Ujio wa DRC EAC

Ujio wa DRC EAC

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Inaonekana safari ya DRC kuingia EAC imeiva. Bado hatua chache tu lakini technically ni imekubaliwa.

Inasemwa kuwa lengo la Kenya kwenye EAC ni kupata soko la bidhaa zake, kuwekeza mtaji wake unaozidi na kupata ardhi. Rwanda, na labda Burundi, malengo yao ni kupata sehemu ya kupeleka watu wanaozielemea. Tz na Ug, Hazisomeki, labda zinaona ni fasheni kuwa kwenye jumuia. Pengine ndiyo maana Tz imekuwa mpinzani mkubwa wa mambo mengi ndani ya EAC.
Kwa SS, labda wanaona watakuwa salama ndani ya EAC.

Sasa ujio wa DRC unazipa nchi kama Kenya na Rwanda wanachotaka. Ardhi, fursa za kuwekeza na soko kubwa. Na Tshekedi ameacha milango wazi. Tayari kakaribisha majirani kufaidika na madini ya DRC. Pengine ile ya Tz kujidai kuwa hakuna EAC bila Tz itakufa. Nchi sita zinaweza kwenda vizuri bila sisi. Pengine labda ni wakati wa Tz kuunda mkakati wa kufaidika na EAC badala ya kuwa huko kama fasheni.

Labda niulize, Tz inafaidikaje/inapanga kufaidikaje na EAC?
 
Hatuna viongozi wenye maono; hawajiwezi darasani, kwenye siasa na kwenye mipango ya maendeleo.Magufuli alijenga viwanda mdomoni, Mama Samia hadi muda huu hatujui vipaumbele vyake nini na anataka Tanzania iweje baada ya miaka 5 kuisha, hapo unategemea kiongozi wa aina hiyo awaze namna ya kufaidika na ujio wa Congo?

Reli ya SGR ilitakiwa iende Kigoma, tupokee na kupeleka mizigo Congo, bahati mbaya akaja Jiwe na ubinafsi wake kaipeleka Mwanza kuchukua abiria.

Kenya hawana rasilimali yoyote ya maana zaidi ya watu lakini wanaweza kuvutia wawekezaji wakubwa pamoja na wao wenyewe kupanga mipango ya uwekezaji, bahati mbaya kwa Tanzania sijui lini tutafikia hatua hii. Kikwete na Mkapa walijitahidi sana kuwaleta wawekezaji wakubwa, ila kipindi cha Jiwe chote pamoja na cha huyu mama wa sasa, ni wapenda sifa tu ila kwenye mipango ya uwekezaji ni zero kabisa.
 
Ni kweli hatuna viongozi wenye vision ila tuna watawala wenye kupenda kuabudiwa hadi siku hizi serikali ikitoa fedha 💸 ambayo pia ni kodi za wananchi inatakiwa isemwe rais ametoa, yaani ujinga mtupu.

Tuna watawala ambao wao usiku na mchana wanachowaza ni namna ya kuhodhi na kubaki madarakani lakini kiukweli hawana mkakati wowote wa maana wa kuitoa hii nchi hapa ilipo.

Hizi jumuiya hazina kabisa maana kama watu hawawezi wakatembea katika nchi zanachama bila kikwazo na hata kama bidhaa tu haziwezi kusafirishwa bila kulipia ushuru hii jumuiya itabaki ni propaganda za wanasiasa tu, hamna lolote.
 
Inawezekan tuna viongozi wazuri tena visionary ila the problem ni kuwa wengi wao ni wachumia tumbo. Matumbo yao na familia zao kwanza Tanzania baadae.
 
Hatuna viongozi wenye maono; hawajiwezi darasani, kwenye siasa na kwenye mipango ya maendeleo.Magufuli alijenga viwanda mdomoni, Mama Samia hadi muda huu hatujui vipaumbele vyake nini na anataka Tanzania iweje baada ya miaka 5 kuisha, hapo unategemea kiongozi wa aina hiyo awaze namna ya kufaidika na ujio wa Congo?

Reli ya SGR ilitakiwa iende Kigoma, tupokee na kupeleka mizigo Congo, bahati mbaya akaja Jiwe na ubinafsi wake kaipeleka Mwanza kuchukua abiria.

Kenya hawana rasilimali yoyote ya maana zaidi ya watu lakini wanaweza kuvutia wawekezaji wakubwa pamoja na wao wenyewe kupanga mipango ya uwekezaji, bahati mbaya kwa Tanzania sijui lini tutafikia hatua hii. Kikwete na Mkapa walijitahidi sana kuwaleta wawekezaji wakubwa, ila kipindi cha Jiwe chote pamoja na cha huyu mama wa sasa, ni wapenda sifa tu ila kwenye mipango ya uwekezaji ni zero kabisa.
Naona unaandika bila kuwa na upeo wa kufahamu kwamba maendeleo ni lazima yawe ya kwako, siku zote mtegemea cha nduguye hufa masikini.

Tanzania haiwezi kujisifia kutajirika kwa kuwanyonya wengine. SGR itarahisisha usafirishaji wa watu pamoja na bidhaa nchini kwa haraka na wakati unaotakiwa na utawezesha Watanzania kutatua changa moto zao. SGR itaokoa pesa nyingi za ukarabati wa barabara kwa kuondoa maroli ya mizigo barabarani nk. Kasome ilani ya CCM ambayo ndio Serikali ya SSH na CCM wanaifuata. Hao wezi unaowasifa ie Kikwete na Mkapa ndio walifilisi hii nchi bila kuwa na taswira ya kueleweka. Mkapa aliuza viwanda vyote kwa bei ya peremende (Kumbuka viwanda vyote alivyojenga Nyerere). Huyo Mzee wa msoga bado jinamizi lake tunalo aka Vasco da Gama.
 
Naona unaandika bila kuwa na upeo wa kufahamu kwamba maendeleo ni lazima yawe ya kwako, siku zote mtegemea cha nduguye hufa masikini.

Tanzania haiwezi kujisifia kutajirika kwa kuwanyonya wengine. SGR itarahisisha usafirishaji wa watu pamoja na bidhaa nchini kwa haraka na wakati unaotakiwa na utawezesha Watanzania kutatua changa moto zao. SGR itaokoa pesa nyingi za ukarabati wa barabara kwa kuondoa maroli ya mizigo barabarani nk. Kasome ilani ya CCM ambayo ndio Serikali ya SSH na CCM wanaifuata. Hao wezi unaowasifa ie Kikwete na Mkapa ndio walifilisi hii nchi bila kuwa na taswira ya kueleweka. Mkapa aliuza viwanda vyote kwa bei ya peremende (Kumbuka viwanda vyote alivyojenga Nyerere). Huyo Mzee wa msoga bado jinamizi lake tunalo aka Vasco da Gama.
Naomba niku sahihishe Nyerere hakujenga viwanda bali alitaifisha.vingi vili iletea hasara selikali kwa kushindwa kujiendesha hii ni sababu ya serikali kuvitaifisha.
 
Naona unaandika bila kuwa na upeo wa kufahamu kwamba maendeleo ni lazima yawe ya kwako, siku zote mtegemea cha nduguye hufa masikini.

Tanzania haiwezi kujisifia kutajirika kwa kuwanyonya wengine. SGR itarahisisha usafirishaji wa watu pamoja na bidhaa nchini kwa haraka na wakati unaotakiwa na utawezesha Watanzania kutatua changa moto zao. SGR itaokoa pesa nyingi za ukarabati wa barabara kwa kuondoa maroli ya mizigo barabarani nk. Kasome ilani ya CCM ambayo ndio Serikali ya SSH na CCM wanaifuata. Hao wezi unaowasifa ie Kikwete na Mkapa ndio walifilisi hii nchi bila kuwa na taswira ya kueleweka. Mkapa aliuza viwanda vyote kwa bei ya peremende (Kumbuka viwanda vyote alivyojenga Nyerere). Huyo Mzee wa msoga bado jinamizi lake tunalo aka Vasco da Gama.
Tatizo lako we ni kasuku. Kufanya kazi peke yake hakuwezi kuwaondoa wananchi kwenye umaskini kama hakuna sera, sheria nzuri pamoja na mipango inayotekelezeka. Ili ufanye kazi yenye kuleta faida ni lazima mazingira wezeshi yawepo na hapo ndipo serikali inapoingia. Serikali ya China inajisifia imewatoa watu milioni 100 kwenye umasikini, je serikali ndio ilikuwa inafanya kazi au hao watu m.100?, serikali za Ulaya zinapopambana kupunguza unemployment rate kwenye Nchi zao, wanafanya makosa?

Kuhusu SGR, maelezo yako hayana uhusiano na nilichocomment. Kama ni abilia hata Kigoma wapo ila lengo mama ilikuwa ni mizigo.
 
Naona unaandika bila kuwa na upeo wa kufahamu kwamba maendeleo ni lazima yawe ya kwako, siku zote mtegemea cha nduguye hufa masikini.

Tanzania haiwezi kujisifia kutajirika kwa kuwanyonya wengine. SGR itarahisisha usafirishaji wa watu pamoja na bidhaa nchini kwa haraka na wakati unaotakiwa na utawezesha Watanzania kutatua changa moto zao. SGR itaokoa pesa nyingi za ukarabati wa barabara kwa kuondoa maroli ya mizigo barabarani nk. Kasome ilani ya CCM ambayo ndio Serikali ya SSH na CCM wanaifuata. Hao wezi unaowasifa ie Kikwete na Mkapa ndio walifilisi hii nchi bila kuwa na taswira ya kueleweka. Mkapa aliuza viwanda vyote kwa bei ya peremende (Kumbuka viwanda vyote alivyojenga Nyerere). Huyo Mzee wa msoga bado jinamizi lake tunalo aka Vasco da Gama.
Ingejengwa kwenda DRC, Rwanda na Burundi inge ingiza mapato, Bandari ingezidi kuingia mihela na muda mfupi reli ingeweza kuelekezwa Mwanza na mikoa ya Kusini.
 
Sasa ujio wa DRC unazipa nchi kama Kenya na Rwanda wanachotaka. Ardhi, fursa za kuwekeza na soko kubwa. Na Tshekedi ameacha milango wazi. Tayari kakaribisha majirani kufaidika na madini ya DRC. Pengine ile ya Tz kujidai kuwa hakuna EAC bila Tz itakufa. Nchi sita zinaweza kwenda vizuri bila sisi. Pengine labda ni wakati wa Tz kuunda mkakati wa kufaidika na EAC badala ya kuwa huko kama fasheni.

Labda niulize, Tz inafaidikaje/inapanga kufaidikaje na EAC?
ujio wa DRC katika comunity ki kama Ukrain, Fin na sweden anayopambana kuingia NATO, anatafuta usalama dhidi ya tishio la PAKA
 
Back
Top Bottom