Ujumbe toka uchaguzi wa Marekani

Ujumbe toka uchaguzi wa Marekani

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Obama kafanikiwa kutetea kiti chake cha urais. Uchaguzi umeenda haraka na kwa uwazi na matokeo yametoka bila kigugumizi. Mshindani wake kakubali matokeo na mwisho wa siku maisha yanaendelea.

Bila ya shaka ni kwamba idadi kubwa ya watu nje ya Marekani walipenda kuona tena kuwa Obama anamalizia muda wake. Bila kujali vyama vyetu tulitamani hivyo na imekuwa.

Democrats ni chama tawala na Republican ni wapinzani. Walio nje ya Marekani wengi watu tulitaka chama tawala kiendelee na utawala na upinzani upotezewe.

Tuko katika mchakato wa kuelekea uchaguzi mkuu hapa Tanzania. Chama kikuu cha upinzani ni cdm, na chama tawala ni ccm. Tulio wanachama na mashabiki wa cdm tulitaka chama tawala Marekani-Democrats waendelee na upinzani-Republican washindwe, na tukafurahi. Hii inaleta picha gani kwetu? Ni nini hasa nguvu ya chama tawala? Labda mazingira yanatofautiana, lakini siasa ni zile zile.

Kwa nini tupende chama tawala kiendelee kwa wenzetu wakati kwetu tunataka kuking'oa?
 
Obama kafanikiwa kutetea kiti chake cha urais. Uchaguzi umeenda haraka na kwa uwazi na matokeo yametoka bila kigugumizi. Mshindani wake kakubali matokeo na mwisho wa siku maisha yanaendelea.

Bila ya shaka ni kwamba idadi kubwa ya watu nje ya Marekani walipenda kuona tena kuwa Obama anamalizia muda wake. Bila kujali vyama vyetu tulitamani hivyo na imekuwa.

Democrats ni chama tawala na Republican ni wapinzani. Walio nje ya Marekani wengi watu tulitaka chama tawala kiendelee na utawala na upinzani upotezewe.

Tuko katika mchakato wa kuelekea uchaguzi mkuu hapa Tanzania. Chama kikuu cha upinzani ni cdm, na chama tawala ni ccm. Tulio wanachama na mashabiki wa cdm tulitaka chama tawala Marekani-Democrats waendelee na upinzani-Republican washindwe, na tukafurahi. Hii inaleta picha gani kwetu? Ni nini hasa nguvu ya chama tawala? Labda mazingira yanatofautiana, lakini siasa ni zile zile.

Kwa nini tupende chama tawala kiendelee kwa wenzetu wakati kwetu tunataka kuking'oa?

hili swali inatakiwa kujipanga......sio kukurupuka......
 
hili swali inatakiwa kujipanga......sio kukurupuka......

Ndio maana hii mada ikaja huku, Preta. Ni kweli tunahitaji kulijua hili kwanza kabla ya sisi kufanya maamuzi
 
Ndio maana hii mada ikaja huku, Preta. Ni kweli tunahitaji kulijua hili kwanza kabla ya sisi kufanya maamuzi

Hata miaka minne nyuma, Obama na wenzake walikuwa Chama Pinzani, na kina Romney walikuwa Chama Tawala. Lakini nadhani hata wewe ulitaka Chama Tawala kiangushwe kwa kipindi hiko!
Kumbuka, kinachobeba chama si Uchama Tawala wake wala Uchama Pinzani wake, bali ni IMANI ya watu juu ya Falsafa na Sera za Chama, na committment ya viongozi wa chama husika!
Ndicho kinachotokea leo USA na Hapa kwetu!
Mungu wetu anaita sasa!
 
Hata miaka minne nyuma, Obama na wenzake walikuwa Chama Pinzani, na kina Romney walikuwa Chama Tawala. Lakini nadhani hata wewe ulitaka Chama Tawala kiangushwe kwa kipindi hiko!
Kumbuka, kinachobeba chama si Uchama Tawala wake wala Uchama Pinzani wake, bali ni IMANI ya watu juu ya Falsafa na Sera za Chama, na committment ya viongozi wa chama husika!
Ndicho kinachotokea leo USA na Hapa kwetu!
Mungu wetu anaita sasa!

Ni kweli kuwa kipindi hicho nilitaka chama tawala kiondolewe (Republican). Lakini ukweli mwingine ni kuwa hii imani waliyo nayo watu wetu juu ya chama kilichoko madarakani inatokana na nini? Bila shaka mazingira yana nafasi kubwa sana hapa
 
Kwa nini tupende chama tawala kiendelee kwa wenzetu wakati kwetu tunataka kuking'oa?
Kwa sababu watu hawataki kukiondoa chama madarakani eti kwa sababu tu ni chama tawala. Watu hutaka kukiondoa chama madarakani kwa sababu aidha kimeshindwa kutekeleza ahadi zake au kimeshindwa kuwaletea watu mabadiliko wanayoyahitaji.
 
Hapa tunaangalia ni nani mzalendo na anayeweza kulikwamua hili Taifa kutoka katika hii hali mbaya inayoendelea
 
Naamini upigaji kura wa wenzetu kwa kiasi kikubwa unahusisha tafakari za kina za nani anasema nini na siyo kufuata mkumbo au ushabiki. Ukiangalia mijidala ya wagombea unaona wazi mwisho kuwa mpiga kura anapewa nafasi ya kuwaelewa wagombea, uwezo wao, ufahamu wao na hata msimamo wao.
 
Binafsi nilitegemea kwa mfano cdm iwe bega kwa bega na Republican kwa kuwa hawa wawili ni wapinzani. Lakini kuna tabia kwamba mpinzani akishika madaraka basi huunganisha nguvu na vyama vinavyoshika Dola katika mataifa mengine. Mfano mzuri ulikuwa ni upinzani Kenya dhidi ya KANU, ambapo walikuwa na ukaribu na upinzani nchini. Lakini waliposhika Dola, Odinga alikuja Tanzania kiziara na moja ya kauli yake ni kuwa wao sasa si wapinzani bali wenye Dola
 
Back
Top Bottom