Ukipewa nafasi ya kujua jambo 1 tu kuhusu Maisha yako ambalo bado halijatokea, utatamani kujua nini?

Duh
 
Nahitaji sana kujua kinachoendelea katika maisha yangu na nini hatma yake
 
Nakufa lini ili nijipimie nguvu zangu za kutafuta nisijekuwa nahangaika kutafuta maisha kumbe ntakufa kabla sijashika hata hela.
 
Lini nitakuwa bilionea
 
Maisha yangu nimeweka "auto-pilot mode" yatakavyoenda ni sawa tu.
In fact Mungu ndo muamuzi, atakayotaka kuyafunua kwangu basi atayafunua. Alikuwa na maana ya kutuficha baadhi ya mambo tusijue.

But natamani kujua vyote ambavyo akili yangu itastahimili kuvibeba.😂
 
Jibu ni rahisi Kaa karibu na MUNGU lazima siku zako zikiwadia atakuonyesha live amini hivyo.
 
Sitatamani kujua chochote,

Sitaki kuondoa ule uhondo wa maisha.

Ungekuwa unajua mwisho wa movie ungeiangalia kweli?

Na ndo maana hata wale wanaotafuta dhumuni/kusudi la kuishi naona wanajichosha tu.

Fanya yanayokupa furaha, jipende, basi.
 
Nataka kujua kama nitasalitiwa na huyu mwanamke au laah!
 
Ningetamani niujue mwisho wangu utakuwa ni upi
 
Ntantamani kujua ntafariki lini
 
Ni lini nitatimiza malengo yangu ya kisiasa na uongozi ili kutoa mchango wangu katika ujenzi na ustawi wa taifa letu
 
Wangejua hatma zao Dunia isingekuwa na maendeleo ...Kumbe yule dogo aliyekufa huko Kilimanjaro na Rava4 ,alikuwa ndo katoka kuinunua Halafu ni chalii chini ya miaka 30 .,hawa waliopata ajira juzi kati.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…