Ukaidi wa wenzake ulimnusuru kunyweshwa mkojo wa binadamu!

Ukaidi wa wenzake ulimnusuru kunyweshwa mkojo wa binadamu!

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Nilishaona hilo likifanyika nilipokuwa mdogo. Jirani yetu aliyekunywa sumu alinyweshwa mkojo wa binadamu kwa ajili ya kumtapisha.

Miaka mingi baadaye, nikiwa nimeshahitumu Chuo, tukio kama hilo lilitokea tena jirani na kwetu. Binti mmoja alikunywa sumu, na kabla ya kukimbizwa hospitalini, alinyweshwa mkojo wa binadamu na kisha kutapishwa.

Sikufikiri kama na mimi ningekuja kuliunga mkono hilo wazo. Hata sikujua kama nilikuwa ninaamini kwamba mkojo unaweza kutumika kama "dawa". Lakini unapokuwa katika dharura, ndipo kile unachokiamini huweza kuthihirika. Aliye vitani katika mazingira ya hatari hachagui silaha.

Miaka ya 2000, nilikuwa nikifanya kazi katika shule fulani mikoani "huko".

Siku moja, wakati wa mapumziko, wanafunzi walinifuata na kuniambia mwenzao wa kiume kanywa sumu bwenini! Nilifuatana nao hadi bwenini alimokuwa huyo mwanafunzi.

Nilipofika na kumkuta amelala sakafuni haongei, nilipatwa na taharuki. Haraka niliwaambia wambebe, nikakimbia nao hadi kwenye gari na kumwambia dereva atukimbize hospitalini.

Nakumbuka nilikuwepo mimi, dereva na wanafunzi kadhaa wa kiume.

Ndipo wazo la mkojo liliponijia. Lakini nilipowaambia wanafunzi niliokuwa nao wampe mwenzao msaada wa mkojo, ni kama vile hakuna aliyenielewa. Nikarudia tena kuwaelesha, kuwa mmoja wao amkojolee kinywani kwa sababu mkojo utamfanya atapike, lakini hawakunitii japo si kawaida yao.

Nilipokosa ushirikiano wao, niliamua kuachana na hilo wazo. Lakini njiani tulinunua maziwa freshi na kumnywesha.

Tulimfikisha hospitalini na alipata huduma, na kesho yake aliruhusiwa.

Ilikuwa kila nikilikumbuka hilo najikuta nacheka. Sikujua kuwa na mimi nilikuwa ninaamini katika kutumia mkojo kama dawa ya kupunguza makali ya sumu.

Nilijikuta ninawaza
1. Kama hao wanafunzi wangetii, na katika harakati za kumnywesha mkojo kwa kutumia viungo vyao(hatukuwa na chombo cha kukingia mkojo), na ikatokea akang'atwa na anyenyweshwa mkojo, ingekuwaje?

2. Tungefika hospitalini na kuwaambia kuwa tulimnywesha mkojo, ningeelewekaje?

3. Wanafunzi wenzake wasingemkejeli baada ya kupona?

Ingawa mwanzoni niliwakasirikia hao wanafunzi, baada ya kutulia, nilijikuta nashukuru kwa kutokutii kwao!

1. Waliniepusha na sintofahamu ambayo ingeibuka!

2. Walimwepusha mwenzao kunywa mkojo wa binadamu!

Ingawa sina uhakika kama kweli mkojo wa binadamu ni tiba ya mtu aliyekunywa sumu, lakini nafurahi kwa kutokutii kwa hao wanafunzi.

Na cha kumshukuru Mungu zaidi ni kuwa ingawa huyo mwanafunzi hakunyweshwa mkojo, aliweza kupata huduma hospitalini na kesho yake kuruhusiwa.
 
Mimi kama miezi kadhaa nyuma nilisoma huku kuhusu mkojo, kuondoa nuksi na mikosi, sikuchukua poa, nikaenda gugo nakuona kuwa mkojo wa kwanza asubuhi ni tiba ya magonjwa mengi na huleta mwonekano mzuri wa ngozi. Watu kadhaa wameshuhudia kutumia urine therapy kila siku kwaajili y kujiepusha na magonjwa mbalimbali.
Tangu wakati huo, nilianza kutumia mkojo wa kwanza asubuhi kujisugua kwenye ngozi yangu, mwili mzima, hakika nimekuwa na rangi nzuri sana ya kupendeza. Na mara chache huwa nakunywa kiasi na kupigia mswaki. Ukinywa unatapika so ni kweli anayekunywa sumu, akipewa mkojo atatapika na kupunguza sumu.

Kwasasa situmii kipodozi chochote zaidi ya urine therapy. Na hunielezi chochote kuhusu kojo, ha ha ha.

Naishukuru sana JF ina mambo mengi, watu wana mengi sana ya kutufundisha.
 
Mkojo wa binadamu? We acha tu, ulikuwa unatumika kama dawa ya vidonda kichwani na upele mwilini unaogeshwa nayo. Unavundikwa kwenye chombo kinaitwa sururu/kibuyu. Unanuka balaa na pia ulikuwa unatumika kama kitisho kutoa adhabu kwa mtoto mtukutu/mtundu/mkorofi na mbishi asiyetii wazazi wake. Hata maziwa ya mtu yalitumika kumkamulia aliyetemewa mate na nyoka machoni au aliyetoswa na minyaa machoni. Ustaarabu umebadilisha hayo na dawa za kisasa zipo hospitalini
 
Mimi kama miezi kadhaa nyuma nilisoma huku kuhusu mkojo, kuondoa nuksi na mikosi, sikuchukua poa, nikaenda gugo nakuona kuwa mkojo wa kwanza asubuhi ni tiba ya magonjwa mengi na huleta mwonekano mzuri wa ngozi. Watu kadhaa wameshuhudia kutumia urine therapy kila siku kwaajili y kujiepusha na magonjwa mbalimbali.
Tangu wakati huo, nilianza kutumia mkojo wa kwanza asubuhi kujisugua kwenye ngozi yangu, mwili mzima, hakika nimekuwa na rangi nzuri sana ya kupendeza. Na mara chache huwa nakunywa kiasi na kupigia mswaki. Ukinywa unatapika so ni kweli anayekunywa sumu, akipewa mkojo atatapika na kupunguza sumu.

Kwasasa situmii kipodozi chochote zaidi ya urine therapy. Na hunielezi chochote kuhusu kojo, ha ha ha.

Naishukuru sana JF ina mambo mengi, watu wana mengi sana ya kutufundisha.
Unaweza kunywa wa mtu mwingine?
 
Mkojo wa binadamu? We acha tu, ulikuwa unatumika kama dawa ya vidonda kichwani na upele mwilini unaogeshwa nayo. Unavundikwa kwenye chombo kinaitwa sururu/kibuyu. Unanuka balaa na pia ulikuwa unatumika kama kitisho kutoa adhabu kwa mtoto mtukutu/mtundu/mkorofi na mbishi asiyetii wazazi wake. Hata maziwa ya mtu yalitumika kumkamulia aliyetemewa mate na nyoka machoni au aliyetoswa na minyaa machoni. Ustaarabu umebadilisha hayo na dawa za kisasa zipo hospitalini
Tulilotoka ni mbali! Vizazi vijavyo vitashangaa vitakapokuja kusimuliwa.
 
Nilishaona hilo likifanyika nilipokuwa mdogo. Jirani yetu aliyekunywa sumu alinyweshwa mkojo wa binadamu kwa ajili ya kumtapisha.

Miaka mingi baadaye, nikiwa nimeshahitumu Chuo, tukio kama hilo lilitokea tena jirani na kwetu. Binti mmoja alikunywa sumu, na kabla ya kukimbizwa hospitalini, alinyweshwa mkojo wa binadamu na kisha kutapishwa.

Sikufikiri kama na mimi ningekuja kuliunga mkono hilo wazo. Hata sikujua kama nilikuwa ninaamini kwamba mkojo unaweza kutumika kama "dawa". Lakini unapokuwa katika dharura, ndipo kile unachokiamini huweza kuthihirika. Aliye vitani katika mazingira ya hatari hachagui silaha.

Miaka ya 2000, nilikuwa nikifanya kazi katika shule fulani mikoani "huko".

Siku moja, wakati wa mapumziko, wanafunzi walinifuata na kuniambia mwenzao wa kiume kanywa sumu bwenini! Nilifuatana nao hadi bwenini alimokuwa huyo mwanafunzi.

Nilipofika na kumkuta amelala sakafuni haongei, nilipatwa na taharuki. Haraka niliwaambia wambebe, nikakimbia nao hadi kwenye gari na kumwambia dereva atukimbize hospitalini.

Nakumbuka nilikuwepo mimi, dereva na wanafunzi kadhaa wa kiume.

Ndipo wazo la mkojo liliponijia. Lakini nilipowaambia wanafunzi niliokuwa nao wampe mwenzao msaada wa mkojo, ni kama vile hakuna aliyenielewa. Nikarudia tena kuwaelesha, kuwa mmoja wao amkojolee kinywani kwa sababu mkojo utamfanya atapike, lakini hawakunitii japo si kawaida yao.

Nilipokosa ushirikiano wao, niliamua kuachana na hilo wazo. Lakini njiani tulinunua maziwa freshi na kumnywesha.

Tulimfikisha hospitalini na alipata huduma, na kesho yake aliruhusiwa.

Ilikuwa kila nikilikumbuka hilo najikuta nacheka. Sikujua kuwa na mimi nilikuwa ninaamini katika kutumia mkojo kama dawa ya kupunguza makali ya sumu.

Nilijikuta ninawaza
1. Kama hao wanafunzi wangetii, na katika harakati za kumnywesha mkojo kwa kutumia viungo vyao(hatukuwa na chombo cha kukingia mkojo), na ikatokea akang'atwa na anyenyweshwa mkojo, ingekuwaje?

2. Tungefika hospitalini na kuwaambia kuwa tulimnywesha mkojo, ningeelewekaje?

3. Wanafunzi wenzake wasingemkejeli baada ya kupona?

Ingawa mwanzoni niliwakasirikia hao wanafunzi, baada ya kutulia, nilijikuta nashukuru kwa kutokutii kwao!

1. Waliniepusha na sintofahamu ambayo ingeibuka!

2. Walimwepusha mwenzao kunywa mkojo wa binadamu!

Ingawa sina uhakika kama kweli mkojo wa binadamu ni tiba ya mtu aliyekunywa sumu, lakini nafurahi kwa kutokutii kwa hao wanafunzi.

Na cha kumshukuru Mungu zaidi ni kuwa ingawa huyo mwanafunzi hakunyweshwa mkojo, aliweza kupata huduma hospitalini na kesho yake kuruhusiwa.
DR Mambo Jambo
 
Mkojo pia unaleta bahati,yani unaweza ukapata kitu usichokitarajia au jambo zuri usilotarajia,.....apa nna ushahidi
 
Mimi kama miezi kadhaa nyuma nilisoma huku kuhusu mkojo, kuondoa nuksi na mikosi, sikuchukua poa, nikaenda gugo nakuona kuwa mkojo wa kwanza asubuhi ni tiba ya magonjwa mengi na huleta mwonekano mzuri wa ngozi. Watu kadhaa wameshuhudia kutumia urine therapy kila siku kwaajili y kujiepusha na magonjwa mbalimbali.
Tangu wakati huo, nilianza kutumia mkojo wa kwanza asubuhi kujisugua kwenye ngozi yangu, mwili mzima, hakika nimekuwa na rangi nzuri sana ya kupendeza. Na mara chache huwa nakunywa kiasi na kupigia mswaki. Ukinywa unatapika so ni kweli anayekunywa sumu, akipewa mkojo atatapika na kupunguza sumu.

Kwasasa situmii kipodozi chochote zaidi ya urine therapy. Na hunielezi chochote kuhusu kojo, ha ha ha.

Naishukuru sana JF ina mambo mengi, watu wana mengi sana ya kutufundisha.
Duh unakbiliana vipi na harufu sasa?
 
Back
Top Bottom