Ukahaba,uchangudoa na umalaya. . .. . . . . Kulikoni?

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,891
Nina maswali mawili hapo. . .Moja,je majina ya sifa hizo yana maana sawa?Ni kwanini majina hayo huitwa wanawake tu?Swali la pili,hivi mwanaume nae anaweza kuwa na sifa kama ya ukahaba,changudoa au malaya?Kama siyo kwanini?
 
Mi nitajibu la pili... wapo wanaume wanojiuza tena wengi sana hapa dar na Arusha..wanaosimama barabaran ni wale gays,wasio simama ni wale ambao wanajitegesha tu kwenye ma-bar kuwasubiri mashugamami... Na wanaume malaya pia wapo tena wakutosha tu.
 
HiviHEART,gays ni wanaume?Namaanisha mwanaume kama yule aliyemzungumziaAsprin wakati fulan hivi!Yaani mwanaume anaeitumia jinsia yake ipasavyo anaweza kuwa kahaba,malaya na changudoa wakati huohuo?
 
Eiyer....
Sijui wenngine wanavyoyatumia ila mie nayatumia kwa jinsia zote mbili, kama mwanaume anajiuza nitasema mwanaume huyu ni changupaka, zu mwanaume huyu ni kahaba au kama mwanayme ni malaya nitamwita hivyo pia.........

Subiri wenzetu wenye utaalamu na lugha waje....au una tuki ucheki yanavyotumika?
 
Hivi HEART,gays ni wanaume?Namaanisha mwanaume kama yule aliyemzungumzia Asprin wakati fulan hivi!Yaani mwanaume anaeitumia jinsia yake ipasavyo anaweza kuwa kahaba,malaya na changudoa wakati huohuo?

Bila ubishi yaaani,kwenye kumbi za starehe ni wengi mno...mi mwenyewe nshawashuhudia. Wanafanya vyote hivyo..wanajichubua na kubadilisha hadi miondoko ya kutembea...
 
Last edited by a moderator:
MMMh kumbe me mshamba hivyo!! Sikujua kuwa wanawake wananunua eti!!!!!
 
kwa hiyo mnataka kusema mashoga si wanamme?

Akiambiwa kuandika jinsia huwa wanaandika KE?

Wanamme bana, kila kibaya ni cha mwanamke.

Nashanga!!!!
Wamesahau kuwa mwanaume ni jinsia........ hayo mengine ni characters tu!!
 
HiviHEART,gays ni wanaume?Namaanisha mwanaume kama yule aliyemzungumziaAsprin wakati fulan hivi!Yaani mwanaume anaeitumia jinsia yake ipasavyo anaweza kuwa kahaba,malaya na changudoa wakati huohuo?

Ikiwa mwanaume ndiye yule pekee aliyeelezewa na babu Asprin..........ni wangapi watakuwa wanaume?? Are you??

Yaani wanaume wenzenu wakitenda makosa .......basi mwawageuzia upande wetu, inamaanisha kuwa wanaume hawana mabaya hivyo yote yamfaa mwanamke tu???

Dhana kama hizi zinawafanya mshindwe kujifunza/kujirekebisha na kubaki mkimtazama mwanamke kwa jicho la tuhuma!!
 
Last edited by a moderator:
hapa bila kamusi tunatoana jasho leo, maana haya maneno yameshaanza kutafsiriwa kijenda.

Hata hivyo hata kamusi hizi zilitengenezwa ndani ya mfumo dume, sishangai nazo zikakandamiza upande mmoja.
 
Hahahaha Kipipi kitamu kumbe somo lilikuingia na kulielewa eh? Orayt, come this way baby.....:lock1:
 
Last edited by a moderator:
Bila ubishi yaaani,kwenye kumbi za starehe ni wengi mno...mi mwenyewe nshawashuhudia. Wanafanya vyote hivyo..wanajichubua na kubadilisha hadi miondoko ya kutembea...
Bibie HEART... nenda kafanye homework yako vizuri ili uweze kutofautisha wafuatao:
Mwanaume - mvulana
Mwanaume - gumegume
Mwanaume - Sharobaro
Mwanaume wa kiume..... yaani mwanaume!

Mwanaume mwanaume hawezi kupumuliwa mgongoni wala kumpumulia mwanaume mwenzie mgongoni, PERIOD!!!
 
Last edited by a moderator:
Kwa mimi nadhani hayo maneno yanatumika kotekote ila kwa sababu wanawake wanafanya sana na pia kufanya hadharani ndio maana wanakuwa wanatambulika hivyo sana kuliko wanaume....(Ni issue ya kiuchumi zaidi. Men are natural fighters that's why wanaojiuza ni wachache)

Halafu dada na mama zangu, nawapenda sana >>> Tuwe tunadiscuss mada kama zilivyo na ukweli wake, hizi habari za kufukua gender issues kwenye kila mada zinaharibu ladha ya mada iliyoko. Na mwishowe mtoa mada akakosa cha kuhitimisha..
 
i don't know the kiswahili terms but we have

1) players - a man who multiple girlfriends at a time

2)man wh*r* - a man who has casual sex with many women. it can involve money or just for fun


In red, what 'type' of men are those?
 
jinsia zote majina ni hayohayo ingawa kwa wanaume wao wataonekana ni ujanja au hua wanasemaga huyu jamaa ni moto wa kuotea mbali au jamaa ni noma huyu so wakitumia maneno kama haya yanakua haayana ukali sana.
ivo inakua kama kwa mwanaume ni kama sifa flan ivi ila kwa mdada ni tabia mbaya
 
Sio kwa wanawake au wanaume tu. Hata wanasiasa wanao hama Chama kila kukicha kwa ajili ya maslahi ya matumbo yao nao ni Malaya, Machangudoa na Makahaba wa Kisiasa.
 
Kipipi,BADILI TABIA,Kongosho na HEART,mimi simzungumzii mwanaume ambae ni shoga,kwa sababu anachokifanya ni kinyume na maumbile.Sidhani kama kuna mwanamke ambae ni lesbian halafu akaitwa malaya,changudoa au kahaba kutokana na kutokua mwaminifu kwa ulesbian wake,ataitwa majina hayo kutokana na matumizi halali ya jinsia yake.Na mwanaume ninaemwongelea hapa ni yule ambae si mwaminifu kutokana na matumizi halali ya jinsia yake,je ataitwa kahaba au changudoa?Lakini pia nini tafsiri halali ya maneno hayo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…