Katika maeneo lisilofahamika, zinaonekana Jet fighters za Uingereza na Marekani zikirushwa kuelekea eneo ambalo kundi la kigaidi la Hauthi kutokea Yemen lilikoweka kambi.
Kundi la Hauthi limeleta kashi kashi katika Mwambao wa bahari ya Sham (Red Sea) na kupelekea Meli zinazokatiza bahari hiyo kwenda Ulaya na Asia kukatisha safari au na nyinginezo zikiamua kuzunguka bahari ya Atlantic ili ziweze kwenda Asia. Kitendo kilichokwamisha Biashara ya usafirishaji katika Mwambao huo wa bahari ya shamu unaounganisha Bara la Afrika na bara la Asia lenye nchi za kiarabu linaloitwa Mashariki ya kati.
Hivi karibu kundi la kigaidi la Hauthi lilianzisha harakati za kivita kupambana na Israel kama jitihada za kusaidia kundi la Hamas la nchini Palestina.
USA walipotoa ile meli ya kivita kwa kuogopa isije ikalipuliwa wakapata hasara huko Red Sea nilijua kitakachofatia watatuma ndege za kivita kwanza hao jamaa wa Yemen wanadanganywa na Iran kutaka kushindana na Wababe wangetulia tu kuliko hii hali inakokwenda sio kabisa...