Elections 2010 Ukimwekea Mtego Mama wa Kambo, Mtego Hurudi na Maiti ya Mama Yako!

Elections 2010 Ukimwekea Mtego Mama wa Kambo, Mtego Hurudi na Maiti ya Mama Yako!

Omutwale

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2008
Posts
1,429
Reaction score
1,047
Nimetooa methali hii kutoka lugha ya Kihaya. Wao husema: “Olutega Mu-Kasho lwija na Nyoko”

Na nimeikumbuka methali hii baada ya kutathmini nini kimetokea mpaka Babu, Shangazi, Wajomba na Bibi zangu kijijini wanaielewa vema hali ya ufisadi, siasa za maji taka, uwezo, udhaifu na mapungufu ya wagombea. Na kubwa zaidi wana-mwanga wa kutosha kung’amua nini na kipi ahadi ya kweli na kama mtoaji anaaminika kuweza kuitekeleza. Baada ya kutathmini nimegundua suala la kufunga vyuo ili kukwepesha wanavyuo kushiriki kikamilifu katika kampeni na kuchagua viongozi katika maeneo walijiandikisha badala ya kuwa hasara limeguak mtaji lulu. Hawa wanafunzi walioshindwa kubaki mijini wanastaili pongezi baada ya October 31, 2010. Kiukweli binafsi nawapa heko maana utafiti wangu unaonyesha mchango wao kupanua mawazo huko walikokwenda umefanikiwa. Hapa ndiko Serikali ilimwekea mtego wa kifo mama wa kambo na sasa umerudi na maiti ya Mama aliyemzaa! Tuwashauri sasa wafanyeje!
 
So philosophical...wanasema ukiufunga mlango mmoja mingine mingi inafunguka...imekula kwao!
 
Na tuone mwisho tutaweza kulinda haki zetu?! Kwa hakika "NGOME" wanapaswa kujidhatiti hapo TU! Huku kwingine mabadiliko yamekwishaonekena. Ni jukumu letu soote kuhakikisha tunapiga kura na kulinda tusinyanganywe tonge kooni kwani sasa tayari linaelekea mdomoni na mshindani yuko hoi taabani amegalagala chini.
 
Mkuu Omutwale,

Hii ni sawa na ile Film ya Troy aliyocheza Brad Pitt.

CCM walichokifanya ni Kuchukua Mzinga wa nyuki na nyuki zake na kuupeleka Makao Makuu.

Walichokifanya CCM ni kile TROY walifanya miaka ileee!!!!!! Kweli Historia hujirudia.

Nina imani kubwa sana kuwa Wanafunzi wa Universities wana hasira sana na hii serikali.

Asante kwa maelezo yaliyotulia na mfano wako ni Wa Kitanzania zaidi ya hao TROY.
 
Back
Top Bottom