Ukiongezwa damu je dna? Inaweza badilika

Ukiongezwa damu je dna? Inaweza badilika

Jewel

Senior Member
Joined
May 1, 2008
Posts
180
Reaction score
65
Bonjour !great thinkers hivi naomba kuuliza je ukiugua na umepata upungufu wa damu je? Dna itabadilika ? Au hiyo damu huwa inajitenga ?na kama inajitenga inaenda wapi? Jamani mwenye jibu naomba anipatie
 
Nope haibadiliki
Dna is not about blood its about everything in you

Mimi si mtaalamu wa hii makitu nashindwa namna bora ya kukuelezea
Hakuna kitu inaweza kubadili dna yako
 
Bonjour !great thinkers hivi naomba kuuliza je ukiugua na umepata upungufu wa damu je? Dna itabadilika ? Au hiyo damu huwa inajitenga ?na kama inajitenga inaenda wapi? Jamani mwenye jibu naomba anipatie

Kama alivyokuambia Paulss hapo juu, DNA ya binadamu haibaliki, na ndio maana inatumika katika kutambua miili iliyoharibika kwa mfano kuungua ama kugundulika ikiwa imeoza (forensic), au pia kugundua mhalifu kama ameacha chochote kwenye crime scene ambacho kinaweza tumika kupima DNA (eg damu, nywele, etc).

Unapowekewa Damu, DNA yako haibadiliki kuwa ya damu ile uliyowekewa. Kwa kawaida damu hukaa kwa muda na kuharibiwa na mwili wenyewe na damu mpya ikijitengeneza, hii ni process ya kawaida mwilini na kila siku kuna chembe chembe za damu zinazoharibiwa na nyingine kutengenezwa, na hizi zote zinatengenezwa kwa kufuatana DNA yako..
 
Nakubaliana 100% na wachangiaji Riwa na paulss kuongezewa damu ni kwa ajilil ya kuweza kuboresha usafirishaji wa hewa safi (oygen) kwenda sehemu mbali mbali za mwili. Mtu ambaye anaongezewa damu anapewa chembe chembe nyekundu (red blood cells) ili kumsaidia kwa muda mfupi wakati mwili wake upo kwenye mchakato wa kufidia upungufu uliopo. Kwa maana hiyio hizo chembe zinakuja na DNA yake na hazina uwezo wa kubadilisha DNA ya mpokeaji wa damu.
 
Last edited by a moderator:
kama uongezaji wa damu hautegemei DNA sasa watu si wangeongezewa damu ya ngombe au mbuzi au ngoooo zzinzo mwajika bure kule kwenye machinjio zetu ukiuliza watahalamu wanasema tatizo ni utofauti wa blood group au dNA sasa kama DNA za binadamu ni tofauti mbona wenye ze same blood group wanapeana damu? Wataalam wa DNA mtujibu basi haya si ndiyo mambo mnayosomea?
 
Jee ina maana sample ya damu si vema kuitumia kupata DNA profile ya mtu, na hasa kama amewahi kuongezawa damu?
 
Hii kitu mpaka ifanyiwe utafiti na wengine ndo uambiwe humu.

Ngoja hata mm niku-gugie afu nitakupa majibu.
 
Nakubaliana 100% na wachangiaji Riwa na paulss kuongezewa damu ni kwa ajilil ya kuweza kuboresha usafirishaji wa hewa safi (oygen) kwenda sehemu mbali mbali za mwili. Mtu ambaye anaongezewa damu anapewa chembe chembe nyekundu (red blood cells) ili kumsaidia kwa muda mfupi wakati mwili wake upo kwenye mchakato wa kufidia upungufu uliopo. Kwa maana hiyio hizo chembe zinakuja na DNA yake na hazina uwezo wa kubadilisha DNA ya mpokeaji wa damu.

Sasa DNA kwenye Damu inatofautishwaje iwapo damu ndo itatumika?
 
Mkuu mleta mada umeuliza swali moja zuri sana..

JIBU LA SWALI LAKO NI "HAPANA" au kwa kirefu naweza sema "HAKUNA NAMNA ya DNA(Vinasaba) kubadilika"
Damu huwa imeundwa na vitu vinne;

1. Red blood cells-RBC (Chembe Hai Nyekundu)
2. White blood cells-WBC
(Chembe Hai Nyeupe)
3. Platelets
4. Plasma.

Sasa ni ukweli uliopo ni kuwa WBC
(Chembe Hai Nyeupe) ndio huwa inabeba DNA (Vinasaba) na kawaida lengo kubwa la "Blood transfusion" ni kuongeza Chembe Hai Nyekundu ambazo kiasili huwa hazina Vinasaba.
Wakati pekee ambapo unaweza ukahamisha DNA ya mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine nayo ni rarely sana, ni pale mtu anapoongezewa Bone marrow "
uboho".


Sasa DNA kwenye Damu inatofautishwaje iwapo damu ndo itatumika?


 
Mkuu mleta mada umeuliza swali moja zuri sana..

JIBU LA SWALI LAKO NI "HAPANA" au kwa kirefu naweza sema "HAKUNA NAMNA ya DNA(Vinasaba) kubadilika"
Damu huwa imeundwa na vitu vinne;

1. Red blood cells-RBC (Chembe Hai Nyekundu)
2. White blood cells-WBC
(Chembe Hai Nyeupe)
3. Platelets
4. Plasma.

Sasa ni ukweli uliopo ni kuwa WBC
(Chembe Hai Nyeupe) ndio huwa inabeba DNA (Vinasaba) na kawaida lengo kubwa la "Blood transfusion" ni kuongeza Chembe Hai Nyekundu ambazo kiasili huwa hazina Vinasaba.
Wakati pekee ambapo unaweza ukahamisha DNA ya mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine nayo ni rarely sana, ni pale mtu anapoongezewa Bone marrow "
uboho".





ok umesema kwenye damu kuna vitu vinne na kinachobeba DNA ni WBc.swali je wakati mtu anongezewa damu Hiyo WBC inatolewa kwenye damu? Na kama haitolewi je mtu akisha ongezewea damu sasa si atakuwa na DNA zake pamoja na huyo aliye muongezea damu? Ufafanuzi tafadhari na hata kama zipo kidogo je hazionekani?na kama zinaonekana zinakwenda wapi? Au ina baki mchanganyiko wa DNA au mpaka wazungu waje watujibie au kuna baadhi ya watu walikwisha pewa majibu feki ya dna kutokana na kuwa waliongezewaga damu? Au kwa vile hatuna wataalam kwa hiyo jibu lolote ni sawa.nitarudi baadae.
 
Swala la kupewa damu na kuchanga damu ni pana sana. Maelezo yanayotolewa humu ni oversimplication ili kuweza kuwajulisha wale ambao hii siyo fani yao. Mtu anayepewa damu sehemu ya damu yake na ya mchaniaji zinafanyiwa uchunguzi kama zinakubaliana (compatible). Kimsingi tunatumia mfumo wa ABO na Rh kufanya compatibility tests. Ingawaje kuna magroup mengi sana ya damu ambayo hayana athari katika uchangiaji au kupewa damu. Kwa ajili hiyo damu ya mbuzi au ng'ombe haiwezi kuwa compatible na muongezewa damu anaweza kupata reaction ya hiyo damu.
 
Jambo moja unalopaswa kulifahamu ni kuwa si lazima mtu anapotaka kupimwa DNA huwa sample ya damu pekee ndio huwa inachukuliwa.
Wakati mwingine mate, nywele n.k hutumika kwenye vipimo vya DNA na bado majibu huwa sahihi..
Sasa kama nilivyoeleza hapo juu, lengo la "blood transfusion" ni kumuongezea mtu idadi ya RBC pamoja na kwamba WBC na contents nyingine huingia kwenye mwili wa muhitaji.
Kawaida WBC hukaa ndani ya mwili kwa siku 7 hivi kabla ya kufa na kuzalishwa nyingine na mwili, hivyo hilo alien WBC will eventually die and no longer affect ones DNA.

Halafu, ondoa dhana mgando ya wazungu na mambo kama hiyo...maana nadhani bila wao sidhani kama ungekuwa na fursa ya kuandika haya unayoandika...internet, na ICT(kumbuka JF ni zao la ICT) kwa ujumla imetoka kwao sasa sijui hujafikiria hilo.

ok umesema kwenye damu kuna vitu vinne na kinachobeba DNA ni WBc.swali je wakati mtu anongezewa damu Hiyo WBC inatolewa kwenye damu? Na kama haitolewi je mtu akisha ongezewea damu sasa si atakuwa na DNA zake pamoja na huyo aliye muongezea damu? Ufafanuzi tafadhari na hata kama zipo kidogo je hazionekani?na kama zinaonekana zinakwenda wapi? Au ina baki mchanganyiko wa DNA au mpaka wazungu waje watujibie au kuna baadhi ya watu walikwisha pewa majibu feki ya dna kutokana na kuwa waliongezewaga damu? Au kwa vile hatuna wataalam kwa hiyo jibu lolote ni sawa.nitarudi baadae.
 
Mi nafikiri jibu liwe tu na mtu akimeza denda lako, ambavyo DNA haibadiliki.

Vinginevyo, link tu ndo itatoa majibu.

Hakuna majibu zaidi ya blabla. Watu wanafaulu wakati kila siku wako disko. Wengine bila kujua kusoma na kuandika.
Chezea elimu ya tanzania wewe.
 
Wajameni DNA ni alama(utambulisho) inayopatikana kwenye kila kitu cha mwili wako namaanisha kila kitu kuanzia ukucha hadi nywele, jasho hadi machozi, mate mkojo shahawa mifupa yaani everything
Turudi kwenye mada, damu ni sehemu tu ya mwili wako na inakuwa destroyed baada ya muda fulani tu
Sasa upimaji wa dna upoje?
Ni kwamba itachukuliwa sample kutoka sehemu yoyote ya mwili iwe jasho au mkojo au mate au nyele si lazima damu,
Na sample hii italinganishwa na sample fulani against ili kupata matokeo, so kama mtoto wangu ataongezwa damu ya invisible na punde akachukuliwa dna test haina maana vinasaba vyangu vitapotea(hapa tukumbuke damu ya mtoto itapimwa vinasaba(dna) against vinasaba vyangu kupata matokeo
Mind that kwakuwa mtoto atakuwa kawekewa damu punde basi kama itapima dna against vinasaba vya invisible vitaonekana pia
(but I don't know for how long vinasaba hivi vitadumu)
Kwakuwa tumezoea vinasaba vinapimwa kwa damu tu ndio maana tunapata dhana hii
Tunapaswa kujua kwamba vinasaba havina tokeo moja pia, ntoto akipimwa vinasaba atakuwa navyo vya baba na atakuwa na vya mama pia na vitaendelea kufanana kiukoo kila vitavyopimwa against na vingine

Vinasaba havipimwi kama makundi ya damu kuwa huyu ana a na yule o HAPANA vinasaba vinapimwa kufananisha against kingine kupata mfanano

dhana ya dna ni pana sana kwa mfano ukijamiiana na mwanamke vinasaba vya kwenye shahawa yako ndani y uke vinaweza kuonekana hata baada ya siku kadhaa pia

Mfano kama mimi ni jambazi na sample yangu ya dna ipo basi nikienda Arusha nikapata denu akaumwa nikamuongezea damu kisha nikashtukiwa, ikiwa watamuwahi yule demu na wakamchukua sample kutoka kwenye damu yake na wakaipima against yangu basi nitagundulika kama ni mimi kutoka kwa damu ya yule demu
Lakini hii haimaanishi amebadilika dna hapana

Kuna mablack america wanakuja afrika sikuhizi na kuanza kupima dna kutrace machimbuko yao

Hitimisho dna haina sura moja kama kupima malaria its all about kufananisha
 
Back
Top Bottom