Kilichofuata baada ya kupatikana uhuru ilikuwa ni kukamatwa, kuwekwa kizuizini na kuhamishwa kwa masheikh na Waislamu wengine waliodhaniwa kuwa wanapinga utawala wa Nyerere.
Mashuhuri miongoni mwao walikuwa: Abdillah Schneider Plantan, Sheikh Abdulkarim Abdulwahid, Maalim Popo Saleh, Suleiman Masudi Mnonji, Ali Migeyo, Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Sharff Hussein Badawiy, Shariff Mwinyibaba na Shariff Adnan
Wengine ni Bilali Rehani Waikela, Sheikh Jumanne Bias, Maalim Matar, Abdalah Mwamba, Sheikh Hashim Haji Abdallah, Sheikh Nurdin Hussein, Salum Abdallah Popo, Sheikh Mzee Ali Comoriam, Sheikh Al Amin Maftah, Rajab Kiguu cha Mbuzi na wengine wengi.
Lakini ukweli ulikuwa kwamba si wote katika wale waliokamatwa na kuwekwa kizuizini walijihusisha na siasa. Baadhi yao walikamatwa kwa sababu tu walikuwa wakishirikiana na wale waliodhaniwa ni wapinzani wa Nyerere.
Maalim Matar na Shariff Adnan walifungwa jela kwa sababu tu walihusika na msikiti wa Badawiy mjini Dar es Salaam ambako Sheikh Hassan bin Amir, wakati huo akichukuliwa kuwa ndiyo roho ya waumini wa Tanganyika, alikuwa ikiendesha madrasa yake kila magharibi pale msikitini.
Shariff Hussein na nduguye Mwinyibaba walihamishiwa Kenya, walikotoka si kwa sababu walikuwa wamejishughulisha katika harakati za kuipinga serikali, ila lakini kwa sababu walikuwa waangalizi wa msikiti wa Badawiy.
Sheikh Mzee Ali Comorian alitiwa kizuizini kwa sababu kila mara alikuwa akifuatana na Sheikh Hassan bin Amir kama vile alikuwa kivuli cha sheikh. Huenda kile kilichomfanya Nyerere kuwatia kizuizini masheikh na wengine kuhamishwa ni kufuata ule msemo wa Biblia usemao, 'yule ambae hayuko nasi basi ni dhidi yetu'.
Jinsi siasa na za Tanzania zilivyobadilika na jinsi Nyerere alivyoanza kuonesha uadui dhidi ya Waislamu kulimsikitisha sana Abdulwahid. Alishindwa kuelewa uhasama huu ulikuwa unatoka wapi. Alihisi kuwa anahusika na yale yaliyokuwa yanawapata Waislamu. Mawazo haya yalimzonga kama jinamizi. Kwa ufahamu wake alikuwa akidhani matatizo yote ya udini walikuwa wameyashinda toka miaka ya 1950. Mwaka 1953 Abdulwahid akiwa Muislamu na akiungwa mkono na Al Jamiatul Islamiyya aligombea kiti cha urais wa TAA na Nyerere, Mkatoliki.
Abdulwahid alishindwa uchaguzi ule. Waislamu hawakuuchukulia uchaguzi ule kama uchaguzi kati ya Muislamu na Mkristo. Kilichotazamwa ni uwezo wa wagombea.
Mashuhuri miongoni mwao walikuwa: Abdillah Schneider Plantan, Sheikh Abdulkarim Abdulwahid, Maalim Popo Saleh, Suleiman Masudi Mnonji, Ali Migeyo, Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Sharff Hussein Badawiy, Shariff Mwinyibaba na Shariff Adnan
Wengine ni Bilali Rehani Waikela, Sheikh Jumanne Bias, Maalim Matar, Abdalah Mwamba, Sheikh Hashim Haji Abdallah, Sheikh Nurdin Hussein, Salum Abdallah Popo, Sheikh Mzee Ali Comoriam, Sheikh Al Amin Maftah, Rajab Kiguu cha Mbuzi na wengine wengi.
Lakini ukweli ulikuwa kwamba si wote katika wale waliokamatwa na kuwekwa kizuizini walijihusisha na siasa. Baadhi yao walikamatwa kwa sababu tu walikuwa wakishirikiana na wale waliodhaniwa ni wapinzani wa Nyerere.
Maalim Matar na Shariff Adnan walifungwa jela kwa sababu tu walihusika na msikiti wa Badawiy mjini Dar es Salaam ambako Sheikh Hassan bin Amir, wakati huo akichukuliwa kuwa ndiyo roho ya waumini wa Tanganyika, alikuwa ikiendesha madrasa yake kila magharibi pale msikitini.
Shariff Hussein na nduguye Mwinyibaba walihamishiwa Kenya, walikotoka si kwa sababu walikuwa wamejishughulisha katika harakati za kuipinga serikali, ila lakini kwa sababu walikuwa waangalizi wa msikiti wa Badawiy.
Sheikh Mzee Ali Comorian alitiwa kizuizini kwa sababu kila mara alikuwa akifuatana na Sheikh Hassan bin Amir kama vile alikuwa kivuli cha sheikh. Huenda kile kilichomfanya Nyerere kuwatia kizuizini masheikh na wengine kuhamishwa ni kufuata ule msemo wa Biblia usemao, 'yule ambae hayuko nasi basi ni dhidi yetu'.
Jinsi siasa na za Tanzania zilivyobadilika na jinsi Nyerere alivyoanza kuonesha uadui dhidi ya Waislamu kulimsikitisha sana Abdulwahid. Alishindwa kuelewa uhasama huu ulikuwa unatoka wapi. Alihisi kuwa anahusika na yale yaliyokuwa yanawapata Waislamu. Mawazo haya yalimzonga kama jinamizi. Kwa ufahamu wake alikuwa akidhani matatizo yote ya udini walikuwa wameyashinda toka miaka ya 1950. Mwaka 1953 Abdulwahid akiwa Muislamu na akiungwa mkono na Al Jamiatul Islamiyya aligombea kiti cha urais wa TAA na Nyerere, Mkatoliki.
Abdulwahid alishindwa uchaguzi ule. Waislamu hawakuuchukulia uchaguzi ule kama uchaguzi kati ya Muislamu na Mkristo. Kilichotazamwa ni uwezo wa wagombea.