Ukakasi wa majibu ya Naibu Waziri juu ya ongezeko la bei ya Sukari Nchini

Ukakasi wa majibu ya Naibu Waziri juu ya ongezeko la bei ya Sukari Nchini

Joined
Oct 7, 2019
Posts
51
Reaction score
157
Mwaka 1879 Malkia aliyekuwa anaiongoza Ufaransa Bi Marie Antoniette aliambiwa wananchi wake hawana Mikate akajibu kwa kifaransa “Qu’ils mangent de la brioche” kwa maana ya kiingereza “Let them eat cake" kwa kiswahili kisicho rasmi Sana ni kuwa Waambie wale Keki.

Inatajwa kuwa Brioche waliyoambiwa wale kilikuwa Chakula Cha matajiri Sana Ufaransa, ambacho kwa walalahoi wa Ufaransa walikuwa hawawezi kukinunua ndio maana walikuwa wanahitaji mikate. Baada ya kauli ile Kutoka Malkia alipinduliwa na wananchi wenye hasira Kali.

Leo naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Bi Stella Manyanya ameambiwa Sukari imepanda Bei na kufikia shilingi 3000 kwa kilo Moja yeye akajibu watu watumie asali. Kitu ambacho Manyanya hajui ni kuwa asali Ni ghali kuliko Sukari na asali kwa Sasa Ni Chakula Cha matajiri.

Lita Moja tu ya asali ni shilingi 10,000 sawa na kilo tatu za Sukari za mlalahoi. Manyanya yeye kununua hata ndoo ya Asali si big issue kipato kinaruhusu. Nafikiria familia ya watu watano pale kijijini ambao kipato cha Kaya Ni shilingi elfu 3 kwa siku au chini ya hapo wanaweza kununua lita Moja ya Asali? Je, wataitumia siku ngapi?

Asali siku hizi ni anasa kubwa Sana kwa watu Manyanya asitutukane. Najiuliza je, asali inafaa kutumika kwenye kuoka Mikate? Kwenye utengenezaji wa vinywaji huku kijijini? Kwenye maandazi tutaweka asali?

Ni kweli kuwa Manyanya hawezi kutengeneza Mbinu za Sukari kushuka Bei? Yaani akili yake imeshindwa kumnasua mlalahoi wa Tanzania ambaye Chai ndio kinywaji chake Cha kifahari? Sasa tunamlipa mshara na kumpa V8 la Nini Kama hata Jambo dogo hivi anashindwa kulitatua?

Akili kubwa ni Mali ya Rais, ndio wanaotakiwa kumzunguka Rais hawa ndio akili kubwa ya Tanzania ambayo inatakiwa kuhudumia watanzania?

Albert Einstein aliwahi kusema "We can't solve problems by using the same kind of thinking we used when we created them" huyu jamaa alikuwa na akili sana yaani akili iliyotengeneza tatizo haiwezekani ikatatua tatizo hilo.

Tunawaza kidogo sana Manyanya aangalie hata wenzetu huko njee wanafanyaje hasa katika kipindi hiki Cha Korona.
 
Tatizo sio serikali...tatizo ni wafanyabiashara wenyewe wanatumia mbinu chafu kuficha sukari(hoarding) ili ipande bei watuuzie bei kubwa.
 
Tatizo sio serikali...tatizo ni wafanyabiashara wenyewe wanatumia mbinu chafu kuficha sukari(hoarding) ili ipande bei watuuzie bei kubwa.
Hivi hawa wafanyabiashara wanakaa ulaya mbona watu wakiandika tu matusi kwenye twita wanakamatwa hawa wanaishi wapi
 
Kuna kipindi bei ya sukari ilipanda sana hapa nchini lakin kutokana na kushuka kwa thamani ya kwacha nchini Zambia ilikua ukinunua kwacha kwa tsh na kwenda kununua sukari Zambia unaipata kwa bei ya chini.

Nakumbuka bei iliyokuwepo kwa kl1 ya sukar tz ni sawa na kl2 za sukari ukinunulia Zambia, watu kibao walipiga sana pesa kipindi kile. Cha kushangaza naona ile hali imejirudia sasa ivi. Bei ya sukari imepanda sana na kutokana na thamani ya kwacha kuporomoka ukienda kununua sukari Zambia bei ipo chini, kuna nini?

1kwacha=126tsh

Katoni inauzwa elfu k280 ambayo ukiibadili unapata 35280tsh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna kipindi bei ya sukari ilipanda sana hapa nchini lakin kutokana na kushuka kwa thamani ya kwacha nchini Zambia ilikua ukinunua kwacha kwa tsh na kwenda kununua sukari Zambia unaipata kwa bei ya chini.

Nakumbuka bei iliyokuwepo kwa kl1 ya sukar tz ni sawa na kl2 za sukari ukinunulia Zambia, watu kibao walipiga sana pesa kipindi kile. Cha kushangaza naona ile hali imejirudia sasa ivi. Bei ya sukari imepanda sana na kutokana na thamani ya kwacha kuporomoka ukienda kununua sukari Zambia bei ipo chini, kuna nini?

1kwacha=126tsh

Katoni inauzwa elfu k280 ambayo ukiibadili unapata 35280tsh

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata kwa sasa Tunduma sukari 2000 kwa kilo hivyo tunavyosikia sukari 3000 watz wa mpakani wanashangaa maana wao wananunua 1800-2000 kwa kilo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom