Ukimchunguza kuku sana hutamla..............


Kwasababu tu hatuna uhakika kwamba tutakuwa hai miaka miwili ijayo haina maana tusijenge wala tusiweke akiba. Kwasababu tu hatujui kama kama tutafaulu mitihani ya mwisho haina maana tuache kwenda shule.

Ikitokea hivyo utakua umejifunza kitu, na ni bora ukawa mwangalifu ukose cha kulaumu ukianguka kuliko kuwa mzembe baadae kuwe na " laiti ningejua " nyingi kupitiliza.
 
Muhimu kujua yaliyopita. Kama ndio hivyo hata historia zisingefundishwa mashuleni. Lol.
 

ni kweli kabisa yabidi tujifunze kwa mwenyezi Mungu jinsi anavyotuonea huruma na dhambi zetiu kibao lakini hutusamehe........
 
Muhimu kujua yaliyopita. Kama ndio hivyo hata historia zisingefundishwa mashuleni. Lol.

yajue lakini ujue ya kuwa hayana uhusiano na kesho yako............kesho yako lazima itakuwa tofauti kabisa........
 

hakika ningelifurahi maisha yangelikuwa mepesi hivyo.................lakini ukweli life rermains a puzzle even to wachunguzi wa kuku.....kuku wako mle tu mengineyo Muumba atakuongoza..... kipenda roho .ni kitamu tu hata kama kinarendemka......
 
Si vibaya kujua ya mtu ya nyuma, ila tu uwe na nia ya kuanza mwanzo mpya nae na si ya kumuacha. Binadamu wana sababu nyingi sana za kufanya mabaya au makosa katika maisha yao,so ni vema tu yakazungumzwa kwa kiasi na kukawa na commitment from both side ya kuanza mwanzo mpya pamoja na kusaidiana kuwa bora zaidi kwenye maisha yao pamoja.....!
 
Tunahitaji kujua ya jana na leo ili tuweze kufanya prediction ya yatakayofuta.
 
hakika ningelifurahi maisha yangelikuwa mepesi hivyo.................lakini ukweli life rermains a puzzle even to wachunguzi wa kuku.....kuku wako mle tu mengineyo Muumba atakuongoza..... kipenda roho .ni kitamu tu hata kama kinarendemka......

Well kila mtu anakula kwa kuzingatia anayojua yeye. Anaekula alimradi nae awe amekula ana haki ya kufanya hivyo na tunaokula pale tunaporidhika tu tuna haki ya kuridhisha nafsi zetu kwanza. Kila mtu afanye na kuishi vile aonavyo inamfaa. ..
 
Ni kweli huwezi kumchunguza bata ila ni vyema ukapata brief history. Mwisho wa siku kila mtu ana past yake kwenye mapenzi!!
 
sioni umuhimu wa kuchunguzana kupita kiasi, cha muhimu ni kuchunguza kama mnashabihiana kitabia,
 
lizy umetoa point nzuri,kama uchafu umeshakua sugu utakuchafua na wewe...unamtupilia mbali tena asikusogelee kabisaaa
 

Michele tatizo ni kuwa ukishamjua huwezi kumkubali kama mwanzo na huku ukijua ya kuwa the past is irrelevant why bother?
 
lizy umetoa point nzuri,kama uchafu umeshakua sugu utakuchafua na wewe...unamtupilia mbali tena asikusogelee kabisaaa

tatizo unalolisahau ni kuwa umdhaniaye ndiye kumbe siye........................msafi leo kesho anakuwa ana ukurutu sugu................hata kukufanya umkumbuke yule wa awali..........
 
sioni umuhimu wa kuchunguzana kupita kiasi, cha muhimu ni kuchunguza kama mnashabihiana kitabia,

na hili utalipima kwa mawasiliano yenu ya ana kwa ana.......................badala ya kukusanya majungu ya mtaani kama baadhi wanafikiri ndiyo njia nzuri ya kumla kuku mtamu..............
 
Well kila mtu anakula kwa kuzingatia anayojua yeye. Anaekula alimradi nae awe amekula ana haki ya kufanya hivyo na tunaokula pale tunaporidhika tu tuna haki ya kuridhisha nafsi zetu kwanza. Kila mtu afanye na kuishi vile aonavyo inamfaa. ..

kuna siku utakiri kwenye hili jamvi ya kuwa kumchunguza sana kuku kabla ya kumchinja na kumla ni kupoteza muda...........sanasana utaambulia majungu lakini undani wake ni wakati tu wa miadi ya kumtafuna utafumbuka macho..............
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…