Ujumbe Wangu wa Jumapili Kwenu

Mzigua90

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2014
Posts
38,342
Reaction score
88,625
Maisha mfupi haya kuanza kuingilia maugomvi ya watu usoyajua hata yalipoanzia na wewe kuchukua nafasi ya kugombana na mwingine. Waache wanaogombana wagombane wenyewe maana siku wakipatana utabaki na aibu.

Pia wale tunaogombana na wenzetu tujaribu kutoa tofauti zetu. Tusijenyamaza milele na visasi kwenye mioyo yetu.

Nawatakia week njema inayoanza kesho
 
Wagombanao ndio wapatanao! Rafiki wa leo ni adui wa kesho na kinyume chake!

La muhimu ni kutambua sote tunapita tuu, vinyongo, chuki na fitina visitukoseshe mbingu. Yanapita tuu hayo, la mno ni kupendana na kuheshimiana na zaidi sana kuvumiliana!!
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nimecheka huo mstari wa mwisho ngoja niangalie kama nitaweza kuacha tabia ya kukunywea na kutoa yangu ya moyoni
Hebu uache bwana, hujui tuu unavyonitishaga aki!!
 
Wagombanao ndio wapatanao! Rafiki wa leo ni adui wa kesho na kinyume chake!

La muhimu ni kutambua sote tunapita tuu, vinyongo, chuki na fitina visitukoseshe mbingu. Yanapita tuu hayo, la mno ni kupendana na kuheshimiana na zaidi sana kuvumiliana!!
Heshima yako mkuu, ebu mwambie muhudumu akuongeze moja nitalipa mimi... tehteehhh
 
Kuna ugomvi uliibuka hapa jamvini, mmoja wa wagimbanao akataka kukuingiza Na wewe kwenye ugomvi huo, Mungu ni mwema ulitumia hekima sana kujiepusha
 
Hebu uache bwana, hujui tuu unavyonitishaga aki!!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] halafu tatizo hata nikamwambia niko nakunywa unaogopa unajua nakunywea dada angu kumbe nakupa taarifa tu ujue
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…