Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Siku chache tangu zisambae picha mtandaoni kwamba kuna wagonjwa wanapelekwa hospitalini kwa kutumia matenga huko mkoani Ruvuma, Rais Samia jana ameamu kujibu mapigo.
Akiwa anahutubia jana huko mkoani Ruvuma Samia alisema kuwa anasikitishwa na baadhi ya watendaji wanaokaa kimya pindi taarifa za uongo zinaposambazwa mtandaoni kuhusu serikali na kuwataka watendaji wasisubiri Rais au mawaziri kuja kukanusha badala yake wawe wanakanusha wenyewe.
Samia alifananisha viongozi au watendaji wanaokaa kimya wakisubiri taarifa zinazochafua serikali zikanushwe na Rais au mawaziri kama wanaume wanaokimbia nyumba zao kwenda kwenye nyumba za wanaume kuomba msaada pindi wanapovamiwa na nyoka.
Kwa kweli inafikirisha sana kuona viongozi wetu wanakerwa na mambo petty petty kama maoni ya watu wa mitandaoni.
Nawasilisha!
Akiwa anahutubia jana huko mkoani Ruvuma Samia alisema kuwa anasikitishwa na baadhi ya watendaji wanaokaa kimya pindi taarifa za uongo zinaposambazwa mtandaoni kuhusu serikali na kuwataka watendaji wasisubiri Rais au mawaziri kuja kukanusha badala yake wawe wanakanusha wenyewe.
Samia alifananisha viongozi au watendaji wanaokaa kimya wakisubiri taarifa zinazochafua serikali zikanushwe na Rais au mawaziri kama wanaume wanaokimbia nyumba zao kwenda kwenye nyumba za wanaume kuomba msaada pindi wanapovamiwa na nyoka.
Hii ni sawa na mwanaume kaingia nyoka ndani ya nyumba yako, unatoka mbio unaenda kumuita mwanaume mwenzio, njoo unitolee nyoka nyumbani kwangu. Ujana dume uko wapi hapo?
Kwa kweli inafikirisha sana kuona viongozi wetu wanakerwa na mambo petty petty kama maoni ya watu wa mitandaoni.
Nawasilisha!