The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amelishauri Shirika la Reli Tanzania (TRC) kushughulikia changamoto zilizojitokeza katika ujenzi wa kipande cha Dar es Salaam–Dodoma ili zisijirudie katika ujenzi wa kipande cha Mwanza–Isaka.
Prof. Mbarawa ametoa ushauri huo alipokuwa Malampaka, mkoani Simiyu, akikagua maendeleo ya mradi huo. Amesema ujenzi wa reli hiyo utafungua fursa nyingi za kiuchumi kwa wakazi wa Simiyu, Mwanza na mikoa jirani.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa, amesema ujenzi wa kipande hicho umefikia asilimia 63.04 na TRC itahakikisha unakamilika kwa wakati ili wananchi wanufaike.
Prof. Mbarawa ametoa ushauri huo alipokuwa Malampaka, mkoani Simiyu, akikagua maendeleo ya mradi huo. Amesema ujenzi wa reli hiyo utafungua fursa nyingi za kiuchumi kwa wakazi wa Simiyu, Mwanza na mikoa jirani.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa, amesema ujenzi wa kipande hicho umefikia asilimia 63.04 na TRC itahakikisha unakamilika kwa wakati ili wananchi wanufaike.