Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 324
- 649
MFAHAMU HAYATI KENNETH KAUNDA(KK).
Na Elius Ndabila
0768239284
Taarifa iliyoripitiwa hivi leo na vyombo vya ndani vya Zambia ni kuwa Rais wa Rais wa Kwanza wa Zambia Mzee Kenneth KAUNDA ambaye kule wanapenda kumwita Baba wa Taifa ameaga Dunia.Mzee Kaunda ni pekee yake kati ya Wazee wa Mwanzo waasisi wa Uhuru barani Afrika aliyekuwa bado hai.
Mzee Kaunda ana historia ndefu na ya kuvutia, leo nitajaribu kukupa historia yake fupi huyu moja ya miamba ya Afrika aliyefariki Leo akiwa na miaka 97 na miezi karibia 2.
Wapo wanaosema Mzee Kaunda ni mtu wa Malawi ambaye alienda kusaidia Zambia kupata Uhuru.Leo nitakujuza kudogo na kukupa majibu juu ya utata huu ambao watu wengi wanao.
Kabla sijamzunguzia Hayati Kaunda, ninaomba nijibu kwanza hoja ya utata wa mahusiano ya Kaunda na Malawi na kwa nini Kaunda alikuwa na mahusiano ya karibu sana na Rais wa Kwanza wa Malawi Mzee Banda? Jibu la hili ni kuwa Baba yake Kenneth KAUNDA alikuwa ni mzaliwa wa Malawi. Baba yake Kenneth KAUNDA Mzee David Kaunda na Mama yake Kenneth KAUNDA walikuwa ni Walimu. Walichukuliwa kwendq kufundisha Nothern Rhodesia/Zambia kutoka Nyasalanda/Malawi. Wakiwa huko ndipo walibahatika kumzaa Kenneth KAUNDA Kama sehemu ya watoto wao nane. Hivyo Kaunda ni Mzambia kwa kuzaliwa lakini akiwa na asili ya Malawi.Ninadhani hapo tumeelewana. Mama yake alikuwa ni mwanamke wa Kwanza Afrika kufundisha katika shule za kikoloni.
Tumtazame sasa Kenneth KAUNDA.
Ukisoma maandiko mbalimbali ya Zambia Hayati Kaunda hajaandikwa sana. Hivyo ninaweza kusema ni mtu ambaye pamoja na umaarufu wake mkubwa lakini hajawekwa sana kwenye kumbukumbu za kwenye maandishi. Kidigo kwenye mtandao wa Britannic.com wamejaribu kumuelezea kinagaubaga.
Keneth Kaunda alizaliwa 24/4/1924 katika Kijiji Cha Lubwa ambacho kipo karibu na mji wa Chinsali Kaskazini mwa Zambia.
KK alisoma shule ya msingi katika shule waliyokuwa wakifundisha wazazi wake. Alihitimu masomo ya sekondari mwaka 1940. Kama ilivyo kwa Waafrika wengine ambao walau walikuwa wamepata elimu ya kati, Kaunda naye alienda kuwa Mwalimu. Aliwahi kufundisha Zambia na Tanganyika/Tanzania katika ya miaka ya 1940.
Mwaka 1949 Kaunda alirejea Zambia na akawa Mkalimani na mshauri wa Sir Stewart Gere-Browne a leberal white Settler ambaye pia alikuwa Mbunge. Huko Kaunda alijifunza vitu vingi ikiwepo siasa.
Mwaka 1950 Kaunda alijiunga na chama Cha ANC's na baadaye akawa katibu mkuu(Mtendaji mkuu). Nafasi hii ilimuongezea exposure na akawa maarufu sana. Hata 1958_59 ANC ilipoanza malengo ya kudai Uhuru Kaunda ndiye alipewa majukumu makubwa ya kutengeneza program.
Baadaye alikuja kuwa kiongozi mkuu wa taasisi hiyo na kuanza kufoji baadhi ya nyalaka za kizungu katika makoloni ya Uingereza hasa Zambia, Malawi na Zimbabwe. Alijitahidi kuwashawishi wananchi kupigania Uhuru lakini wengi wakawa waoga. Akaanzisha kitu kilichoitwa "Positive nonviolent action" ambacho kilihusika na raia kutokutii maagizo ya sera za ukolini. Matokeo haya hili yalikuwa mawili ambapo mojawapo alikamatwa yeye na wenzake na kwenda jera. Hii iliwapa ushujaa na kipindi hicho afrika nzima ilikuwa kwenye mapambano ya kudai Uhuru.
January 1960 aliruhusiwa kutoka magereza na akachaguliwa kuwa Rais wa UNDP( UNITED NATIONAL INDEPENDENCE PARTY) ambacho kilizaliwa mwaka 1959 ba Mainza Chona.
Mwaka 1960 mwishoni Uingereza ilimualika kuhutubia baraza Hilo Londan kueleza kwa nini anataka Uhuru?
Uchaguzi ulipofanyika 1962 chama chake kilishinda. Na mwaka 1964 ikapata Uhuru kamili Kaunda akiwa Rais.
Kama yalivyomaeneo mengine, baada ya Zambia kupata Uhuru vilizuka Vita vya ukabila, hasa ukizingatia Kaunda alikuwa na asili ya Malawi. Na uchaguzi ulipofanyika mwaka 1968 Kaunda alishinda. Alipoona mbele haoni kuendelea kuwa Rais hasa ukizingatia Vita ya ukabila na Utaifa, mwaka 1972 alifutilia mbali mfumo wa vyama vingi na mwaka 1973 akatengeneza katiba.
Mwaka 1970 Zambia ikuwa black nationalistic guerrillas led by Joshua Nkomo( Nitaandika next time).
Mwaka 1990 Kaunda aliruhusu Mfumo wa vyama vingi na mwaka 1991 Kaunda na Chama chake Cha UNIP walushindwa vibaya kwenye uchaguzi na Chama Cha Movement Multiparty Democracy (MMD) ilishinda kwa ushindi wa kishindo(landslide) na Fredrick Chiluba kuwa Rais.
Kaunda amefariki akiwa na miaka 97.
RIP Kaunda.
Zaidi, soma:
1). News Alert: - Kenneth Kaunda afariki dunia akiwa na miaka 97
Na Elius Ndabila
0768239284
Taarifa iliyoripitiwa hivi leo na vyombo vya ndani vya Zambia ni kuwa Rais wa Rais wa Kwanza wa Zambia Mzee Kenneth KAUNDA ambaye kule wanapenda kumwita Baba wa Taifa ameaga Dunia.Mzee Kaunda ni pekee yake kati ya Wazee wa Mwanzo waasisi wa Uhuru barani Afrika aliyekuwa bado hai.
Mzee Kaunda ana historia ndefu na ya kuvutia, leo nitajaribu kukupa historia yake fupi huyu moja ya miamba ya Afrika aliyefariki Leo akiwa na miaka 97 na miezi karibia 2.
Wapo wanaosema Mzee Kaunda ni mtu wa Malawi ambaye alienda kusaidia Zambia kupata Uhuru.Leo nitakujuza kudogo na kukupa majibu juu ya utata huu ambao watu wengi wanao.
Kabla sijamzunguzia Hayati Kaunda, ninaomba nijibu kwanza hoja ya utata wa mahusiano ya Kaunda na Malawi na kwa nini Kaunda alikuwa na mahusiano ya karibu sana na Rais wa Kwanza wa Malawi Mzee Banda? Jibu la hili ni kuwa Baba yake Kenneth KAUNDA alikuwa ni mzaliwa wa Malawi. Baba yake Kenneth KAUNDA Mzee David Kaunda na Mama yake Kenneth KAUNDA walikuwa ni Walimu. Walichukuliwa kwendq kufundisha Nothern Rhodesia/Zambia kutoka Nyasalanda/Malawi. Wakiwa huko ndipo walibahatika kumzaa Kenneth KAUNDA Kama sehemu ya watoto wao nane. Hivyo Kaunda ni Mzambia kwa kuzaliwa lakini akiwa na asili ya Malawi.Ninadhani hapo tumeelewana. Mama yake alikuwa ni mwanamke wa Kwanza Afrika kufundisha katika shule za kikoloni.
Tumtazame sasa Kenneth KAUNDA.
Ukisoma maandiko mbalimbali ya Zambia Hayati Kaunda hajaandikwa sana. Hivyo ninaweza kusema ni mtu ambaye pamoja na umaarufu wake mkubwa lakini hajawekwa sana kwenye kumbukumbu za kwenye maandishi. Kidigo kwenye mtandao wa Britannic.com wamejaribu kumuelezea kinagaubaga.
Keneth Kaunda alizaliwa 24/4/1924 katika Kijiji Cha Lubwa ambacho kipo karibu na mji wa Chinsali Kaskazini mwa Zambia.
KK alisoma shule ya msingi katika shule waliyokuwa wakifundisha wazazi wake. Alihitimu masomo ya sekondari mwaka 1940. Kama ilivyo kwa Waafrika wengine ambao walau walikuwa wamepata elimu ya kati, Kaunda naye alienda kuwa Mwalimu. Aliwahi kufundisha Zambia na Tanganyika/Tanzania katika ya miaka ya 1940.
Mwaka 1949 Kaunda alirejea Zambia na akawa Mkalimani na mshauri wa Sir Stewart Gere-Browne a leberal white Settler ambaye pia alikuwa Mbunge. Huko Kaunda alijifunza vitu vingi ikiwepo siasa.
Mwaka 1950 Kaunda alijiunga na chama Cha ANC's na baadaye akawa katibu mkuu(Mtendaji mkuu). Nafasi hii ilimuongezea exposure na akawa maarufu sana. Hata 1958_59 ANC ilipoanza malengo ya kudai Uhuru Kaunda ndiye alipewa majukumu makubwa ya kutengeneza program.
Baadaye alikuja kuwa kiongozi mkuu wa taasisi hiyo na kuanza kufoji baadhi ya nyalaka za kizungu katika makoloni ya Uingereza hasa Zambia, Malawi na Zimbabwe. Alijitahidi kuwashawishi wananchi kupigania Uhuru lakini wengi wakawa waoga. Akaanzisha kitu kilichoitwa "Positive nonviolent action" ambacho kilihusika na raia kutokutii maagizo ya sera za ukolini. Matokeo haya hili yalikuwa mawili ambapo mojawapo alikamatwa yeye na wenzake na kwenda jera. Hii iliwapa ushujaa na kipindi hicho afrika nzima ilikuwa kwenye mapambano ya kudai Uhuru.
January 1960 aliruhusiwa kutoka magereza na akachaguliwa kuwa Rais wa UNDP( UNITED NATIONAL INDEPENDENCE PARTY) ambacho kilizaliwa mwaka 1959 ba Mainza Chona.
Mwaka 1960 mwishoni Uingereza ilimualika kuhutubia baraza Hilo Londan kueleza kwa nini anataka Uhuru?
Uchaguzi ulipofanyika 1962 chama chake kilishinda. Na mwaka 1964 ikapata Uhuru kamili Kaunda akiwa Rais.
Kama yalivyomaeneo mengine, baada ya Zambia kupata Uhuru vilizuka Vita vya ukabila, hasa ukizingatia Kaunda alikuwa na asili ya Malawi. Na uchaguzi ulipofanyika mwaka 1968 Kaunda alishinda. Alipoona mbele haoni kuendelea kuwa Rais hasa ukizingatia Vita ya ukabila na Utaifa, mwaka 1972 alifutilia mbali mfumo wa vyama vingi na mwaka 1973 akatengeneza katiba.
Mwaka 1970 Zambia ikuwa black nationalistic guerrillas led by Joshua Nkomo( Nitaandika next time).
Mwaka 1990 Kaunda aliruhusu Mfumo wa vyama vingi na mwaka 1991 Kaunda na Chama chake Cha UNIP walushindwa vibaya kwenye uchaguzi na Chama Cha Movement Multiparty Democracy (MMD) ilishinda kwa ushindi wa kishindo(landslide) na Fredrick Chiluba kuwa Rais.
Kaunda amefariki akiwa na miaka 97.
RIP Kaunda.
Zaidi, soma:
1). News Alert: - Kenneth Kaunda afariki dunia akiwa na miaka 97