zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 20,537
- 31,729
Intelijensia inaelezwa kama taarifa za siri zinazokusanywa,kuchakatwa na kuchambuliwa ili kuwezesha serikali kuchukua maamuzi fulani ili kuongeza ufanisi. Umuhimu wa intelijensia haupimwi kwa uwezo wa wingi au usiri wa taarifa unaopatikana bali katika uwezo wa zile taarifa kupelekea maamuzi sahihi kufanyika. Kwahiyo kama taarifa nyingi na muhimu zikipatikana lakini maamuzi mabovu yakachukuliwa then intellijensia imefeli.
Tofauti ya Intelijensia na taarifa ni USIRI. Maana taarifa inawezwa kutafutwa kwa uwazi na kusambazwa kwa uwazi ila intelijensia inasakwa kwa usiri mkubwa na kusambazwa kwa usiri sana.
Vyombo vya habari kwa miaka mingi vinaonekana kama nyenzo tu ya taarifa ambazo zinapatikana kwa raia yeyote hivyo hazina madhara kwenye ujasusi. Lakini kitu ambacho wengi hawafahamu ni kwamba mataifa mengi yanatumia vyanzo vya habari kama maeneo ya kusaka taarifa za siri dhidi ya maadui wa nchi au viashiria vyenye hatari au faida kwa nchi hasa kiuchumi.
Moja ya mfano mkubwa kabisa ni shirika la utangazaji la Uingereza (BBC) ambalo kwa miaka mingi sasa linatumika kama kiwanja cha kusaka taarifa za kijasusi ulimwengu mzima na kusukuma mbele propaganda za taifa lao kwa ajili ya maslahi mapana ya kiuchumi na kisiasa.
Kwenye vita ya pili ya dunia BBC ilitumika kama chanzo cha kusaka taarifa muhimu kutoka uwanja wa vita hasa kwa kunasa mawasiliano ya majeshi ya Axis (Germany,Japan na Italia) na kuzituma kwenye wizara ya ulinzi/Habari ili waweze kufanya maamuzi ya kijeshi.
Media za Tanzania hazipo kiutafiti bali kutoa taarifa tu na hapa ndio inanisukuma kuandika uzi huu. Ni mara chache sana unakuta media za Tanzania zinaleta habari za kiuchunguzi ukiachana na wachache kama enzi hizo Mama Terry au Jerry Muro,Kubenea,Jesse kwayu etc lakini TBC ambayo ndio inajukumu kuu kuwa media leader sababu ni chombo cha umma kinapwaya sana hapa. Habari nyingi unakuta ni za Warsha,makongamano,hotuba etc ila ni ngumu kukuta taarifa za kiuchunguzi kutoka kila kona ya dunia.
Angalau Media za Kenya mfano KTN na Citizen nimeona wamejitahidi katika eneo hili. Wanakua na habari za kiuchunguzi nyingi ambazo wanazileta kwenye kadamnasi na zingine kwa siri kusaidia vyombo vya ulinzi kuchukua hatua.
Nimewahi ona documentary moja kuhusu utesaji kwenye sober house (Eneo la kutibu kisaikolojia walioacha vilevi mbalimbali) yaani wamevaa kamera za siri na vinasa sauti na mwingine kujifanya teja yote ili wakusanye taarifa na mwisho wa makala wakapata taarifa muhimu ambazo baada ya documentary ile watu walitumbuliwa na serikali kuweka usimamizi mkali wa hizo sober house.
Investigative journalism juu ya kifo cha saitoti
Tukirudi Tanzania media nyingi sana zimekalia kutafuta habari za umbea,udaku,ngono etc ilihali nchi ina vivutio,taarifa za kutisha na kustaajabisha kabisa ambazo zingeletwa kwenye jicho la umma lingesaidia hatua nyingi kuchukuliwa. Lakini ukiingia youtube, channel 90% ni za udaku kuhusu video za menina!!, sasa kwa staili hii tutajuaje chanzo cha ukimwi kusambaa, Ajira kukosekana, Kilimo kukosa tija n.k ilihali vyombo vya habari haviingii ndani kuchimba kupata taarifa za kina.
Kwahiyo niseme tu kuna uhusiano mkubwa kati ya Vyombo vya habari na intelijensia hivyo ningeshauri hasa TBC ijikite kwenye kutafuta taarifa za kina zenye tija kwa taifa kuliko kukamia kwenye propaganda za kisiasa.
Dunia ya sasa imehama kutoka vita za kisiasa kuelekea za kiuchumi na teknolojia. Sasa TBC ilipaswa ifanye propaganda za kiuchumi kwa kuiuza Tanzania kwa dunia kuhusu taarifa za kustaajabisha mfano kikombe cha babu enzi zile ili Tanzania angalu inufaike na utalii au wawekezaji n.k kuliko kudeal na habari za kisiasa tu zisizo leta faida yeyote kwa taifa. Wajifunze kwa BBC ambayo ni zaidi ya media ya kawaida.
Naomba kuwasilisha
Cc: Malcom Lumumba Kiranga Mshana Jr Chige Wick Daimler Richard lifecoded mtu chake mpite huku.
Tofauti ya Intelijensia na taarifa ni USIRI. Maana taarifa inawezwa kutafutwa kwa uwazi na kusambazwa kwa uwazi ila intelijensia inasakwa kwa usiri mkubwa na kusambazwa kwa usiri sana.
Vyombo vya habari kwa miaka mingi vinaonekana kama nyenzo tu ya taarifa ambazo zinapatikana kwa raia yeyote hivyo hazina madhara kwenye ujasusi. Lakini kitu ambacho wengi hawafahamu ni kwamba mataifa mengi yanatumia vyanzo vya habari kama maeneo ya kusaka taarifa za siri dhidi ya maadui wa nchi au viashiria vyenye hatari au faida kwa nchi hasa kiuchumi.
Moja ya mfano mkubwa kabisa ni shirika la utangazaji la Uingereza (BBC) ambalo kwa miaka mingi sasa linatumika kama kiwanja cha kusaka taarifa za kijasusi ulimwengu mzima na kusukuma mbele propaganda za taifa lao kwa ajili ya maslahi mapana ya kiuchumi na kisiasa.
Kwenye vita ya pili ya dunia BBC ilitumika kama chanzo cha kusaka taarifa muhimu kutoka uwanja wa vita hasa kwa kunasa mawasiliano ya majeshi ya Axis (Germany,Japan na Italia) na kuzituma kwenye wizara ya ulinzi/Habari ili waweze kufanya maamuzi ya kijeshi.
Media za Tanzania hazipo kiutafiti bali kutoa taarifa tu na hapa ndio inanisukuma kuandika uzi huu. Ni mara chache sana unakuta media za Tanzania zinaleta habari za kiuchunguzi ukiachana na wachache kama enzi hizo Mama Terry au Jerry Muro,Kubenea,Jesse kwayu etc lakini TBC ambayo ndio inajukumu kuu kuwa media leader sababu ni chombo cha umma kinapwaya sana hapa. Habari nyingi unakuta ni za Warsha,makongamano,hotuba etc ila ni ngumu kukuta taarifa za kiuchunguzi kutoka kila kona ya dunia.
Angalau Media za Kenya mfano KTN na Citizen nimeona wamejitahidi katika eneo hili. Wanakua na habari za kiuchunguzi nyingi ambazo wanazileta kwenye kadamnasi na zingine kwa siri kusaidia vyombo vya ulinzi kuchukua hatua.
Nimewahi ona documentary moja kuhusu utesaji kwenye sober house (Eneo la kutibu kisaikolojia walioacha vilevi mbalimbali) yaani wamevaa kamera za siri na vinasa sauti na mwingine kujifanya teja yote ili wakusanye taarifa na mwisho wa makala wakapata taarifa muhimu ambazo baada ya documentary ile watu walitumbuliwa na serikali kuweka usimamizi mkali wa hizo sober house.
Investigative journalism juu ya kifo cha saitoti
Tukirudi Tanzania media nyingi sana zimekalia kutafuta habari za umbea,udaku,ngono etc ilihali nchi ina vivutio,taarifa za kutisha na kustaajabisha kabisa ambazo zingeletwa kwenye jicho la umma lingesaidia hatua nyingi kuchukuliwa. Lakini ukiingia youtube, channel 90% ni za udaku kuhusu video za menina!!, sasa kwa staili hii tutajuaje chanzo cha ukimwi kusambaa, Ajira kukosekana, Kilimo kukosa tija n.k ilihali vyombo vya habari haviingii ndani kuchimba kupata taarifa za kina.
Kwahiyo niseme tu kuna uhusiano mkubwa kati ya Vyombo vya habari na intelijensia hivyo ningeshauri hasa TBC ijikite kwenye kutafuta taarifa za kina zenye tija kwa taifa kuliko kukamia kwenye propaganda za kisiasa.
Dunia ya sasa imehama kutoka vita za kisiasa kuelekea za kiuchumi na teknolojia. Sasa TBC ilipaswa ifanye propaganda za kiuchumi kwa kuiuza Tanzania kwa dunia kuhusu taarifa za kustaajabisha mfano kikombe cha babu enzi zile ili Tanzania angalu inufaike na utalii au wawekezaji n.k kuliko kudeal na habari za kisiasa tu zisizo leta faida yeyote kwa taifa. Wajifunze kwa BBC ambayo ni zaidi ya media ya kawaida.
Naomba kuwasilisha
Cc: Malcom Lumumba Kiranga Mshana Jr Chige Wick Daimler Richard lifecoded mtu chake mpite huku.