Old Member (Retired)
JF-Expert Member
- Sep 29, 2012
- 3,401
- 1,610
Ipo,mwambie anunue m/benz alete atauza kwa faida!Nenda kafanye kilichokupeleka urudi nyumbani kuendelea na shughuli zako. Hakuna biashara toka Hamburg unayoweza kuleta Bongo kwa faida.
Habari zenu wadau....
Nimepata safari ya kikazi kwenda ujerumani(hamburg) hivyo kwa wazoefu naomben mnijuze kuna vitu gani vya kununua kwa wenye mitaji midogo ili nilete tanzania?
Nawasilisha
lete simu popula brands mpya au used kwa idadi ya pesa yako, au flash disks au digital camera- brand zinazokubalika huku.
sawa mkuu, nimekubali. Labda apitie dubai nadhani bei ya vitu hivyo hapo ni chini kuliko ulaya. Hivi bei za simu za LG/nokia/sumsung laini moja, mbili au tatu hapo dubai ni kiasi gani?Una wazo zuri lakini kuhusu simu sina uhakika sana kama atatengeneza faida yoyote,makampuni yanayotengeneza simu uwa wanatarget wateja wake mfano europe..africa..middle east etc sasa simu ya europe nyingi zinakuwa juu japokuwa wao huko wanaona bei ya kawaida..simu nyingi utakuta ni euro 400 sasa kwa pesa yetu inayoshuka kila siku hiyo ni pesa nyingi sana kupata faida inakuwa ngumu,na kuzingatia itakuwa ngumu kununua kwa jumla....
Nunua saa hasa za kiume always ni cheap europe zina big profit almost 10 times the purchase price
Kwanza kabisa exchange rate itakuchanganya tu hii pesa yetu inayoshuka kila siku ni kikwazo sana ktk biashara za nje...nawezakukushauri kama king'asti kuwa pitia kwenye duty free wawezapata perfume na vitu vingine vidogodogo hii inawezakuwa option,pili kama jamaa alivyoshauri hapo juu sijuhi transit unafanyia wapi..kama ni dubai wawezapata vitu cheaper kuliko humberg maana dubai vitu vinaingizwa bila ushuru..na ata vingine ni vya deal,CHAICHUNGU kakushauri m/benz ni kweli wawezapata cheap lakini sina uhakika na soko lake labda uwe umepata order...ZE MARCOPOLO kakwambia hakuna biz unayoweza toa kule kuleta Tz inawezekana ana point vitu rahisi unavyowezapata pale ni F&B yaani vyakula na vinywaji...vingine wawezapata lakini sijuhi kama vitakupa faida nzuri mfano kiatu cha timberland ni cheap sana kule ni $70 lakini ukibadili kwenye TSH ni wachache wataowezanunua..kuna vipodozi aina ya olay kuna perfume aina ya hugo boss hivi wawezapata kwa bei nzuri....Electronics ni bei sana...pia wawezajaribu kuulizia mitumba wawezapata mzigo mzuri grade A kwa bei nzuri na kama ni biz option hii ni kubwa..vitu vinavyoingizwa kule toka nje vina ushuru mkubwa sana...kule wanautamaduni mmoja utaushangaa sana uchangudoa unaruhusiwa na ni kazi yenye heshima sana,mke anamuaga mume kuwa anakwenda kazini!!!sawa mkuu, nimekubali. Labda apitie dubai nadhani bei ya vitu hivyo hapo ni chini kuliko ulaya. Hivi bei za simu za LG/nokia/sumsung laini moja, mbili au tatu hapo dubai ni kiasi gani?