Ukifikiria vizuri utaona kuwa dini zote zilianzishwa na watu kama Zumaridi

Ukifikiria vizuri utaona kuwa dini zote zilianzishwa na watu kama Zumaridi

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Ni kwamba tu dini hizi zilianzishwa zamani sana ndiyo maana tunaona sawa. Mimi ni mkristo, lakini leo atokee Seremala aanze kusema ni mwana wa Mungu na katoka mbinguni lazima kila mtu ashtuke na kumuona hayupo sawa kichwani.

Akitokea mtu akisema anashushiwa aya na malaika kutoka kwa Mungu lazima kila mtu amuone ni muongo na tapeli.

Musa kusema amekutana na Mungu mlimani amemtuma kukomboa watu lazima ingekuwa kitu cha kutilia shaka sana. Hasa ukizingatia watu kama yeye huibuka sana jamii inapokuwa kwenye matatizo, kama utumwani.

Dini pekee ambayo iliundwa kwa mtu kufanya tafakari ya kina ni ubudha.

My take. Hakuna haja ya kumshangaa Zumaridi kusema alienda mbinguni. Hakuna haja ya kumshangaa Geordavie kusema alitokewa na Yesu.

Na kama TCRA inataka kubana hao kwa kuita wanamawazo ya kufikirika basi wakataze kurushwa kwa habari zote za dini maana zote ni za kufikirika.
 
Ni kwamba tu dini hizi zilianzishwa zamani sana ndiyo maana tunaona sawa. Mimi ni mkristo, lakini leo atokee Seremala aanze kusema ni mwana wa Mungu na katoka mbinguni lazima kila mtu ashtuke na kumuona hayupo sawa kichwani...
Tatizo huna elimu ya Dini, hao mitume uliowataja walianza kuandaliwa wakiwa bado wangali wadogo, halafu wewe unalinganisha na story za huyu chizi?
 
Ni kwamba tu dini hizi zilianzishwa zamani sana ndiyo maana tunaona sawa. Mimi ni mkristo, lakini leo atokee Seremala aanze kusema ni mwana wa Mungu na katoka mbinguni lazima kila mtu ashtuke na kumuona hayupo sawa kichwani...
Tambua wanadamu hawa kujua kitu kinacho itwa mungu au kuumbwa kwao,mpaka hapa alipo jitokeza mtu wa kwamza adamu akawaeleza watoto wake kuhusu chanzo chao ilikuwa ngumu kupinga ni sawa na baba yako akusimulie chimbuko lake alafu ukamkatalia utakuwa huna akili timamu
 
Ni kwamba tu dini hizi zilianzishwa zamani sana ndiyo maana tunaona sawa. Mimi ni mkristo, lakini leo atokee Seremala aanze kusema ni mwana wa Mungu na katoka mbinguni lazima kila mtu ashtuke na kumuona hayupo sawa kichwani...

Mkuu, ni hivi, tangu zamani kulikuwa na namna ya kuwachuja manabii, na hata leo maelekezo yapo jinsi ya kuchuja uongo na ukweli.

usipo kuwa mwerevu na unayejua mambo ya Mungu utadanganyika. ni rahis kupotezwa.

Hivyo alipotokea mtu akadai ni nabii au mtume alipimwa. Hata zumaridi anatakiwa kupimwa kwa vigezo na kuwekwa kunakostahili


Kumbukumbu 13:1-3 “Kukizuka katika yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia, akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; wewe usiyasikilize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto…”

Kutokana na andiko hili hapa juu linaonyesha wazi ya kwamba tunaweza kuwatambua manabii wanaopotosha kwa mambo yale wanayotuambia au kutuelekeza kinyume na neno la Mungu. Na ikiwa hawana matunda mazuri hao ni manabii wa uongo. Ndio maana imeandikwa; Mathayo 7:15-20 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa - mwitu wakali. Mtawatambua kwa matunda yao. Je! watu huchukua zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.

Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.” Mfano wa mti mwema ni yule mtu anayeyafanya mapenzi ya Mungu (matakwa ya Mungu). Na mfano wa mti mwovu ni mtu asiyeyafanya mapenzi ya Mungu.

7.Unabii walioutoa ulilingana na neno la Mungu. Haukupigana na neno la Mungu mahali popote katika biblia. Mwamini anaweza kuutambua unabii kwa kutumia neno la Mungu. Lakini ni lazima kwanza ayafahamu maneno ya Mungu na kuyahifadhi moyoni.

Wakolosai 3:16

"Na neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote…” Mtu akiwa na maneno ya Mungu kwa wingi moyoni anaweza kuyapima mambo yote ya Kiroho.

Jinsi ya kuwatambua manabii wa uongo. Ni kwa njia zifuatazo;
1. Tunaweza kuwatambua au kuwapambanua kwa tabia zao ambazo haziendani na neno la Mungu na ziko dhahiri wala haziwezi kufichika. Tunaweza kuwatambua kwa kutumia neno la Mungu na tunda la Roho.
Wagalatia 5:22-23.

“Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.”

2. Kuwatambua kwa mafundisho yao ya kibinadamu. Mafundisho yao wameyatunga hayaendani na neno la Mungu. Wanafundisha na kuhubiri kwa kutafsiri mistari ya biblia kinyume neno la Mungu. Kwa sababu hiyo wanakuwa wamewapotosha waamini katika njia ya Mungu. Hutumia mafundisho ya uzushi na uongo na kuyachanganya na maandiko ya neno la Mungu kana kwamba ni neno la Mungu. Kwa sababu hiyo huwapotosha wasiolijua neno la Mungu kwa ukamilifu. Ikiwa mwamini yuko makini na anayafahamu maandiko kwa ukamilifu ni lazima atagundua ya kwamba mafundisho wanayofundisha na kuyahubiri yanapingana na neno la Mungu katika biblia. Ndio maana imeandikwa tusiamini kila roho (kila nafsi) tuzijaribu kwanza. 1Yohana 4:1.

“Wapenzi msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.”

Kujua maandiko ni muhimu sana
 
Yba tu dini hizi zilianzishwa zamani sana ndiyo maana tunaona sawa. Mimi ni mkristo, lakini leo atokee Seremala aanze kusema ni mwana wa Mungu na katoka mbinguni lazima kila mtu ashtuke na kumuona hayupo sawa kichwani.
Akitokea mtu akisema anashushiwa aya na malaika kutoka kwa Mungu lazima kila mtu amuone ni muongo na tapeli.

Musa kusema amekutana na Mungu mlimani amemtuma kukomboa watu lazima ingekuwa kitu cha kutilia shaka sana. Hasa ukizingatia watu kama yeye huibuka sana jamii inapokuwa kwenye matatizo, kama utumwani...
Yesu alisema hata wewe ni mwana wa Mungu
 
Mkuu, ni hivi, tangu zamani kulikuwa na namna ya kuwachuja manabii, na hata leo maelekezo yapo jinsi ya kuchuja uongo na ukweli
usipo kuwa mwerevu na unayejua mambo ya Mungu utadanganyika. ni rahis kupotezwa.
Hivyo alipotokea mtu akadai ni nabii au mtume alipimwa. Hata zumaridi anatakiwa kupimwa kwa vigezo na kuwekwa kunakostahili


Kumbukumbu 13:1-3 “Kukizuka katika yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia, akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; wewe usiyasikilize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto…”

Kutokana na andiko hili hapa juu linaonyesha wazi ya kwamba tunaweza kuwatambua manabii wanaopotosha kwa mambo yale wanayotuambia au kutuelekeza kinyume na neno la Mungu. Na ikiwa hawana matunda mazuri hao ni manabii wa uongo. Ndio maana imeandikwa; Mathayo 7:15-20 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa - mwitu wakali. Mtawatambua kwa matunda yao. Je! watu huchukua zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.” Mfano wa mti mwema ni yule mtu anayeyafanya mapenzi ya Mungu (matakwa ya Mungu). Na mfano wa mti mwovu ni mtu asiyeyafanya mapenzi ya Mungu.

7.Unabii walioutoa ulilingana na neno la Mungu. Haukupigana na neno la Mungu mahali popote katika biblia. Mwamini anaweza kuutambua unabii kwa kutumia neno la Mungu. Lakini ni lazima kwanza ayafahamu maneno ya Mungu na kuyahifadhi moyoni.
Wakolosai 3:16
"Na neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote…” Mtu akiwa na maneno ya Mungu kwa wingi moyoni anaweza kuyapima mambo yote ya Kiroho.

Jinsi ya kuwatambua manabii wa uongo. Ni kwa njia zifuatazo;
1. Tunaweza kuwatambua au kuwapambanua kwa tabia zao ambazo haziendani na neno la Mungu na ziko dhahiri wala haziwezi kufichika. Tunaweza kuwatambua kwa kutumia neno la Mungu na tunda la Roho.
Wagalatia 5:22-23
“Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.”

2. Kuwatambua kwa mafundisho yao ya kibinadamu. Mafundisho yao wameyatunga hayaendani na neno la Mungu. Wanafundisha na kuhubiri kwa kutafsiri mistari ya biblia kinyume neno la Mungu. Kwa sababu hiyo wanakuwa wamewapotosha waamini katika njia ya Mungu. Hutumia mafundisho ya uzushi na uongo na kuyachanganya na maandiko ya neno la Mungu kana kwamba ni neno la Mungu. Kwa sababu hiyo huwapotosha wasiolijua neno la Mungu kwa ukamilifu. Ikiwa mwamini yuko makini na anayafahamu maandiko kwa ukamilifu ni lazima atagundua ya kwamba mafundisho wanayofundisha na kuyahubiri yanapingana na neno la Mungu katika biblia. Ndio maana imeandikwa tusiamini kila roho (kila nafsi) tuzijaribu kwanza. 1Yohana 4:1
“Wapenzi msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.”

Kujua maandiko ni muhimu sana
unataka list ya manabii waliochujwa zamani na kuuawa?
unamkumbuka aliye teswa msalabani?

mkuu unajua maandiko?
 
Ni kwamba tu dini hizi zilianzishwa zamani sana ndiyo maana tunaona sawa. Mimi ni mkristo, lakini leo atokee Seremala aanze kusema ni mwana wa Mungu na katoka mbinguni lazima kila mtu ashtuke na kumuona hayupo sawa kichwani.

Akitokea mtu akisema anashushiwa aya na malaika kutoka kwa Mungu lazima kila mtu amuone ni muongo na tapeli.

Musa kusema amekutana na Mungu mlimani amemtuma kukomboa watu lazima ingekuwa kitu cha kutilia shaka sana. Hasa ukizingatia watu kama yeye huibuka sana jamii inapokuwa kwenye matatizo, kama utumwani.

Dini pekee ambayo iliundwa kwa mtu kufanya tafakari ya kina ni ubudha.

My take. Hakuna haja ya kumshangaa Zumaridi kusema alienda mbinguni. Hakuna haja ya kumshangaa Geordavie kusema alitokewa na Yesu.

Na kama TCRA inataka kubana hao kwa kuita wanamawazo ya kufikirika basi wakataze kurushwa kwa habari zote za dini maana zote ni za kufikirika.

Tcra nao ni wajinga na watumwa wa kifikra,hasa usishangae.
 
Mimi mwenyewe ni nabii (NABII CHIKWENGULA) ila bado sijanunua supika aina ya Fidek pia Hela ya airtime kwenye radio na tv mbali×2
 
Yes angezaliwa zamani hizoo huyu Bishosti angekua hata nabii.

Watu wa zamni walikua wakupeleka tu mara unaamka anasema hiki nawanakuamini bila kutafakari.
Waliwahoji sana tu. Ila mahojiano hayakurekodiwa halafu wafuasi wao waliwashughulikia wahojaji. Watu wengi ilibidi watie tu.
Mkuu kuna nchi mpaka leo ukihoji unashughulikiwa kikatili, shukuru mungu umezaliwa Tanzania Africa ampabo dini zipo zipo kiaina hazina nguvu ya dok
La.
 
Back
Top Bottom