VYA UKIMWI (ARV). Dawa haziuzwi, tunazo za kutosha na zikipungua tutanunua zingine. Wananchi msiwe na hofu."

Screenshot 2025-02-10 094113.png

Baada ya hiyo, Wizara ya Afya Tanzania iliweka taarifa ya kusema kuwa uvumi unaosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu ARV kuuzwa ni potofu, na kwamba dawa zipo za kutosha.

Nilipokutana na hiyo taarifa ya Msigwa niliagiza nitafutiwe gazeti nione kilichokuwa kimeandikwa... aisee boda walizunguka kote gazeti hamna, kuna sehemu moja akaambiwa gazeti halijatoka!

Ndio nikaelewa pini lilipigwa kabla magazeti hayajasambazwa kwenye vijiwe, na kama yalifika basi kote taarifa ilifika yasiuzwe.

Najiuliza, mpaka Nipashe wameandika ina maana walikuwa na ushahidi wa claims hizo. Badala ya kuzuia habari hiyo kuchapishwa na kushupasha shingo si wangetumia taarifa hiyo kuweka mambo sawa na kuuelewesha umma kuwa hakuna upungufu wa dawa hizo.

Maonyo 2 yametoka siku mmoja kwenye habari ambazo ukiangalia unashangaa kwanini inatokea hivi. Kadri tunavyosogea kwenye uchaguzi ndivyo vyombo vya habari vinavyozidi kuminywa.

Mkuu, mnataka kila mtu awe kasuku kurudia kile tu ambacho serikali inasema? Gerson Msigwa
 
Nafikiri Nipashe wenyewe ndio wanaweza kueleza iwapo hiyo habari ilichapwa kwenye hard copy na likazuiwa mitaani au kitu gani kilitokea.
Pia badala ya kuomba upatiwe kipande cha gazeti ili kufahamu dawa zipo au hazipo, ungetusaidia kama ungeenda mbele zaidi.

Inashibdikana vipi kuwatafuta wanaotumia au wanaogawa hizo dawa ili kuthijitisha kwamba hizo dawa hazipo au kwanini usiende pharmacy ukanunue ili ubaini uongo wa Msigwa na ukweli wa Nipashe?
 
Nafikiri Nipashe wenyewe ndio wanaweza kueleza iwapo hiyo habari ilichapwa kwenye hard copy na likazuiwa mitaani au kitu gani kilitokea.
Pia badala ya kuomba upatiwe kipande cha gazeti ili kufahamu dawa zipo au hazipo, ungetusaidia kama ungeenda mbele zaidi.

Inashibdikana vipi kuwatafuta wanaotumia au wanaogawa hizo dawa ili kuthijitisha kwamba hizo dawa hazipo au kwanini usiende pharmacy ukanunue ili ubaini uongo wa Msigwa na ukweli wa Nipashe?
😂 😂 unataka uthibitisho gani na gazeti halitoka, lingetoka ningelipata.... wenye kazi yao walifanya reseach yao majibu yameminywa, nimeshawasadia kuwaletea hapa sasa unajua pumba na mashudu
 
Ni tishio la usalama wa Taifa

Tulipaswa kuwa na ma spy kwenye circle ya Trump ili kubaini sera zake kabla hajawa raisi zitaiathiri vipi bongo☺️


Kisha tungejiandaa mapema
NB: Mimi ni mpenzi wa drama haya mawazo yangu ni ya kufikirika tu kwa sababu naangalia movie nyingi

Wenzetu kabla mtu hajawa raisi ktk taifa lake hufanya tathmini kuona kama atahatarisha usalama wao kulingana na sera zake
 
Ni tishio la usalama wa Taifa

Tulipaswa kuwa na ma spy kwenye circle ya Trump ili kubaini sera zake kabla hajawa raisi zitaiathiri vipi bongo☺️


Kisha tungejiandaa mapema
NB: Mimi ni mpenzi wa drama haya mawazo yangu ni ya kufikirika tu kwa sababu naangalia movie nyingi

Wenzetu kabla mtu hajawa raisi ktk taifa lake hufanya tathmini kuona kama atahatarisha usalama wao kulingana na sera zake
Vice versa is true wao wanaweza hilo kuliko sisi wazee wa kuchomana.
 
Kama sisi ni nchi huru na hatuwezi hata kununua au kutengeneza dawa tu kwa ajili yetu wenyewe kujitibu badala yake tunategemea taifa/nchi fulani nje huko litibu magonjwa yetu, basi iko shida fulani kubwa sana ktk vichwa vya viongozi wetu ktk kupanga mipango ya nchi yetu...

Tunashindwa nini kualika wawekezaji wa viwanda vya madawa haya na kuwapa incentives za kutosha ili wao watengeneze dawa hizo hapa hapa nchini na sisi tukazipata kwa bei ya chini 10× zaidi kuliko tunavyonunua sasa..?

Uongozi chini ya serikali hii ya CCM ni wazi kuwa umechoka sana na hauna mawazo mema yoyote kwa ajili ya ustawi wa wananchi. Mabadiliko yanahitajika...

Donald Trump kapiga chafya kidogo tu huko, viongozi wa serikali za wajinga na masikini wa mawazo na mipango nyingi za ki - Afrika wanaanza kulialiia kana kwamba yeye Donald Trump anaongoza taifa/nchi iliyo ktk sayari nyingine wakati wote tuko hapahapa duniani tuliogawiwa na Mungu kila moja rasrimali asili zake za kumfanya aishi na kustawi..

Kama ni hivyo, ikawaje wao waweze kujihudumia na kujitosheleza na sisi tushindwe huku Mungu akiwa ametupa kila rasrimali tunayohitaji: Ardhi, watu, maji, hewa, anga, miti, madini, mbuga za wanyama nk nk..??

Tujiulize wote: Shida iko wapi...?

MAJIBU YA SWALI HILI NI KUWA, haina shaka yoyote kuwa shida au tatizo ni: UWEPO WA UONGOZI WA HOVYO na SIASA CHAFU zinazozaa matatizo kama rushwa, ufisadi, urasimu, ubinafsi wa viongozi kujifikiria na kujipenda wenyewe na matumbo yao badala ya watu wanaowaongoza...
 
Vice versa is true wao wanaweza hilo kuliko sisi wazee wa kuchomana.
Unakuta watu wanashangilia ushindi wa Trump kwenye uchaguzi wa marekani tena wabongo kabisa kama vile ni mpira wa simba na yanga bila kujua sera zake zitaathiri vipi nchi yetu

Ni muda sasa wa nchi yetu kuweka majasusi ktk nchi zote tunazonufaika nazo ktk namna yeyote ikiwemo misaada ili kupata intelijensia, kupredict sera za mlengwa na nammna tutakavyo jipanga sio kusubiri mambo yaharibike kama hivi ndio tuanze kupanic

Nchi isijikite kuangalia usalama wa ndani tu tunahitaji na level za kimataifa

Watu wanajua kushabikia tu hawashirikishi bongo zao


Si unaona wenzetu Rwanda
 
Unakuta watu wanashangilia ushindi wa Trump kwenye uchaguzi wa marekani tena wabongo kabisa kama vile ni mpira wa simba na yanga bila kujua sera zake zitaathiri vipi nchi yetu

Ni muda sasa wa nchi yetu kuweka majasusi ktk nchi zote tunazonufaika nazo ktk namna yeyote ikiwemo misaada

Nchi isijikite kuangalia usalama wa ndani tu tunahitaji na level za kimataifa


Si unaona wenzetu Rwanda
Mkuu sikio la kufa mkuu tuyaache tu.
 
Nmeshafafanua
Kusema ni usalama wa taifa hujatoa ufafanuzi Mkuu, na ndicho hicho kinachotumiwa na serikali kuminya uhuru wa kupata taarifa.... Kwenye The Johannesburg Principles on National Security, Freedom of Expression and Access to Information ambayo Tanzania ni moja kati ya nchi iliyosaini makubaliano hayo kuwa itaheshimu... imeeleza vizuri kuwa taarifa itahesabika kama tishio kwa usalama wa taifa endapo;

1739177180075.png


Na haitakuwa legit endapo dhumuni ni kuserve interest za watu wachache au kuilinda serikali kutokana na aibu baada ya kuboronga sehemu, ambapo we all know hii ndio sababu kubwa.

1739177281782.png
 
Ni tishio la usalama wa Taifa

Tulipaswa kuwa na ma spy kwenye circle ya Trump ili kubaini sera zake kabla hajawa raisi zitaiathiri vipi bongo☺️


Kisha tungejiandaa mapema
NB: Mimi ni mpenzi wa drama haya mawazo yangu ni ya kufikirika tu kwa sababu naangalia movie nyingi

Wenzetu kabla mtu hajawa raisi ktk taifa lake hufanya tathmini kuona kama atahatarisha usalama wao kulingana na sera zake
Tungekuwa smart hivyo tusingeachia huu uholelaholela hadi Mzee Trump auone na kuugeuza fimbo ya kutuchapia.Uzoefu au ukongwe ni hazina na wamarekani wameiibua hazina yao na itawasaidia kweli kweli.Ila tuliolala na kusinzia tutakoma kweli kweli.Hivisasa ni rasharasha,ikifika muda warashasha mbivu na mbichi ya athari zitakuwa hadharani.Badala ya kufarijiana hivi sasa ni vyema mikakati ya haraka,ya uwazi na ukweli ikaanza bila kuchelewa.Iwapo tuna ndoto kuwa kizuizi ni cha miezi mitatu tu na tukaendelea kumbonji.Babu ana maono huenda tukaingizwa kwenye list ya kununuliwa ama kuhamishwa kwani ataamini hatujiwezi.Nihayo tu kwa sasa.Kwa sasa nikiwa safarini Bukavu.
 
Unakuta watu wanashangilia ushindi wa Trump kwenye uchaguzi wa marekani tena wabongo kabisa kama vile ni mpira wa simba na yanga bila kujua sera zake zitaathiri vipi nchi yetu


Si unaona wenzetu Rwanda
Kwa hiyo ulitaka kila mtu amsupport Kamala Harisi kisa tu sera zake za ki pro-globalist ni rafiki sana kwa nchi zetu za dunia ya tatu hizi ambazo zimejaa viongozi wavivu, warafi,wezi, wazembe na ambao hawana maarifa au??

Kwamba unaona wote wanaomsapoti Trump ni hamnazo kisa tu kasitisha misaada na badala yake nyie ambao mnachukizwa na sera zake ndio mna akili?

Wewe una mentality za kimaskini na hata akili zako ni duni sana kama viongozi wako.

Trump is Godsent leader aliyekuja kuwatoa usingizi nyie wajinga mliozoea kuishi dependent life miaka nenda miaka rudi.
 
Back
Top Bottom