Ujenzi nyumba hizi kutumia miti/mbao unatufaa Tanzania?

Candid Scope

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
11,897
Reaction score
6,925


Nyumba nyingi za Ulaya na Marekani hujengwa kwa mtindo huu, na wakishafunika juu yake kwa makaratasi na maplastic inaonekana bomba sana kumbe ni mbao tu na hata sakafu imesakafishwa kwa mbao.

Ujenzi huu wa gharama nafuu je, unafaa Tanzania kutokana na gharama kubwa za saruji, mchanga na mengineyo?
 
Inategemea ni wapi. Kama ni Moshi Arusha Mbeya na Lushoto zinaweza kufaa kutokana na hali ya hewa kuzikubali. Tatizo ni kwamba usalama hauzikubali maana wezi wataingia kama kwao. Hivyo fikiri kabla ya kuingia mkenge.
 


Badala ya kumaliza miti kwa kuchoma mkaa bora tungeitumia kujenga nyumba kwa mtindo huu kwa gharama nafuu.
 


Ubora kwa nchi za tropic na dhoruba tuzijuavyo nyumba aina hii inaweza kuhimili misukosuko ya hali ya hewa?
 
Inategemea ni wapi. Kama ni Moshi Arusha Mbeya na Lushoto zinaweza kufaa kutokana na hali ya hewa kuzikubali. Tatizo ni kwamba usalama hauzikubali maana wezi wataingia kama kwao. Hivyo fikiri kabla ya kuingia mkenge.

Hilo neno, maana ni msumeno tu inatosha jamaa kujitosa ndani. Majuu usalama kidogo ni mzuri kwa maana kwamba litokeapo jambo vyombo vya usalama hutumia pungufu ya dakika kumi kufika eneo la hatari, kwa bongo masaa zaidi ya mawili usalama hatarini.
 
Huku kwetu mbao ni more expensive than cement I guess.

Hao wanajenga hivyo pia kwa ajili ya vimbunga kule kwao si unajua ikija Tornado hata mbao zikikudondokea ni afadhali kuliko kuporomokewa na zege.
 
Mkuu umeleta wazo zuri, ila kwa wakati huu na bei za mbao zilivyopanda kujenga nyumba kama hii ni ya gharama kubwa kuliko tunavyofikiri. Ni afadhal mtu kama uwezo wake ni mdogo, afikirie angalau kutumia tofali za kuchoma kwani bei yake sio mbaya sana.
 

mchwa teh teh
 
ni wazo zuri ila sio cost effective kwa sasa, mbao expensive sana pia kuna issue ya moto....
waakti wenzetu wana bima ya nyumba na zimamoto zao nzuri sie hatuna bima halafu kuna short za umeme wako, moto wa jirani, wa magari yalioacha njia etc na zima moto zetu unaita gari inakuja baada ya saa mbili na usaini cheque 5ml uhudumiwe..... mie naona njia mbadala kama alivyopendekeza mdau hapo juu tofali za kuchoma au hydrafoam....
 

Kwenye red hata hizo za tofali moto ukiwaka zitaungua tuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…