Ujasusi wa Uturuki 'yamkata makali' mkuu wa kijasusi wa Iraq wa PKK

Ujasusi wa Uturuki 'yamkata makali' mkuu wa kijasusi wa Iraq wa PKK

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
Ujasusi wa Uturuki 'yamkata makali' mkuu wa kijasusi wa Iraq wa PKK.png

Ankara imekuwa ikifanya mashambulizi kadhaa ya kupambana na ugaidi kaskazini mwa Iraq ili kuwaangamiza magaidi. / Picha: Jalada la AA

Hasan, kwa jina maarufu Celal Kaya, aliyetambuliwa kama 'afisa wa Ujasusi' na kundi la kigaidi la PKK nchini Iraq, "amekatwa makali " katika operesheni iliyofanywa na MIT, Shirika la Kitaifa la Ujasusi la Uturuki, katika mji wa Sulaymaniyah nchini Iraq.

Mamlaka ya Uturuki hutumia neno "kukata makali" kumaanisha magaidi wanaohusika aidha wamejisalimisha au wameuawa au kukamatwa.

Kulingana na MIT, Kaya pia ndiye alihusika vikubwa kupanga mauaji ya mwanadiplomasia wa Uturuki Osman Kose huko Erbil mnamo 2019, na alikuwa akifanya kazi kaskazini mwa Iraqi kwa muda mrefu.

Akiwa amehusika katika kuandaa harakati za kundi la kigaidi ndani na nje ya nchi, Kaya alishika wadhifa wa juu katika kile kinachojulikana kama kikundi cha kijasusi cha PKK.

Anasemekana aliongoza mtandao wa wafanyakazi wa kisiri ambao walijihusisha na ujasusi na kutafuta habari kuhusu mitambo na mali ya Uturuki kwa PKK, na kusaidia harakati za kundi la kigaidi dhidi ya vikosi vya usalama vya Uturuki kaskazini mwa Iraq.

Wakiongozwa na Kaya, watendaji hawa pia walihusika katika utekaji nyara wa maafisa wa umma wa Uturuki, ilisema MIT.

MIT imepata uelewa mkubwa juu ya shughuli za siri za ugaidi za PKK kwani imekuwa ikifuatilia takwimu za kiwango cha juu za PKK kupitia mtandao wake wa kijasusi wa ndani.

MIT, ambayo mara kwa mara ilikuwa ikipata habari juu ya Kaya, mara kwa mara ilibadilisha timu yake katika mkoa ili isijulikane. Mpango dhidi ya Kaya ulikuwa ukiendelea kwa muda mrefu.

Katika kampeni yake ya zaidi ya miaka 35 ya ugaidi dhidi ya Uturuki, PKK - iliyoorodheshwa kama shirika la kigaidi na Uturuki, Marekani, na Umoja wa Ulaya - imehusika na vifo vya takriban watu 40,000, ikiwa ni pamoja na wanawake, watoto, na watoto wachanga.
 
Imekuaje Uturuki na ubabe wake wote wa kijeshi imeshindwa kabisa kuwaangamiza PKK ?....bora wazungumze nao tu.

T14 Armata
 
Imekuaje Uturuki na ubabe wake wote wa kijeshi imeshindwa kabisa kuwaangamiza PKK ?....bora wazungumze nao tu.

T14 Armata
PKK haiwezi isha na haitokaa ife labda ibadilike jina. Ukitaka kuua wanamgambo wa Kikurdi basi uwape nchi waishi, hapo katikati ya Turkey, Syria na Iraq ndipo nchi ya Kurdistan ilitakiwa iwepo ila mgawanyo wa wakoloni hasa Waingereza na Wafaransa walipuuza hilo. Mwishowe ikaachwa jamii inayobaguliwa kiimani na kiasili na kila jirani yake ikiwa katikati na haina makazi kila sehemu wanaikataa na kuifukuza.

Kwanza Wakurdi ni wapiganaji wazuri sana. Usumbufu wao ni sawa na usumbufu wa Wayahudi kabla hawajawekwa sehemu moja ya kuita nyumbani.
 
PKK haiwezi isha na haitokaa ife labda ibadilike jina. Ukitaka kuua wanamgambo wa Kikurdi basi uwape nchi waishi, hapo katikati ya Turkey, Syria na Iraq ndipo nchi ya Kurdistan ilitakiwa iwepo ila mgawanyo wa wakoloni hasa Waingereza na Wafaransa walipuuza hilo. Mwishowe ikaachwa jamii inayobaguliwa kiimani na kiasili na kila jirani yake ikiwa katikati na haina makazi kila sehemu wanaikataa na kuifukuza.

Kwanza Wakurdi ni wapiganaji wazuri sana. Usumbufu wao ni sawa na usumbufu wa Wayahudi kabla hawajawekwa sehemu moja ya kuita nyumbani.
Ukweli ni kuwa hakuna atakayewapa nchi nyakati hii (labda wawape madaraka ya ndani tu kama huko Iraq na huenda Syria ikafanya hivyo baadae).

ila hata hapo walipo wanaweza tu kujichanganya na kuishi vizuri tu mfano Rais wa Iraq ni mkurdi, hata huko Uturuki na Iran wapo wanasiasa wakurdi mpaka bungeni.

Erdogan tu ndio anachochea huu mzozo kwa manufaa yake ya kisiasa.
 
Back
Top Bottom