Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,509
- 3,756
Mwongozo ulioombwa bungeni jijini Dodoma na mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally Keissy akitaka wabunge kuichangia klabu ya Yanga umekwama baada ya wawakilishi hao wa wananchi kupinga hoja hiyo.
Keissy ameomba mwongozo huo leo asubuhi Aprili 5, 2019 baada ya Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kuitambulisha kamati ya kuhamasisha kuichangia Yanga ya jijini hapa iliyoalikwa kutembelea Bunge.
Keissy amesema kutokana na uwepo wa kamati hiyo, ni vyema likapitishwa kapu bungeni ili wabunge waweze kuichangia klabu hiyo ambayo jana ilitoka sare ya bao 1-1 na Ndanda katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
“Keissy amezungumza kuhusu kuichangia Yanga na mwongozo wake anazungumzia kapu kuletwa hapa (bungeni) kulingana na matangazo yaliyopo. Kwa kuwa wote tunamfahamu Keissy kuhusu mchango tumkubalie kwa maana tukatwe fedha ili,” amesema Dk Tulia ambaye alishindwa kumalizia kauli yake kutokana wabunge kuanza kupaza sauti, kuzungumza bila kufuata utaratibu.
“Wabunge tusikilizane, naomba tusikilizane waheshimiwa wabunge, nimeombwa mwongozo hapa na hili jambo linahusu wabunge kuridhia kwa mujibu wa Keissy na pendekezo lake.”
Sent using Jamii Forums mobile app
Keissy ameomba mwongozo huo leo asubuhi Aprili 5, 2019 baada ya Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kuitambulisha kamati ya kuhamasisha kuichangia Yanga ya jijini hapa iliyoalikwa kutembelea Bunge.
Keissy amesema kutokana na uwepo wa kamati hiyo, ni vyema likapitishwa kapu bungeni ili wabunge waweze kuichangia klabu hiyo ambayo jana ilitoka sare ya bao 1-1 na Ndanda katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
“Keissy amezungumza kuhusu kuichangia Yanga na mwongozo wake anazungumzia kapu kuletwa hapa (bungeni) kulingana na matangazo yaliyopo. Kwa kuwa wote tunamfahamu Keissy kuhusu mchango tumkubalie kwa maana tukatwe fedha ili,” amesema Dk Tulia ambaye alishindwa kumalizia kauli yake kutokana wabunge kuanza kupaza sauti, kuzungumza bila kufuata utaratibu.
“Wabunge tusikilizane, naomba tusikilizane waheshimiwa wabunge, nimeombwa mwongozo hapa na hili jambo linahusu wabunge kuridhia kwa mujibu wa Keissy na pendekezo lake.”
Sent using Jamii Forums mobile app