Uingereza yatoa zaidi ya dola za Marekani mil. 13 kusaidia kilimo nchini

Uingereza yatoa zaidi ya dola za Marekani mil. 13 kusaidia kilimo nchini

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
David%20Mathayo(1).jpg

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk. David Mathayo.


Serikali ya Uingereza imetoa dola za Marekani milioni 13.4 kwa ajili utekelezaji wa mradi mkubwa wa kilimo nchini.

Serikali ya Uingereza imekabidhi fedha hizo kwa shirika lisilokuwa la kiserikali la BRAC-Tanzania, ambalo litasimamia utekelezaji wa mradi huo wa miaka 4, ambao umepewa jina la Lead.

Mradi huo uliozinduliwa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk. David Mathayo, unatarajiwa kutekelezwa katika mikoa 18 nchini. “Kwa kupitia mradi huu, tunaweza kuzalisha ajira nyingi sana kwa Watanzania, wakulima, wafanyabiashara na wafugaji,” alisema Mathayo wakati wa uzinduzi huo.

Alisema mradi huo utaisaidia serikali ambayo inakabiliwa na uhaba wa fedha kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo ya kilimo ambao ni uti wa mgongo wa taifa.

Mradi huu unalenga kuongeza kipato kwa wakulima, kuwaongezea uwezo wakulima wadogo na kuongeza tija na ufanisi katika sekta nzima ya kilimo, pamoja na kuhakikisha usalama wa chakula. Mathayo alisema mradi utalenga maeneo mawili makuu, kilimo (hasa cha mahindi) na maendeleo ya mifugo.

Katika utekelezaji, alisema mradi utahusisha wakulima wa mifugo 48, 000 katika mikoa husika, na utasaidia kutoa ufumbuzi matatizo ya muda mrefu yanayowakabili wakulima na kuongeza uwezo wa kitaalamu, kuwasaidia kupata masoko ya mazao yao na mbegu bora na zenye viwango.

Balozi wa Uingereza nchini, Diane Melrose, amelielezea shirika la BRAC kama mfano wa kuigwa, hasa katika utekelezaji wa miradi inayowalenga watu maskini ulimwenguni.

Mwanzilishi na Mwenyekiti wa BRAC--International, Afazia Hasan Abed, alisema shirika lake limeshafanya maandalizi ya utekelezaji wa mradi huo, kutoa mafunzo kwa wataalam watakaosaidia wakulima, na kuwakusanya wakulima na wafugaji.

“Ni matumaini yangu makubwa, mradi utasaidia wakulima na Tanzania kupiga hatua katika sekta ya kilimo” alisema.




CHANZO: NIPASHE

 
Hela ndogo sana hiyo ikilinganishwa na madini wanayochukua!
imagine kilo moja tu ya tanzanite inafikia tsh bilion 32!!
hiyo ni kwa kilo moja tu!
sasa tujiulize wanachukua kilo ngapi?!
how much money they make from us?
alafu leo wanajifanya wanatoa msaada tena ni sehem ndogo sana ya hela wanayotengeza!
na sie tunaona ni sawa tu!
na hotuba zetu juu za kuwashukuru!
hata wao wanatung'ong'a nadhani..
 
Huo msaada utatufikiaje wakulima wadogo na marazote nasikiaga misaada kwa wakulima wadogo lakini sijawahi kusikia hata jirani yangu amepata sasa misaada hii inaendaga kenya au uganda?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Huo msaada utatufikiaje wakulima wadogo na marazote nasikiaga misaada kwa wakulima wadogo lakini sijawahi kusikia hata jirani yangu amepata sasa misaada hii inaendaga kenya au uganda?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums


upewe msaada kwani una undugu wowote au
ùrafiki na kiongozi aliye madarakani?
 
Hapo subiri semina makongamano na warsha za mawazri wa fedha kilimo na maendeleo ya jamii baadae wakuu wa mikoa na wa wilaya na wakurugenzi fedha itaisha kabla ya kumfikia hata afisa ugani chezea fisadi wewe chukua chako mapema
 
Back
Top Bottom