Ujinga ni mbaya sana

wa stendi

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2016
Posts
25,190
Reaction score
27,434
Nakumbuka kipindi nipo mdogo mama alinipa mfuko akanituma kwa jirani yetu mbali kidogo akaniambia mpelekee huu mfuko bibi kuna mzigo wangu atakupa uweke huku ulete!

Mimi nikachukua tyre langu la chuma nililikata kwenye drum!!(kwa wale wa kijijiji wanaelewa tunaliitaga ringi) fasta nikaenda!!

Yule bibi alinipa maharagwe kama kilo 2 hivi, akaniambia ukifika njiani umwagee ee!

Mi nikamwambia haya kumbe yeye alikuwa ananipima akili asee, nikaenda mbele kidogo nikamwita yule bibi. Bibi bibi nimwage hapa? Yule bibi akaniambia mwaga hapo mpelekee mama yako huo mfuko!!

Mimi sikuchelewesha nikamwaga fasta mimi mbio nikarudisha mfuko kumpa mama.Mama akaniuliza mzigo wangu alokupa uko wapi?

Mi nikamwambia mama mbona kaniambia nimwage mi nikamwaga! Daaa nilichezea stiki balaa!!! Mama akaniambia kimbia upesi kaokote yote ulete !

Mimi nikaenda na mahasira yangu nikaokota kidogo mengine nikarusha chini ya mikahawa ili nimalize haraka, nikarudi zangu home na maharagwe!!

Kumbe yale nilotupa chini ya kahawa baada ya siku tano yakaota mareefuu badala (si unajua mche ukiota ukokosa hewa unavyukuwa mrefu kutafuta hewa) basi mama siku akapita akaona miche ilivyo ota mingi akaja home akanishika akaniuliza siku ile yale maharagwe uliokota yote!

Mimi nikamwambia ndio!! Mama akaniambia twende ase tulikuta miche mingi balaa nikapigwa tena stiki!! Hili tukio la pili ambalo sitoweza kusahau!!
 
kwe kwe kwe
utoto tabu!
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ulizidi ujinga
 
Wa Stendi bhana, mada zako zinanchekeshaga sana. Wewe utakua umekulia Arusha vijijini na kama si mmeru bas mwarusha wa Oligilai au Ng'iresi
Ringii, umenkumbusha mbali sana
 
Ulijifunza nini?
Kwanza ujinga wa kwanza ni kwa yule mama alokwambia umwage wakati anaona wewe mtoto mdogo!

Kwako wewe ni utoto tu ndo ulisababisha ufanye hayo!

Tabu - Mama yako ndo alikuwa mjinga zaidi kwa sababu hakutafakari kabla ya skick!

Mi nakumbuka wakati mtoto wangu akiwa mdogo, alipokuwa akikoea .. ilikuwa hivi mfano:

Kwa nini umevunja kikombe? ... Dad sijavuja kikombe...
Ila ... Dad sio ila....

Kwa hali ya kawaida mtoto huyo aliyaongea haya akiwa analia na kutetemeka! ...nilikaa naye na kumbembeleza kwa kumpa onyo asirudie michezo ilosababisha kosa kutendeka ....

Baada ya kuwa mkubwa ........ hadi mi nafurahia ..

Kichapo sio malezi, malezi ni kumdadizi mwanao na kumweleza chanzo cha tatizo ili ahache!
 
Mkuu kijiji wazazi hawajui kubembeleza ni stiki mwanzo mwisho!! Na hapo alieniambia nikamwage ni yule bibi ila kumbe alijuwa anapima akili zangu kama zimekomaa[emoji134] [emoji134] [emoji134]
 
Mkuu mkwepa kodi huyo jamaa mpenda sifa ndo nani ebu mtaje sitamwambia mtu haki ya mungu[emoji134] [emoji134] [emoji134] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji87] [emoji87] [emoji87] [emoji87]
 
ok dad, ila inapsawa kuwa;
skick=stick
akikoea=akikosea
sijavuja=sijavunja
kumdadizi=kumdadisi
ahache=aache.

Natumai ulimfundisha maadili tu na si kusoma na kuandika maana kwa uandishi huu, dad your are the best....................
 
Hapana bhana mkuu niombe radhi mimi sikuwaga na safura asee[emoji87] [emoji87] [emoji134] [emoji134]
 
Wee mwanga lulila wewe chondechonde usifosi kuombavmoto kwa mfuko wa rambo!!!
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji23]mkuu umenifurahisha sana, yan umekula stick PART 1 & PART 2, inaelekea bi mkubwa wako asingekuzaa angekufa... Maana huishi vibweka bhana[emoji16][emoji16][emoji23][emoji23][emoji16][emoji23]
 
Hahaaa bi mkubwa wangu alijuwa teacher hakupendaga ujinga kabisa
 
Wa Stendi bhana, mada zako zinanchekeshaga sana. Wewe utakua umekulia Arusha vijijini na kama si mmeru bas mwarusha wa Oligilai au Ng'iresi
Ringii, umenkumbusha mbali sana
aisee oligilai kwa mbotela .... kwa kavei..anglikana


Ng'iresi darajani.....

kimelok....

Nambere .....

Sekei....

mwisho kabisa water falls dah! kweli jomba kunywa soda nakuja kukulipia mkuu haha...
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] umenifurahisha sana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…