Ujenzi: Kipi kinaanza, plaster au ceiling joists?


Pia itasaidia kuzuia vumbi linalotoka juu kupenya kuja chini
 

..............jibu ni hili hapo juu Ramthods
 
Last edited by a moderator:
hakikisha unakuwepo eneo la tukio kutwa nzima siku za plaster kwani inakula sana cement , unaweza ukaenda tu jioni siku ya kwanza ya kupiga plaster fundi akakuambia kwa leo tu tumetumia mifuko 18 ukarusha ngumi.

Plaster ikila sana cement na render itakuaje?
 
Thax.

Hapo unaposema box ndo sielewi pia.

Ok, iko hivi,...kama nyumba yako ina veranda kwa nje (kibaraza) ambacho kitakuwa kimeshikiliwa na nguzo, basi lazima nguzo zijengwe kwa kusuka nondo na hizo nguzo zitaunganishwa na nyumba kuu kupitia kwenye linta box. Endapo utafanya hivo, ina maana baada ya linta basi itabidi kujengwa tofali ili kufikia usawa wa kupaulia. Hii itafanya kuta za nyumba kuu na kibaraza kuwa kwenye usawa ule ule wa kupaulia. Baada ya kuezekaa (endapo kibaraza hakijamiminwa zege), basi kutakuwa na uwazi unaofanana na box kuanzia pale kwenye linta hadi kwenye ceiling board.

Kwa maelezo hayo kama bado hujanielewa basi itabidi tuwasiliane nikutumia mchoro
 
Kabla ya yote,condrit pipe,then hch unachoita cinling watwat,kimtaa inaitwa blandaring,ndio inafuata thn plaster,kuna mtu ameshakushaur vzr hp juu,bt pipe is tha first!
 
Unapiga zile mbao za 2 x 2, unafata plaster, unamalizia gypsum, cealing board, nk
 
Kabla ya yote,condrit pipe,then hch unachoita cinling watwat,kimtaa inaitwa blandaring,ndio inafuata thn plaster,kuna mtu ameshakushaur vzr hp juu,bt pipe is tha first!

UANDISHI WA HOVYO SANA HUU. Kama utoto vile.
 
Reactions: Kbd
nisaidieni vifaa vya blending na kuweka gipsam HP1 Dengue KakaJambazi Dark City
kuna vifaa vinaitwa kona, mkanda na fiba sivielewi kabisa msaaada
Sista kama sasa ivi upo ndani ya chumba chenye gypsum, ile iliyoshikilia gypsum ukutani ndo mkanda, fiber ni nyusi flani iv zinazotumika kuungia joints za gypsum.

Wengine watakuwekea picha, mi natumia simu.
 
Last edited by a moderator:
Topic nzuri sana. . . . .
1. Mafundi wengi huwa wanataka kazi huyo aliyekuambia muanze plasta ni mason lazima. . . anataka kazi tu mengine hajali. . . . . . .Inategemea sana mtu mwenyewe anavyotaka mambo yake haswa kwenye kupiga blandering yote au kupiga mkanda kwanza. . . . .Ukipiga box zote maana yake conduit phase itakuwa kazi ya mara moja yaani ukutani na juu kabisa. . . . . . .

2. Awamu mbili ni kuwa utaweka mkanda tu then conduit ukutani halafu plasta (baada ya plumbing) ukija piga box zako fundi umeme ndio atapanda juu kwa phase ya pili ya conduit labda na kuvuta nyaya kabisa then board work it be gypsum au tachi

Utashi wa mjenzi tu na mzuka wake saa nyingine wengine wanaanza plumbing na conduits halafu grills na kupiga plasta nje kabisa halafu anakuja ndani for blandering sasa raha yake ni ule muonekano wa nje. . . . .

Si sawa kuanza na plasta kabla ya blandering. . . . .Japo mkanda wa ukutani tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…