white wizard
JF-Expert Member
- May 18, 2011
- 8,566
- 13,770
Wanaangalia na ukubwa wa tukio(vifo) ila hata hivyo mkoa wa mwanza una upendeleo wake wa kipekee awamu hii!! Tambua hiloKwani kwenye tetemeko la ardhi la Bukoba tuliomboleza siku tatu?
Haya ndio Mazito ???"Kuhusu hoja yangu niliyoitoa bungeni ilifanyiwa kazi na Serikali kwa haraka sana na vizuri ambapo tulikuwa Tunahitaji injini mbili ambazo zilipatikana na zikafungwa vizuri labda tu suala ambalo lilikuwa bado tunalifanyia kazi ni kuona namna ya kupunguza idadi ya safari Mengine tumuachie Mungu"
Joseph Mkundi.
Mbunge wa Ukerewe chadema.View attachment 874209
Amenunuliwa huyu. Hata, haiwezekani aseme hivyo.Wakati zoezi la uopoaji miili ya wahanga wa ajali ya maji iliyotokana na kivuko cha Mv Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Kisiwa cha Ukara na Bugorora wilayani Ukerewe, Mbunge wa Ukerewe, Joseph Mkundi amesema kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati.
Amesema kuwa Kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati miezi miwili iliyopita, hivyo kilikuwa sawa na kilikuwa mbioni kubadilishiwa ratiba ikiwemo kuongeza idadi ya safari ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa eneo hilo.
“Kuhusu hoja yangu niliyoitoa bungeni, ilifanyiwa kazi ambapo tulikuwa tunahitaji injini mbili ambazo zilipatikana na zikafungwa labda tu suala ambalo lilikuwa bado tunalifanyia kazi ni kuona namna gani tunaweza kubadilisha idadi ya safari”, amesema Mkundi
Aidha, amesema kuwa yeye mwenyewe ni miongoni wa watu waliopoteza ndugu katika ajali hiyo ambapo amedai kuwa takribani ndugu zake watatu wamefariki kwenye ajali hiyo.
Huyu jamaa ataitwa msaliti very soon."Kuhusu hoja yangu niliyoitoa bungeni ilifanyiwa kazi na Serikali kwa haraka sana na vizuri ambapo tulikuwa Tunahitaji injini mbili ambazo zilipatikana na zikafungwa vizuri labda tu suala ambalo lilikuwa bado tunalifanyia kazi ni kuona namna ya kupunguza idadi ya safari Mengine tumuachie Mungu"
Joseph Mkundi.
Mbunge wa Ukerewe chadema.View attachment 874209
Anajifariji tuAisee kumbe watu wapo kazini
Daah pole sana mkuu...najua umetumia ujasiri mkubwa kuweza kuandika hivi ijapokuwa upo majonzini.....msamehe mleta mada!!!Inatia uchungu sana unapogundua mtu uliyekuwa unamheshimu kuwa ni mtu makini na mwenye busara ndani ya JF ni "bwege na mlamba viatu" Mimi nimefiwa na ndugu zangu kwa uzembe wa serikali siwezi kupokea maoni ya kipumbavu kama haya ya kwako mleta mada na vimada wenzio. Naijua MV Nyerere, naijua MV Ukara. Najua matatizo yake siku nyingi na jinsi tatizo la usafiri lilivyo kubwa Ukara na Ukerewe kwa ujumla. Najua upuuzi wa wapuuzi wanaoshughulikia usafiri wa majini ndani ya ziwa Victoria. Kama ajali ingetokea siku 2 nyuma Mimi nisingekuwa naandika hapa na picha ya maiti yangi ingekuwa mitandaoni ingawaje wengine wasingejua huyu ndiye Bila bila. Kazi yangu imenipeleka katika visiwa hivi vya Ukerewe, Ukara, Kweru, Ilugwa, Kamasi nk. Naongea ninachokijua, hivyo watu wanapolaumu serikali wanajua wanachokiongea kwa jinsi kifo kilivyokuwa usoni mwetu kila siku tunayopanda kivuko hiki. Nanyamaza ila Mungu anawaona nyie wenye HERI.
Duh..! Wabongo kwa kupenda raha...Kutokana na msiba uliolikumba Taifa na Mkuu katangaza Siku NNE za maombolezo.
Je tunaomboleza tukiwa job au home?
Mkuu inawezekana kuzama kabisa nchi kavu kama ilivyotokea! mimi kidogo nimewahi kuwa dereva wa mitumbwi ziwani! injini ikiwa inatembea au chombo kikiwakinatembea kule mbele kwenye mtumbwi kunainuka kwa sababu ya mkandamizo wa injini/propela zilizoko nyuma. kwa hiyo wakati meri ikiwa inatembea inaweza isiwerahisi kuzama kwa sababu ya mzigo uliokombele! lakini kunauwezekano mkubwa wa chombo kuzama kama ukipunguza mwendo gafla na kukawa na mzigo mzito kwa mbele! mimi naamini kwa 80%. inaweza kuwa ni sababu iliyopelekea chombo kile kuzama!! Mzigo ulikimbilia mbele wakati injini tayari ilikuwaimepunguzwa mwendo gafla!Bro,mimi nakiri ili-overload kwa mujibu wa takwimu. Lkn niamini usiniamini,pale kuna kosa lingine kubwa litakuwa lilifanyika hapo. Haingewezekana kamwe isafiri umbali mrefu kiasi kile salama na ikamudu kuyavuka mawimbi makubwa ambayo yangetosha kuizamisha then ije iangukie kwane eneo ambalo maji yana utulivu km maji kwene ndoo. Kulikuwa na tatizo la kiuendeshaji pia na hasa hasa ndilo limetuulia ndugu zetu.
Nchi hii ni ubatili mtupu. Hii haitofautiani na Mama yuko nyumbani anajifanya yuko busy na kufua nguo, huku mwanae katumbukia kwenye sufuria la chakula likiwa jikoni likichemka na kupelekea mtoto kufariki. Sasa huyo mama mtamuona kuwa ana akili? ndo uongozi wetu ulivyo, watu hawawajibiki wako kujikweza tu ningeona la maana nchi ingekuwa na mipango thabiti ya maisha ya watu badala ya kutafuta misifa isiyo na tijaVipaumbele ndo tatizo..tutapata tabu sana kwakweli..
Nahodha aliyefariki ni Deiwaka tu(alipewa aendeshe ingawa hausiki na uendeshaji wa Mv nyerere).Nahodha ambaye ndo alitakiwa kusafiri na chombo ndo huyo ameshikiliwa na polisi kwa kosa la kumuachia Deiwaka aendeshe.Hapo kwa nahodha bado kuna utata, mara anashikiliwa na jeshi la police mara amefariki yupo chini....sasa ipi sahihi??. Watulie hadi mwisho na kama hawamjui nahodha bado wafunge vinywa vyao tu
Wakati zoezi la uopoaji miili ya wahanga wa ajali ya maji iliyotokana na kivuko cha Mv Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Kisiwa cha Ukara na Bugorora wilayani Ukerewe, Mbunge wa Ukerewe, Joseph Mkundi amesema kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati.
Amesema kuwa Kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati miezi miwili iliyopita, hivyo kilikuwa sawa na kilikuwa mbioni kubadilishiwa ratiba ikiwemo kuongeza idadi ya safari ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa eneo hilo.
“Kuhusu hoja yangu niliyoitoa bungeni, ilifanyiwa kazi ambapo tulikuwa tunahitaji injini mbili ambazo zilipatikana na zikafungwa labda tu suala ambalo lilikuwa bado tunalifanyia kazi ni kuona namna gani tunaweza kubadilisha idadi ya safari”, amesema Mkundi
Aidha, amesema kuwa yeye mwenyewe ni miongoni wa watu waliopoteza ndugu katika ajali hiyo ambapo amedai kuwa takribani ndugu zake watatu wamefariki kwenye ajali hiyo.
Bro,mimi nakiri ili-overload kwa mujibu wa takwimu. Lkn niamini usiniamini,pale kuna kosa lingine kubwa litakuwa lilifanyika hapo. Haingewezekana kamwe isafiri umbali mrefu kiasi kile salama na ikamudu kuyavuka mawimbi makubwa ambayo yangetosha kuizamisha then ije iangukie kwane eneo ambalo maji yana utulivu km maji kwene ndoo. Kulikuwa na tatizo la kiuendeshaji pia na hasa hasa ndilo limetuulia ndugu zetu.
Mtoa mada ana viashiria vyote vya mwenye kichaa cha kurithi. Ana tabia ya kuandama mtu wakati wote kwa visababu vya kuokoteza. Pili hakuna tiba ya kawaida iwezayo kumsaidia. LAKINI akikubali kuliweka wazi tatizo lake anaweza KUOMBEWA, akapona akawa mtu mpya. Amen.Mkuu sijaona sehemu amemshukia kama mwewe.Au ulikusudia tu kunogesha uzi
Duuh chuki uleta upofuYote aliyoyasema kwenye press ya Jana ni uongo mtupu. Mbunge wa Ukerewe kuweka kula kitu hadharani soon kuhusu hoja take ya kivuko aliyoitoa bungeni. Stay tuned nitawajuza kupitia hapa hapa!