Hahaha, kwa wenzangu na mii mayai ya kuchemsha epuka, tena pisha mbali! Kama tumbo lako hauliamini jaribu kula vyakula vikavu na visivyo na mafuta, kama biscuits, crisps zilizochomwa vizuri, karanga za kukaangwa, kunywa na energy drink nzuri upendayo, maji usinywe ya kuzidi...pia ni nzuri kubeba pipi mints mbili tatu. Jamaa yangu alinichekesha alipanda basi na dada mmoja "sister duu", kamsalimia amemwangalia kwanza kama sekunde 10 halafu akamjibu "salama" na kugeukia upande wa pili kama vile ana"mboa" flani hivi. Jamaa akachuna safari ikaanza, dada wa watu akaanza kufakamia vitu njiani, mara nyama ya kuku, chipsi, mayai, apple, malta, maziwa fresh, yoghurt....kila kitu kwake yeye pwani; kona na milima ilipoanza balaa ndiyo lilianzia hapo........!:evil: