Ujauzito wa jf na majibu ya HIV

Ujauzito wa jf na majibu ya HIV

ma jery

Senior Member
Joined
Jun 15, 2011
Posts
171
Reaction score
65
jamani mnakumbuka kuhusu yule mpenzi wangu wa humu kutokana na hali ya ujauzito nilionao
na swala la kufunga ndoa ,inabidi tupime afya zetu kiukweli naogopa sana jamani nisaidieni naona furaha yangu inapotea ghafla
 
daaaah? Nenda angaza watakupa tu ushauri nasaha kabla na baada ya kupima wana wataalamu pale
 
Pole dada,umetafuta bwana mtandaoni?,ndo madhara yake hayo.Kapime tu.
 
Usiogope kupima ukikutwa unavyo au huna yote ni matokeo cha msingi ujue jins ya kukabiliana nayo
 
kwanza ukiwa mja mzito lazima upime vvu na wewe ulishasema kuwa una ujauzito...na hii ni compasory.....halafu naona huu ujauzito(kama kweli unao) naona kama ulikuwa umepania kweli na umri umekutupa nini maana kila siku thread zako mara jukwaa la doctor mara huku haziishi!!!!

kupima ni muhimu lakini pia siku hizi kuna vipimo waweza kujipa mwenyewe....
 
jamani mnakumbuka kuhusu yule mpenzi wangu wa humu kutokana na hali ya ujauzito nilionao
na swala la kufunga ndoa ,inabidi tupime afya zetu kiukweli naogopa sana jamani nisaidieni naona furaha yangu inapotea ghafla

Jamani! Ina maana tangu ulivyotujuza hali yako na ushauri tuliyokupa ina maana bado ulikuwa hujaenda kwa wataalam? Nenda leo leo maana Mi naona umechelewa mpaka sasa.
 
kwanza ukiwa mja mzito lazima upime vvu na wewe ulishasema kuwa una ujauzito...na hii ni compasory.....halafu naona huu ujauzito(kama kweli unao) naona kama ulikuwa umepania kweli na umri umekutupa nini maana kila siku thread zako mara jukwaa la doctor mara huku haziishi!!!!

Kupima ni muhimu lakini pia siku hizi kuna vipimo waweza kujipa mwenyewe....
vipimo gani nijipime mwenywewe?
 
teh teh teh!!! langu cheko tu lol!! hii ndio JF
 
sasa mama hadi unafikia maamuzi ya kubeba ujauzito nini hasa kinakuogopesha tena nnilitegemea ungekuwa wa kwanza kwenda kupima kabla ya kila kitu kwa ajili ya kupata ushauri nasaha kwa mwana mtarajiwa kama utakuwa umeupata na ndio ufikirie ndoa .. je waona ndoa ys thamani zaidi ya huyo mtoto uliyenaye???
 
Shosti ivi ulimuamini sana huyo bwana au alikueleza nini mpaka ukampa bila kinga? au mlisha pima kabla yakuingia kwenye uwanja wa nipe yote usinibanie? haya chamsingi nenda ukajiangali mama lakini usijali sana tarajia majibu mazuri...
 
shost maadam una kamjusi
huna ujanja wa kukwepa
we kapime tu ujue moja.
 
usiogope mama,nenda tu kapime, kawa mzima Sinta itakuwa wewe!!
 
jamani mnakumbuka kuhusu yule mpenzi wangu wa humu kutokana na hali ya ujauzito nilionao
na swala la kufunga ndoa ,inabidi tupime afya zetu kiukweli naogopa sana jamani nisaidieni naona furaha yangu inapotea ghafla

mlipokuwa mnabebeshana ujawepezi mbona hukutafuta ushauri kwetu kuhusu afya zenu?
 
Pole sana mpendwa,japo ulijirisk sn,kwa kufanya mapenz kabla hamjapima na kujua afya zenu na kupata ushauri,cha msingi tafuta kituo cha kupimia na ukapime kwanza ukiwa peke yako uyajue majibu vyovyote itakavyokuwa utapewa ushauri na uwe mkweli uwaeleze situation kwan kwa namna yoyote km jamaa naye anajali ipo siku atakushika mkono muende wote kupima,na ukishapima na kujijua tafadhali fauata ushauri utakaopewa kulingana na majibu yako na mshauri na mwenzio mkapime wote ili kila mtu ajue afya ya mwenzake.
 
jamani mnakumbuka kuhusu yule mpenzi wangu wa humu kutokana na hali ya ujauzito nilionao
na swala la kufunga ndoa ,inabidi tupime afya zetu kiukweli naogopa sana jamani nisaidieni naona furaha yangu inapotea ghafla
Siku hizi haina ujanja ni kupima tu.
 
We ma jery ,Kwa nini ulianza mahusiano bila kupima.Kwa hali ya sasa si vizuri kuanza mahusiano na mtu bila ya kupima kwanza .Omba sana Mungu na ukapime kwani kama u mjamzito kupima haikwepeki.All the best.
 
Back
Top Bottom