Sisi Wakazi wa Pemba kuna jambo limekuwa likitutesa kwa muda na kutuathiri sana sisi Wananchi wa eneo hili.
Miaka ya hivi karibuni Serikali imekuwa ikijenga masoko ya kisasa katika kila Wilaya huku Pemba, kwa mfano hapa Chakechake kuna soko lipo pale Matemani.
Pamoja na faida na uzuri wa masoko hayo yanayojengwa upande mwingine yamekuwa ni mwiba mkali kwetu, kwani Serikali imekuwa ikibomoa magenge na sehemu ambazo tumekuwa tukinunua mahitaji yetu ya kila siku, lengo lao ni kulazimisha Wananchi tukanunue mahitaji yetu kwenye haya masoko.
Kwa miezi miwili mitatu iliyopita magenge na maduka yaliyopo barabarani yamevunjwa kwa maagizo ya Halmashauri.
Wananchi kutoka maeneo kama Mkoroshoni, Gombani na maeneo mengine kote huko wamevunjiwa maduka na magenge ili waende kwenye hilo soko kuu kununua mahitaji yao.
Ieleweka wazi kuwa sio kwamba sisi Wananchi hatupendi masoko mapya kwenye Wilaya, HAPANA, lakini mpaka kufika huko ni gharama kubwa maana ni lazima upande Bajaji au usafiri mwingine wowote kwenda kwenye soko.
Kuna soko liko pale Tumbe kwa hiyo maeneo yote karibu na Tumbe wamebomoa magenge ili kufanya Wananchi waende kwenye hilo soko.
Muda mwingine unakuta mtu umeamka na Shilingi 1,000 na unataka ununue zako tungure (nyanya) na viungo ili utengeneze mchuzi lakini huwezi kufanya hivyo kwa hiyo Sh 1,000, ndio utatumia kama nauli ya kufika huko soko kuu.
Tunaomba Serikali iliangalie hili hasa Watu wa Halmashauri, sio kila siku mtu anaweza kwenda sokoni. Tunaomba mruhusu magenge na maduka barabarani ili tupate mahitaji yetu kwa urahisi.
Miaka ya hivi karibuni Serikali imekuwa ikijenga masoko ya kisasa katika kila Wilaya huku Pemba, kwa mfano hapa Chakechake kuna soko lipo pale Matemani.
Pamoja na faida na uzuri wa masoko hayo yanayojengwa upande mwingine yamekuwa ni mwiba mkali kwetu, kwani Serikali imekuwa ikibomoa magenge na sehemu ambazo tumekuwa tukinunua mahitaji yetu ya kila siku, lengo lao ni kulazimisha Wananchi tukanunue mahitaji yetu kwenye haya masoko.
Kwa miezi miwili mitatu iliyopita magenge na maduka yaliyopo barabarani yamevunjwa kwa maagizo ya Halmashauri.
Wananchi kutoka maeneo kama Mkoroshoni, Gombani na maeneo mengine kote huko wamevunjiwa maduka na magenge ili waende kwenye hilo soko kuu kununua mahitaji yao.
Ieleweka wazi kuwa sio kwamba sisi Wananchi hatupendi masoko mapya kwenye Wilaya, HAPANA, lakini mpaka kufika huko ni gharama kubwa maana ni lazima upande Bajaji au usafiri mwingine wowote kwenda kwenye soko.
Kuna soko liko pale Tumbe kwa hiyo maeneo yote karibu na Tumbe wamebomoa magenge ili kufanya Wananchi waende kwenye hilo soko.
Muda mwingine unakuta mtu umeamka na Shilingi 1,000 na unataka ununue zako tungure (nyanya) na viungo ili utengeneze mchuzi lakini huwezi kufanya hivyo kwa hiyo Sh 1,000, ndio utatumia kama nauli ya kufika huko soko kuu.
Tunaomba Serikali iliangalie hili hasa Watu wa Halmashauri, sio kila siku mtu anaweza kwenda sokoni. Tunaomba mruhusu magenge na maduka barabarani ili tupate mahitaji yetu kwa urahisi.