Ujenzi meli ya kisasa Ziwa Victoria wafikia asilimia 35

Ujenzi meli ya kisasa Ziwa Victoria wafikia asilimia 35

elivina shambuni

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2018
Posts
461
Reaction score
295
1573581826885.png


UJENZI wa meli mpya ya kisasa Ziwa Victoria umefikia asilimia 35, ambao unatarajia kugharimu Sh. bilioni 86 hadi kukamilika kwake. Hayo yameelezwa juzi jijini Mwanza na Kaimu Mhandisi Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli (Mscl) Mwanza, Abel Gwanafyo, kwa niaba ya ofisa mtendaji mkuu wa huduma hizo.

“Meli hiyo ina uwezo wa tani 400 yakiwamo magari madogo 20 na makubwa matatu na kubeba abiria 1,200, ambayo itakuwa ya kisasa zaidi kuliko meli zingine katika Ziwa Victoria,” alisema Gwanafyo.

Akizungumza katika kongamano la wasaa wa marafiki wa habari mkoani Mwanza, Gwanafyo alisema ujenzi huo ulianza mwaka 2018 na unatarajia kukamilika 2021. Gwanafyo alisema meli hiyo inajengwa na Kampuni ya Ujenzi ya GAS EntecCO Ltd kwa kuungana na Kang Nam Cooperation ya Korea Kusini pamoja na SUMA JKT ya Tanzania.

Aidha, alisema itakuwa na viti vya kisasa zaidi vya kukaa mtu mmoja mmoja kama kwenye ndege, ambayo itafanya safari zake Mwanza kwenda maeneo ya Kemondo, Bukoba, Musoma pamoja na Uganda kupitia Bandari ya Portbell. Pia inaweza kukodiwa na watalii. Alisema itatumia saa chache kukimbia kutoka Bandari ya Mwanza kwenda bandari zingine kuliko meli ya zamani Mv. Victoria inayofanyiwa ukarabatiwa.
 
SONGORO wameonesha uwezo mkubwa sana katika ujenzi wa meli humu nchini. kwanini hajapeaa hii tenda kuliko kuwapa ulaji wa nje? au nabiii.......!

hatahivyo pongezi lwa serikali kuwajali wana wa kanda ya ziwa, changamoto ya meli kwa safarinza bukoba - mwanza natumai zinaenda kubaki historia.
 
Tutegemee kitu kinachoweza kufanana na hiki chombo kikihudumu katika ziwa victoria?. 🥺
Screenshot_2019-11-12 Silver Whisper All-Equipped Luxury Cruise Ship Silversea.png
 
Subiri NYUMBU waje watakuambia sio kipaumbele hicho. Bora wangepewa ruzuku ya SACCOS yao ya UFIPA. Uncle Magu kamatilia hapo hapo mwisho wa siku watakubali hadharani manake sasa hivi wanaumia tu kimoyomoyo.
Una umri gani? Kama hutajali nipe naka CV kako hapa kwa ufupi. THANKS IN ADVANCE
 
Back
Top Bottom