Ujumbe kwa wanandoa watarajiwa!

Dark City

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2008
Posts
16,253
Reaction score
11,626
Heri ya mwaka mpya wapenzi wa jukwaa letu la MMU na pia natoa pole kwa wote ambao wana migogoro ya kiafya!!


Baada ya mijadala ambayo tumeifanya mwaka uliopita na ile ambayo tumefungia mwaka, baadhi ya wanadau ambao ni next generation ya wanandoa walihisi kwamba wametengwa. Kwa leo nimeona niwawekee maneno kidogo hapa, ili yawasidie wakati wanajiandaa kuingia kwenye hii taasis ambayo ni very simple but yet extremely complex, very sweet but also the hardest to swallow at times (hata quinine haifai) and very exciting but also boring!!

  1. Don't be naïve: Ni muhimu kufanya maandalizi ya ndoa kwa umakini wa hali ya juu na kuachana na utopia ambazo zinaweza kukusababishia matatizo. Haya mambo ya kudanganywa na maua, chocolate, sms za ajabu ajabu, simu za kila baada ya nusu saa (for girls) au ad libitum sex (kwa boys) visitumike kama vigezo vya kumpa mtu nafasi….Hakikisha unafanya home work yako (due diligence ya kutosha) vinginevyo utakumbana na mikataba kama ya Richmond; and that will be too late!!
  2. Hakuna sababu ya kuwa na huruma: Hakuna sababu ya kumwonea mtu huruma kwa sababu wewe siyo mama yake wala Yesu Masiha! .....Utasikia mtu anasema kuwa amekaa na GF au BF wake kwa muda mrefu kwa hiyo anaogopa kumuumiza…Yes ataumia but that will be over after a very short time! Ila kama utajifanya Msamaria na kumkubali mtoto wa watu basi utakuwa umemharibia maisha yake yote…Dhambi hiyo ni kubwa sana!!
  3. Unshakable criteria: Lazima mtu ujitambue wewe mwenyewe ili uweze kuwa na vigezo vya kumpimia mwenzio. Kama huwezi kufanya hiyo kazi, bora jikalie tu utange tange mitaani…It will be very hard to work out your way kwenye ndoa kama hujui unachokitaka. Ni sawa na kwenda kuuza vitu sokoni ambavyo hata hujui bei yake katika masoko….Pia mwenzio akikugundua anaweza kukufanya msukule
  4. Don't compromise on important issue: Kwa mfano, kama unajua kuwa huwezi kulea mtoto wa kambo, basi usifanye urafiki na mtu mwenye mtoto (either sex). Pia usipende kufanya majaribio kwa kuwa na mahusiano na watu ambao wewe unajua kuwa hawana vigezo vyako muhimu (hii inawahusu sana boys ambao wanapenda kuchezea vitoto vya mitaani huku wakijidanganya kwamba wana pass time).
  5. Don't be a spectator: Ukishaamua kuwa na urafiki na mtu, hakikisha unashirikiana naye mambo yake ya muhimu. Kwa mfano, kuna vijana wengi (hata wanaume) wanakuwa na GF ila hawajui hata cycle zao zinaanza na kuisha lini. Matokea yake wanakuja kulalamika mara GF anaporipoti kuwa kapata mimba…................Ni muhimu kushea details na mwenzio ili kuondoa chances za kuwa surprised na mambo ambayo hukuyategemea kabisa na labda ungemsaidia kuya-avoid!
  6. Acha mizaha: Kuna watu wanafanya majaribio ya hatari katika mahusiano..Like kutumia ngono za mitandao isiyoruhusiwa. Pia kuna watu hawajali hata wakipata watoto kwenye mahusiano yasiyoeleweka. Please do whatever possible to avoid pregnancy if you can't be friends without sex!
  7. Expect the unexpected: Mahusiano yoyote kabla ya ndoa hayako binding…Nawashauri vijana wajiandae kwa lolote…But take precautions ili kupunguza maumivu. Kwa mfano, siyo fair kuwa kwenye relationship isiyoeleweka kwa miaka 2 au zaidi!!

Naamini wadau wataongeza au kuboresha ili hii dossier iwe ya manufaa kwa wadau na utukufu wa taasisi ya ndoa urudi mahali pake!!


Mungu awabariki nyote,


Babu DC (1947)
 
Thank you babu DC!!!
I will follow your advice.
:A S-coffee:
 
Duuuu,

This is a stunning revelation!!

Sikujua kama huu uzi ungekuwa multipurpose kiasi hicho!!

Karibu sana na toa maoni yako pia!!

Babu DC!!

Babu tatizo lako unafikiria sana.Sasa hapo kwenye maltipapasi unamaanisha nini?Hainihusu?
 
uzi mzuri
tatizo babu DC unanichanganya kitu kimoja
uzi umekaa kama monogamy relatioship
while najua wewe ndo Chairman wa chama letu la ma polygamist...
 
Ushauri mzuri sana babu, hopefully wahusika wamesikia na wataufanyia kazi.
 
uzi mzuri
tatizo babu DC unanichanganya kitu kimoja
uzi umekaa kama monogamy relatioship
while najua wewe ndo Chairman wa chama letu la ma polygamist...

Please kaka yangu na ndugu yangu, The Boss,

Kila jukwaa lina aina ya mahubiri yake.....

Mwaka huu 2012, tunahubiri jinsi ya kuimarisha taasis hii muhimu sana.....

Nitaleta barua yangu ya kuomba likizo kwenye chama chetu ili nisikumbwe na conflict of interest!!
 

...nimeipenda sana hii...inaukweli mwingi ndani yake,....tushashuhudia jinsi watu namna kwa namna wanavyojishusha thamani yao na wanayoyaamini ili waoe/waolewe na fulani...2012 tutapiga vita kwa nguvu zote. AMEN.
 
Sikujua kama hii thread ingesaidia walau kutenganisha boys Vs men, na girls Vs women,.....Lol!!

Babu DC!!
Hahahahaa.Hii Inamhusu kila mtu.Hata akina babu na bibi, kwa kuwa soon wataoza vijana na mabinti..
Halafu mm nataka kuanza kutoa ushauri nasaha,Hivo nakusukuru sana kwa uzi huu umeanzisha..
 
Duh, babu DC

hadi kufikiri hayo yote lazima mtu uwe mzima kichwani(matured).

Asante, itawafaa sana vijana.
 
Duh, babu DC

hadi kufikiri hayo yote lazima mtu uwe mzima kichwani(matured).

Asante, itawafaa sana vijana.

Mbona wewe unakuwa mchoyo hivyo??

Hata kama interest yako ni kuwa na mpango wa mtumizi ya disposables, bado unaweza kuwasaidia wagogo zako ambao wamejawa na wasi wasi!!

Hebu basi wape mauzoefu yako basi!
 

...nimeipenda sana hii...inaukweli mwingi ndani yake,....tushashuhudia jinsi watu namna kwa namna wanavyojishusha thamani yao na wanayoyaamini ili waoe/waolewe na fulani...2012 tutapiga vita kwa nguvu zote. AMEN.

Ni muhimu sana kaka,

Mie niliapa kwamba sitalea mtoto wa mtu mwingine na pia sitaki mtoto wangu akawe mzigo kwa mtu mwingine.

Dada yangu mmoja akatease na ki swali cha uzushi, kwamba itakuwaje ningempa mimba msichana wa low class kama housegirl??

Jibu langu likuwa simple and clear...Huyo ndiye angekuwa mke wangu na sasa hivi tungekuwa tunamwita Bibi DC!!


Babu DC!!
 
Ujumbe mzuri sana, wakiuzingatia utawafaa sana.

Hebu basi na wewe ongeza kidogo basi,

Mfano, unaonaje suala la kutumia ngono za nje nje kama chambo cha kuingiza watu kwenye ndoa??
 
unajua huwa nashindwa kuelezea mambo ya mahusiano sababu nina Conservative approach ambayo kwa vijana wengi nawachanganya badala ya kuwasaidia

kitu kingine to me marriage is a value like religion, you either believe in it or not. Hakuna kuwa kati.
Siamini eti kama partner anacheat, au ni irresponsible basi basi ampelekee mwenzie kucheat. Haijustify, sababu mtu mwingine hatakiwi kubadili belief yako.

So its very complicated kuelezea.
Mbona wewe unakuwa mchoyo hivyo??

Hata kama interest yako ni kuwa na mpango wa mtumizi ya disposables, bado unaweza kuwasaidia wagogo zako ambao wamejawa na wasi wasi!!

Hebu basi wape mauzoefu yako basi!
 
Naamini wadau wataongeza au kuboresha ili hii dossier iwe ya manufaa kwa wadau na utukufu wa taasisi ya ndoa urudi mahali pake!!


...kuna ule msemo watu wanasema huyu uliyemuoa wala sio type yako,....
hebu mtu mzima ichambue hii, naamini ushawahi isikia...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…