GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
KWANZA
Klabu yangu ‘ pendwa ‘ ya Simba imekuwa Bingwa tena na Kukabidhiwa rasmi Kombe lake ili iweze Kuiwakilisha vyema Tanzania ya Rais wangu Mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli katika Michuano ya Kimataifa ya Klabu Bingwa Afrika ambapo nina uhakika kwa kuwa mwaka huu tumefika hatua ya Robo Fainali basi Msimu ujao ni Kufika Nusu kisha Fainali na hatimaye tunabeba Kombe kabisa.
PILI
Klabu inayotoka Nyumbani kabisa ( Mkoa wangu wa Asili ) wa Mara ( Musoma ) ya Biashara United imebaki Ligi Kuu hivyo bado Msimu ujao wana Mara wote watakula raha na Mkoa utakuwa Kimchezo na Maendeleo yatazidi Kupatikana. Kwa kuendelea Kubaki Ligi Kuu kwa Msimu ujao nina uhakika Vipaji vingi vya Soka vilivyopo Mkoani Mara vitaonekana ili kurudisha enzi za Wachezaji kama akina George Magere Masatu, Bita John, Elias Maguri, Rajab Msoma, Kimune Mwita, Chacha Marwa, Ally Mchumilla na GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE bila kusahau na wengineo wengi sana ambao walicheza Klabu za TP Lindanda ( Pamba FC ) na wengine kwa sasa wanacheza Vilabu mbalimbali kama Mbao FC, Alliance FC, Mwadui FC, KMC FC huku wengi Wao wakiwa katika Timu za Majeshi za Ruvu, Mgambo na wengine wakiwa Timu za Polisi. Kitakwimu Mkoa wa Mara ( Musoma ) unashika Namba Tano ( 5 ) kwa Kutoa Wachezaji wenye Vipaji vya Soka / Kabumbu nchini ukitanguliwa na Mikoa ya Morogoro, Kigoma, Tabora na Mwanza pekee.
TATU
Klabu ya Rafiki yangu Kipenzi na Kocha Bora Kijana kabisa na Nahodha aliyekuwa na Mafanikio Simba SC Mtani wangu wa ‘ Kiha ‘ Suleiman Abdallah Matola ya Lipuli FC imebaki Ligi Kuu na nina uhakika Msimu ujao itafika mbali sana.
NNE
Klabu nisiyoipenda na ninayoichukia mno pamoja na Kocha wake ambaye ‘ hatupendani ‘ kabisa tokea akiwa Mchezaji Mecky Maxime ya Kagera Sugar imeshuka rasmi Daraja. Huyu Kocha ni ' Mnafiki ' mkubwa na ana ' Uyanga Uyanga ' mwingi, wa wazi wazi wala hafichi ambapo Yanga ikicheza na Kagera Sugar huwa anapanga Kikosi ' dhaifu ' makusudi ili Kagera Sugar ifungwe na Yanga lakini akijua anacheza na Simba SC huyu Kocha huwa anatumia muda wake mwingi kuwahimiza Wachezaji wake ' wakaze ' sana huku hadi akiwaahidi ' Zawadi ' nono Wachezaji wake ambazo zingine nyingi huwa anakuwa amepewa na wana Yanga ili tu ' aifunge ' Simba na huku hadi Yeye mwenyewe akishiriki katika ' Kuiroga ' Simba ili Kagera Sugar ishinde.
Kocha Mecky Maxime amevuna alichokipanda na kama wana Simba SC ' tulivyoilaani ' Toto Afrika ambayo nayo ilikuwa na ' Upuuzi ' huu huu wa Kagera Sugar kwa ' Kuikazia ' Simba kupitia kwa Kocha Wao ' Mnafiki ' mwingine Mzee John Tegete ' tumeilaani ' pia na Kagera Sugar na tutahakikisha haipandi tena Ligi Kuu kama ambavyo Simba tunaifanyia ' Fitna ' Kubwa Toto Afrika isipande Ligi Kuu na haitopanda na hazitopanda ng'o hadi wakome / zikome.
Nawasilisha.
Klabu yangu ‘ pendwa ‘ ya Simba imekuwa Bingwa tena na Kukabidhiwa rasmi Kombe lake ili iweze Kuiwakilisha vyema Tanzania ya Rais wangu Mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli katika Michuano ya Kimataifa ya Klabu Bingwa Afrika ambapo nina uhakika kwa kuwa mwaka huu tumefika hatua ya Robo Fainali basi Msimu ujao ni Kufika Nusu kisha Fainali na hatimaye tunabeba Kombe kabisa.
PILI
Klabu inayotoka Nyumbani kabisa ( Mkoa wangu wa Asili ) wa Mara ( Musoma ) ya Biashara United imebaki Ligi Kuu hivyo bado Msimu ujao wana Mara wote watakula raha na Mkoa utakuwa Kimchezo na Maendeleo yatazidi Kupatikana. Kwa kuendelea Kubaki Ligi Kuu kwa Msimu ujao nina uhakika Vipaji vingi vya Soka vilivyopo Mkoani Mara vitaonekana ili kurudisha enzi za Wachezaji kama akina George Magere Masatu, Bita John, Elias Maguri, Rajab Msoma, Kimune Mwita, Chacha Marwa, Ally Mchumilla na GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE bila kusahau na wengineo wengi sana ambao walicheza Klabu za TP Lindanda ( Pamba FC ) na wengine kwa sasa wanacheza Vilabu mbalimbali kama Mbao FC, Alliance FC, Mwadui FC, KMC FC huku wengi Wao wakiwa katika Timu za Majeshi za Ruvu, Mgambo na wengine wakiwa Timu za Polisi. Kitakwimu Mkoa wa Mara ( Musoma ) unashika Namba Tano ( 5 ) kwa Kutoa Wachezaji wenye Vipaji vya Soka / Kabumbu nchini ukitanguliwa na Mikoa ya Morogoro, Kigoma, Tabora na Mwanza pekee.
TATU
Klabu ya Rafiki yangu Kipenzi na Kocha Bora Kijana kabisa na Nahodha aliyekuwa na Mafanikio Simba SC Mtani wangu wa ‘ Kiha ‘ Suleiman Abdallah Matola ya Lipuli FC imebaki Ligi Kuu na nina uhakika Msimu ujao itafika mbali sana.
NNE
Klabu nisiyoipenda na ninayoichukia mno pamoja na Kocha wake ambaye ‘ hatupendani ‘ kabisa tokea akiwa Mchezaji Mecky Maxime ya Kagera Sugar imeshuka rasmi Daraja. Huyu Kocha ni ' Mnafiki ' mkubwa na ana ' Uyanga Uyanga ' mwingi, wa wazi wazi wala hafichi ambapo Yanga ikicheza na Kagera Sugar huwa anapanga Kikosi ' dhaifu ' makusudi ili Kagera Sugar ifungwe na Yanga lakini akijua anacheza na Simba SC huyu Kocha huwa anatumia muda wake mwingi kuwahimiza Wachezaji wake ' wakaze ' sana huku hadi akiwaahidi ' Zawadi ' nono Wachezaji wake ambazo zingine nyingi huwa anakuwa amepewa na wana Yanga ili tu ' aifunge ' Simba na huku hadi Yeye mwenyewe akishiriki katika ' Kuiroga ' Simba ili Kagera Sugar ishinde.
Kocha Mecky Maxime amevuna alichokipanda na kama wana Simba SC ' tulivyoilaani ' Toto Afrika ambayo nayo ilikuwa na ' Upuuzi ' huu huu wa Kagera Sugar kwa ' Kuikazia ' Simba kupitia kwa Kocha Wao ' Mnafiki ' mwingine Mzee John Tegete ' tumeilaani ' pia na Kagera Sugar na tutahakikisha haipandi tena Ligi Kuu kama ambavyo Simba tunaifanyia ' Fitna ' Kubwa Toto Afrika isipande Ligi Kuu na haitopanda na hazitopanda ng'o hadi wakome / zikome.
Nawasilisha.