Ujasiriamali wa Siasa: Siasa kufanywa ajira ya kudumu na demokrasia ya Tanzania

Ujasiriamali wa Siasa: Siasa kufanywa ajira ya kudumu na demokrasia ya Tanzania

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Wanasiasa wengi wa Tanzania hawana kitu kingine wanaweza kufanya nje ya mfumo wa siasa wakapata kipata kizuri na maisha yao yakaendelea vizuri.

Wengi wanaotoka vyuoni wakajiunga na siasa moja kwa moja hawana principles zozote wanazosimamia zaidi ya maslahi yao tu.

Wanaoacha ajira zao wakajiunga na siasa huwa hawawezi kurudi tena kwenye ajira zao na hivyo kuendelea kufanya kila namna ili wabaki katika mfumo wa siasa.Hao leo wanaweza kusema hivi kesho wakasema vile.

Wafanyabiashara wanasiasa huwa hawapendi kutoka kwenye siasa na biashara zao huyumba sana wanapotoka. Hiyo inawafanya wanang'ang'anie siasa maisha yao yote kulinda biashara zao.Huu ndio unaitwa ujasiriamali wa siasa.

Wanasiasa wetu wengi
1. Hawawezi kuandika vitabu wakauza wakapata kipato.
2. Hawaajiriki nje ya siasa
3. Hawawezi kuanzisha kampuni au biashara zikasimama wakiwa nje ya siasa.

Siasa kuwa sekta inayolipa vizuri nchi hii ni janga kwa ustawi wa Taifa.
 
Tatizo ni mfumo ovu wa CCM, huwezi kumlipa 12M mbunge darasa la 7 kwenda kugonga meza ukaacha mtalaam mwenye degree na laki 7huku hana posho wala mazingira mazuri ya kazi utegemee nchi kupata maendeleo.
 
Umeongea jambo la msingi na maana kubwa ndio maana wahafidhina ndani ya chama tawala hawataki mabadiliko yeyote maana chama ndio ajira yao kwa msingi wa siasa.
Mshahara kwa mbunge ungekuwa 1M bila posho hizi za anasa tungepata wabunge wazuri sn wanaojitolea kutoka ndani ya mioyo yao, mbona kuna wachungaji makanisa wanalipwa posho laki 4 kwa mwezi huku wana degree lakini wanaendesha vizuri sn ibada na kuhudumia jamiii kiroho kwa moyo mmoja?
 
Mtu kama John Mrema, hana kitu nje ya Siasa, aliacha U-MC wa harus na kipaimara, akawa msemaji wa chadema.

Kilichobaki wanajaza wake zao kwenye ubunge wa viti maalum.

Hapo Lucy owenya hatakosa, na yule Mukya
 
U-MC sio kitu?
Mtu kama John Mrema, hana kitu nje ya Siasa, aliacha U-MC wa harus na kipaimara, akawa msemaji wa chadema.

Kilichobaki wanajaza wake zao kwenye ubunge wa viti maalum.

Hapo Lucy owenya hatakosa, na yule Mukya
 
Haipaswi kuwa ajira ya kudumu kama ualimu, udaktari, biashara n.k

Kabla ya kuingia kwenye siasa mtu unapaswa kuwa na uzoefu wa kazi nyingine. Unapokataliwa na wananchi, chama, au wateuaji wa serikali unapaswa kukubali, kukaa pembeni na kujikita kwenye mambo mengine badala ya kufanya vimbwanga.
Siasa pia ni ajira boss.
 
Wanasiasa wengi hawatapenda Hiki ulichoandika. Wafuasi wa wanasiasa wanashangaa Hiki ulichoandika.

Watu wenye akili timamu za kuliona hili ni wachache sana.
 
Kuna tofauti kubwa ya watu wanaofanya siasa lengo lao kuu la kwanza likiwa ni kupata kipato huku lengo la pili likiwa ndio wananchi wenyewe na wanaofanya siasa lengo lao kuu la kwanza likiwa ni kuwatumikia wananchi na la pili likiwa ni kipato.
Siasa pia ni ajira boss.
 
Screenshot_20220819-181849_Twitter.jpg
 
Back
Top Bottom