Pre GE2025 Ujumbe mahsusi Kwa Wajumbe wa CHADEMA, msiue matumaini ya Watanzania

Pre GE2025 Ujumbe mahsusi Kwa Wajumbe wa CHADEMA, msiue matumaini ya Watanzania

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Watanzania wana maumivu mengi na hasira kubwa dhidi ya CCM, chama ambacho kimekuwa kama syndicate ya kuwaumiza watanzania walio wengi na kuzineemesha familia chache kupitia kodi za hao wengi wanaoumizwa.

CCM imekuwa na kiburi kisichoelezeka. Wananchi, kupitia tume ya Warioba walisema wanataka katiba mpya, syndicate hii ya CCM imekataa. Wananchi kupitia tume ya Warioba walisema wanataka Tume Huru ya Uchaguzi, kikundi hiki ndani ya CCM kimekataa.

Kikundi hiki kimejimilikisha nchi na kila kitu kilichomo. Wanauza na kugawa rasilimali za nchi na kutapanya rasilimali za nchi hovyo. Wao ndio Tanzania na wao ndio CCM.

Fikiria kuwa sasa hivi, kwa kupitia Rais Mstaafu, wamefikia hata kutamka wazi kuwa 'wachawi ndani ya CCM wamekufa"!!. Ina maana viongozi walioaminiwa na watanzania kushika nafasi za juu katika nchi, walikuwa ni wachawi dhidi yao wao waliojimilikisha CCM. Hii inaongezea kwenye ile kauli ya, "wazuri hawafi".

CCM na hii syndicate, wanatakiwa kupumzishwa. Tanzania irudishwe kwa Watanzania, na CCM irudishwe kwa wanaCCM. Hilo halitawezekana kama hakutakuwa na chama chenye nguvu cha upinzani, chama kilicho madhubuti, na kinachoongozwa na watu madhubuti, watu walionyooka, watu wasiohongeka, watu wakweli wa kauli na nafsi zao, watu walio tayari kuteseka kwa njaa, huku pembeni kuna watu wanaowahonga chakula alimradi tu watoke kwenye misimamo yao thabiti.

Kwa sasa chama kilicho tegemeo pekee ni CHADEMA, lakini ndani ya CHADEMA, ile syndicate ya CCM imekwishajipenyeza, ndiyo maana tunashuhudia baadhi ya wagombea ndani ya CHADEMA, wakipigiwa kampeni kali na machawa wa syndicate ya CCM.

Wajumbe, zingatieni ukweli huu,

"Mkiona mgombea yeyote anapigiwa kampeni na kushabikiwa na machawa wa syndicate ya CCM, hamtakiwi kujiuliza mara 2, pigeni chini huyo mgombea, kwa sababu huyo atakuwa miongoni mwa hao walioletwa na syndicate ya CCM ndani ya CHADEMA kwaajili ya kulinda maslahi ya hiyo syndicate ya CCM, na kuua matumaini ya Watanzania.

kupigiwa kampeni, chapuo na machawa wa syndicate ya CCM, ni disqualification ya moja kwa moja ya kutompa kura mgombea huyo.

Wajumbe leteni uongozi imara utakaoitengeneza CHADEMA mpya, itakayowapa uwanja wananchi wa kuonesha hasira zao dhidi ya syndicate ya CCM, msilete uongozi utakaoifanya CHADEMA kuwa CCMB
 
Mtu mzushi,anayekadhifu wengine,anayetusi hovyo ndiyo apewe chama mnaakili ninyi??
Mungu hawezi kubariki uongozi wa lissu iwapo atashinda uchaguzi nahakika wakurupukaji watampa uenyekiti na mapema watamchoka na kumkinai Kwa mikurupuko yake!!
Huwezi kushindana na serikali kiubabe ubabe eti lisu aivimbie serikali huo ni ujinga wa wazi,atasota jela na mwisho ataishia vibaya acheni kumpa kichwa huyo roporopo.
Chini ya lissu chadema kitakwisha na viongozi wanaofuata watapatikana Kwa kupinduana kihila na kimatusi
 
Acha maneno meengi, we sema tu wajumbe watuletee Lissu, full stop!!.
 
"Mkiona mgombea yeyote anapigiwa kampeni na kushabikiwa na machawa wa syndicate ya CCM, hamtakiwi kujiuliza mara 2, pigeni chini huyo mgombea,...
Nakazia ✍️
Wajumbe wakizingatia huu ushauri mzuri, itabidi Mbowe na Wenje wakatafute kazi zingine
 
Mtu mzushi,anayekadhifu wengine,anayetusi hovyo ndiyo apewe chama mnaakili ninyi??
Mungu hawezi kubariki uongozi wa lissu iwapo atashinda uchaguzi nahakika wakurupukaji watampa uenyekiti na mapema watamchoka na kumkinai Kwa mikurupuko yake!!
Huwezi kushindana na serikali kiubabe ubabe eti lisu aivimbie serikali huo ni ujinga wa wazi,atasota jela na mwisho ataishia vibaya acheni kumpa kichwa huyo roporopo.
Chini ya lissu chadema kitakwisha na viongozi wanaofuata watapatikana Kwa kupinduana kihila na kimatusi
chawa mwingine huyu kaonekana
 
Heshima yako Mkuu.
Vipi kuhusu MwanaCCM Peter Msigwa kum-endorse Tundu Lissu awe Mwenyekiti wa CHADEMA, hii imekaaje Mkuu?
 
Mtu mzushi,anayekadhifu wengine,anayetusi hovyo ndiyo apewe chama mnaakili ninyi??
Mungu hawezi kubariki uongozi wa lissu iwapo atashinda uchaguzi nahakika wakurupukaji watampa uenyekiti na mapema watamchoka na kumkinai Kwa mikurupuko yake!!
Huwezi kushindana na serikali kiubabe ubabe eti lisu aivimbie serikali huo ni ujinga wa wazi,atasota jela na mwisho ataishia vibaya acheni kumpa kichwa huyo roporopo.
Chini ya lissu chadema kitakwisha na viongozi wanaofuata watapatikana Kwa kupinduana kihila na kimatusi
Neno "TUSI" linekuzwa sana kwa hofu ya mtu imara, aitwae Lissu.
 
Back
Top Bottom