Ujenzi wa Maabara Tatu za Masomo ya Sayansi Kwenye Kila Sekondari ya Kata Unaendelea Vizuri: Musoma Vijijini

Ujenzi wa Maabara Tatu za Masomo ya Sayansi Kwenye Kila Sekondari ya Kata Unaendelea Vizuri: Musoma Vijijini

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

UJENZI WA MAABARA TATU ZA MASOMO YA SAYANSI KWENYE KILA SEKONDARI YA KATA UNAENDELEA VIZURI

Jimbo la Musoma Vijijini lenye Kata 21 kwa sasa lina Sekondari 26 za Kata na 2 za Madhehebu ya Dini. Ujenzi wa Sekondari mpya 11 unaendelea kwenye baadhi ya Kata.

Ujenzi wa maabara tatu za masomo ya sayansi (physics, chemistry & biology laboratories) unaendelea vizuri kwa Sekondari zote za Kata za Jimboni mwetu.

Ujenzi huo unachangiwa kwa ushirikiano mzuri wa Serikali, Wanavijiji na Viongozi wao.

Viongozi wa Jumuiya ya WAZAZI ya Mkoa wa Mara, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Mkoa, Ndugu Julius Kambarage Masumbo walitembelea Kata ya Nyakatende yenye sekondari mbili (Nyakatende & Kigera), na kushududia maendeleo mazuri ya miradi ya ujenzi wa maabara tatu za masomo ya sayansi kwa kila sekondari ya Kata ya Jimboni mwetu

Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
Jumatano, 4.9.2024
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2024-09-04 at 11.25.17.mp4
    34.1 MB
Back
Top Bottom