UKIMWI wa ujasiriamali na biashara!

UKIMWI wa ujasiriamali na biashara!

x - mas

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
931
Reaction score
612
Habari za masiku wana jf wapendwa wangu.Baada ya miangaiko mingi na majaribio ya miradi mbalimbali hatimaye nimebahatisha kamradi, kiasi fulani kana faida kamradi kenyewe ni cha kutoa huduma ya usafirishaji wa mizigo na abiria kwa kutumia guta(pikipiki ya mataili matatu)huku kijijini ni dili kwani usafiri ni washida. Nimekuwa nikiandika kumbukumbu za biashara yangu tangu siku ya kwanza nilipo ianza hyo biashara.Kumbukumbu hzo ni kama gharama za petrol,vipuri,matumizi ya mahtaji yangu muhmu pamoja na faida ninayo ipata kwa siku. Baada ya miaezi kadhaa tangu nianze kabiashara changu nilikaa chni na ku tathmin mradi wangu hivyo ili nipasa nichukue daftari ya kumbukumbu,nikatafuta jumla ya kipato changu kwa miezi hyo kisha nikatoa ghalama za petrol,vipuri matumizi yangu ya lazima ya kilasiku kiasi kilichobaki ndio faida yangu kweli faida ilikuwa kubwa sana lakini......inaendelea,
 
chaajabu pamoja na faida yote kwa wakati huu sina pesa ambayo ingezidi hata robo ya faida niliyo ipata,pesa yote nimetumia katika mambo mbalimbali kila nikijaribu kuweka akiba aifikii lengo kiukweli ili nitatizo kubwa sana kwangu naweza nikasema nisawa na ukimwi ktk ujasiriamali.
Ndugu zangu wanajf kupata pesa nijambo rahisi lakini mtihani kwenye kuzitunza ukizingatia sikuhz unaweza kutoa pesa popote kwa njia ya simu basi imekuwa ni sawa na kuweka moto kwnye nyasi kavu.
Nimegundua inawezekana wengi tunashindwa kufanikiwa kwa sababu tunafanya biashara za patapotea,kama ndugu yangu unambinu ambayo inaweza ikatusaidia watu kama mimi ili tufahamu namna ya kutunza pesa ili tufikie amount iliyolengwa tunaomba msaada wako tafadhali,ubarikiwe sana.
 
Tambua matumizi yako ya kila siku halafu linganisha na hiyo uliyoiita faida kama hakuna kinachobaki basi fikiria uwezekano wa kupanua kipato chabiashara yako kama haiwezekani kupanua buni mradi mwingine wenye kukidhi matumizi yako ya kila siku na kubakiza akiba ya kuweka benki.
 
Tambua matumizi yako ya kila siku halafu linganisha na hiyo uliyoiita faida kama hakuna kinachobaki basi fikiria uwezekano wa kupanua kipato chabiashara yako kama haiwezekani kupanua buni mradi mwingine wenye kukidhi matumizi yako ya kila siku na kub.akiza akiba ya kuweka benki.usiweke hela kwenye simu weka benki ikiwezekana usitumie ATM card. Simu ni kwa ajili ya kutuma na kutumiwa hela si kuhifadhi.
 
Back
Top Bottom