Uhusiano ulioanzia kwenye Mtandao wa Craigslist wadaiwa kumfanya binti Mkenya apotee kusikojulikana

Uhusiano ulioanzia kwenye Mtandao wa Craigslist wadaiwa kumfanya binti Mkenya apotee kusikojulikana

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
IMG_3189.JPG
Irene Gakwa ni binti aliyezaliwa nchini Kenya miaka 33 iliyopita ambaye mwaka 2019 alihamia nchini Marekani akiwa na ndoto za kusomea maswala ya afya.

Irene alikutana na upinzani mkubwa kwenye hatua za awali za uamuzi wake huu kutoka kwa wazazi wake ambao hawakutaka ahamie huko, lakini kutokana na uwepo wa baadhi ya ndugu zake nchini Marekani, wazazi wake waliamua kumruhusu ili aende kupigania ndoto yake hii kubwa.

"Hakikisha unakunywa maziwa ya moto kisha pumzika" ni sentensi ya mwisho ya baba yake akizungumza na Irene february 24, 2022 akiwa Nairobi.

Baada ya hapo sauti ya Irene haijawahi kusikika tena.

Tukio hili lilianzaje?
Baada ya kuhamia Marekani, Irene Munga aliishi kwa kaka zake Chris Munga na Kennedy Wainaina kwenye mji wa Idaho city - Meridian.

Hapo ndipo alipokutana na Nathan Hightman (39) kisha kuwa wapenzi. Uhusiano wao ulianzia kwenye mtandao wa Craigslist unaohusika na matangazo ya ajira, nyumba pamoja na bidhaa zingine.

Wapenzi hawa walianza kuishi pamoja pasipo wazazi wake Irene kufahamu.

Mashaka yalianza kuibuka mwanzoni mwa mwezi wa pili baada ya wazazi wake kupokea jumbe kadhaa kupitia mtandao wa WhatsApp zikisema kuwa amekuwa hapatikani kwa sababu alidondosha simu yake kwenye maji, aidha ujumbe mwingine uliandikwa kuwa " Nataka tu mfahamu kuwa wewe (baba) na mama ninawapenda sana"

Kwanini tusizungumze kwa video ya WhatsApp kama tulivyo zoea? Baba yake aliwaza sana, hata hivyo hakupata majibu.

Kati ya Mwezi February hadi Machi, Hightman alihamisha zaidi ya Tsh 8.6M kutoka kwenye akaunti ya benki ya Irene kwenda kwenye akaunti yake binafsi. Pia alifanya manunuzi ya zaidi ya milioni 7.5 kwa kutumia kadi ya benki ya Irene kwenye supermarket moja, kwa mujibu wa ripoti ya polisi wanao fuatilia kisa hiki.

IMG_3188.JPG

Nathan Hightman
Hightman ambaye ni mtuhumiwa wa kwanza ambaye ametajwa na polisi kama "mtu mwenye maslahi kwenye kesi hii" yupo nje kwa dhamana baada ya kulipa kiasi cha Tsh 23M.

Kesi hii itasikilizwa tena mwezi Novemba mwaka huu.

Jitihada kadhaa zimefanywa na ndugu zake ikiwemo kutembelea vyumba vya kuhifadhia maiti mahospitalini, kwenda kwenye maeneo ya ombaomba wasio na makazi, kufanya maandamano pamoja na kuanzisha tovuti maalumu yenye jina la whereisirene.com lakini vyote havijazaa matunda.

Hightman anatuhumiwa pia kubadilisha nywila za benki pamoja na kufuta Barua pepe ya Irene. Kwa mujibu wa polisi, mambo haya yote yalifanyika kupitia IP address zinazo husianishwa naye.

Wasiwasi unazidi kuwa mkubwa kwa kuwa binti huyu hakuwahi kumtambulisha Nathan kwa wazazi wake ambao kwa sasa hawajui wataanzia wapi kumtafuta.

Utetezi wa awali wa Nathan unaonesha kuwa yeye pia hafahamu aliko binti huyo, na kuhusu kuhamisha pesa kutoka benki amesema alifanya hivyo kama njia ya kumfanya arudi kuzichukua pesa zake ili waweze kuonana tena.

CNN
 
Muda waliokua wanaishi na huyu jamaa kwai kaka zake hawakujua maana hapo kabla si alikua kwa kaka zake
 
Mimi mawazo yangu yote yapo kwenye Hilo Limwili la Jamaa na Mwili wa Mwanamke ulivyo. Usikute Kammeza [emoji1787][emoji23]
Hawa hawajali ilimradi ni mzungu, hasa hawa mabinti wa hiyo nchi ya jirani ni desperate sana na wazungu
 
US kuna watu wana mambo ya ajabu sana. Unaweza kuta hili jamaa lina tatizo la kiakili na linawinda wanawake wa type ya huyu dada kwaajiri ya kuwaua na kuficha ushahidi. Siku likikamatwa unakuta linatiwa hatiani kwa mauwaji ya wanawake 70+.

Mtu kama huyu unakuta hana marafiki, mademu hawamuelewi, yupo yupo tu so anakuwa depressed anakosa furaha so anakuwa kama na kisasi cha chini chini anatarget watu wa kundi fulani la wanajamii ili tu kupata hobby ya kufanya kwa usiri.

Jamaa linaonekana kabisa haliko sawa kiakili.

Dada zetu nao kushobokea ngozi nyeupe, sasa ndio mtu gani huyu wa kuwa nae mtu kakaa kama chura usoni?!


Inasikitisha sana. Mademu wa kiafrika acheni shobo na ngozi nyeupe, komaeni na asili yenu at least tukitaka kuwaua tunapiga mkwara hata mara kumi na hapo ni mnakuwa m'metukorofisha kweli kweli yaani ile ya kufika point ya kuchoka kuwavumilia tena. Ila haya majitu linaweza kukuua kwasababu zake binafsi tu, yaani unaweza kuta linajiskia raha kuona mwanamke analia wakati lina mkata kata mwili na anatoka damu.

Majitu yana roho mbaya haya mashetani kabisa.

Dada zetu rudini tu huku afrika tutawalegezea masharti ya kuwaoa ili tuwastili ila nanyie mtulie sasa mkikaa na sisi. Sisi tutavumilia kero ndogo ndogo ila maswala ya kujihusisha na wanaume wakati upo kwenye mahusiano serious walahi mtatuona wabaya tutawanyuka kisawa sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa hawajali ilimradi ni mzungu, hasa hawa mabinti wa hiyo nchi ya jirani ni desperate sana na wazungu
Mademu wa Kenya wapo so brainwashed sana na uzungu. Anaweza olewa na mzungu hana hata mia na akawa very happy sababu ya kuwa ameingia mahusiano na mzungu ila akamletea dharau mwafrika mwenzake ambaye anamsapoti kwnye mahitaji na anamjali.

Vina ubaguzi fulani wa rangi maana vinachukia uafrika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wazungu wanapenda sana kuteka na kuhifadhi sehemu za maandaki .
kuna muvi nyingi zinaeleza sana haya matukio yaliyopo USA.

katika sehemu inatisha ni USA.
kila baada ya lisaa watoto utekwa sana sana wa kike ndio waanga. yani kiufupi mda mwingi ni kuwa makini na mwanao.

Kila baada ya nusu saa watoto walio barehee wakike utekwa ili kufanyishwa biashara ya ngono kwenye madanguro.

kila baada ya mwezi polisi uweza kuokoa wanawake waliofungiwa ndani ya majumba chini ya maandaki wakifanyiwa vitendo vya ngono.


ila uzuri wa wenzetu si rahisi habari kuwa vuvuzera kama kufatilia nchi za wengine
 
Huwa naangalia sana FBI Files hao jamaa wanajua kupeleleza.
 
Back
Top Bottom