Ukisema Jini tayari kuna majini miatatu karibu yako. Kila mtoto mchanga huguswa na jini dakika moja bada ya kuzaliwa. Vitabu vya dini vinasemaje?

duuuuhh
 
Sawa lakini jua hiyo ni laana ya mungu juu yao ndio maana alimpa mwanadamu uwezo wa kutawala vyote vya macho na visivyo na macho,jini wanamiji na himaya zao hadi serikali yao,jini wengine wasio na makazi ni sawa na watoto wa mtaani uwaonao huku wao wakiwa na kazi maalumu ya kujua kila anachokifanya mwanadamu na lengo ni kutaka kumtawala mwanadamu ila hana uwezo na hataweza kwa sababu yeye kaumbwa kwa moto nasi twaumbwa kwa udongo,Che mittoga
 
uzuri ni kwamba hata wasomi nao hawana akili zingine zaidi ya waliosomea,na chochote kilichoandikwa kimeandaliwa na binaadam sasa mtuache tupokee ya wengine halafu tuchuje.sababu quraan na bibilia sio vitabu vya sayansi lakini baadhi ya wanasayansi huviamini.
 
asante", nakufuatilia chief" bdo na subscribe " ili niweze kupata nondo zaidi
 
wadhani katika maumbo yote wayapendayo yapi ni maumbo makubwa zaidi na yenye mamlaka kuu kuliko,haswa dragon,simba na nyoka.katika haya ipi ni falme kuu kabisa.
NYOKA
SIMBA
DRAGON.
 
Hapo ni sawa kabisa, ndio maana kuna mahali pameandikwa, Majini yaliamriwa kumsujudia Adam.
Ibirisi na Majini wakagoma kutii hilo agizo.
Kwakuwa vilikuwa vikimbishia Mungu kwanye mambo mengi vyote vikalaaniwa na Mungu na vikaondolewa Mbinguni na vikatupwa kuzimu, na vinasubiri kuangamizwa siku ya Kiyama.
Kwasasa vimebaki kuhangaika tu na havina makao maalum.
Kao bora la majini ni mwilini mwa binadamu.
Binadamu ukiwa mchafukoge, hupendi kumwomba Mungu, mhalifu, muabudu mizimu, mpenda waganga wa kienyeji wa kupiga ramli na kuroga (waganga wachawi) nk.
Yaani kama unatenda mambo ambayo Mungu ameyakataza, basi unakalibisha kukaliwa na majini ndani yako.
Jini halikai kwa mtu mstaarabu hata siku moja, linamuogopa kwakuwa Mungu ameweka nguvu ya ufalme na utawala ndani yake, na watu wengi hawalifahamu hili jambo kwa usahihi.
Madereva wa maloli makubwa kwenye safari za usiku wakiona vijini njiani wanavigonga tu ndio dawa yake, vinawatokea sana na kuwatisha, wakiogopa tu wanapindua gari, vinawatokea kuwatisha ili wapindue gari vipate damu.
Binadamu ndio kiumbe pekee Bora kabisa kuwahi kutokea na ana nguvu, akili, uwezo busara hekima kuliko viumbe vyote hapa ulimwenguni.
Hiyo pesa ambayo majini wanadai wanaweza kumpa mtu inatengenezwa na binadamu, Jinia hana uwezo wa kutengeneza pesa yoyote.
Ibirisi, Majini, Mizimu, Vindondocha, Vibwengo, Mapepo, Mizungu, Popobawa nk. hizo ni kabila za Majini. Wote hao ni jamii moja.
Wana majina mbalimbali kama Lucifer, Lewiathani, Legioni, nk, wanatabia chafuchafu kama Jinimahaba, Jiniuchawi, Jinikifo, jiniuchafu, jinishetani nk.
Watu wote ambao walipandishwa majini na kuzungumza ukiwauliza hao majini,
Mnamfanyaje mkiti wenu ? hakuna lililosema tumemsaidia jambo fulani jema.
Yote yanasema tunamtesa kwa kumfanya awe masikini, awe kahaba, awe shoga, awe hanithi, awe mgumba, afukuzwe kazi, awe kichaa tunataka kumuua, kumpa ugonjwa nk.
Ukiona mwanao amezidisha kutenda uovu mkubwa na haonyeki, uovu mkubwa kama wa kuwa shoga, au mwizi sugu au mvivu kupindukia, ujue ameshakaliwa na Jini au Majini fulani.
Huyo hata umpige vipi hawezi kubadili hiyo tabia maana hao wadudu Majini ndio wanamwendesha kama gari jipya la kijerumani.
Dawa ni kuwatafuta watumishi wa Mungu waliosimama na kumwombea kijana wako ili Jini limtoke.
Ni njia hiyo tu unaweza kumwondoa Jini ndani ya binadamu.
Jini likisha mtoka mtoto wako mfundishe kuishi kwa maelekezo ya Mungu.
Akichanganya tena na kuzoelea kutenda uovu Majini yanamrudia tena, na safari hii ndio ataharibikiwa kabisa maana yatamkalia mengi na makatili zaidi na kumhalibu zaidi kama kulipa kisasi cha kuyaondoa hapo mwanzo.
Kaa ukilijua hili litakusaidia kwa maisha yako.
 
Majini WOOOOOOTE NI WABAYA, WATUMISHI WA SHETANI. Mungu anatumia MALAIKA. Hawezi tumia JINI. Majini yana kazi ya Kulaghai,kuua,kuharibu,kutesa n.k hakuna jini MWEMA KWA BINADAMU. Anaweza kuwa mwema kwako kwa sababu unamtumikia na ndicho anachotaka ila mkitubuana anakumaliza wewe au wa karibu yako. MAJINI NI WATUMISHI WA SHETANI KAMA MALAIKA WALIVYO WATUMISHI WA MUNGU. na haya majini watu wanafaidika nayo.
 
Majini WOOOOOOTE NI WABAYA, WATUMISHI WA SHETANI. Mungu anatumia MALAIKA. Hawezi tumia JINI. Majini yana kazi ya Kulaghai,kuua,kuharibu,kutesa n.k hakuna jini MWEMA KWA BINADAMU. Anaweza kuwa mwema kwako kwa sababu unamtumikia na ndicho anachotaka ila mkitubuana anakumaliza wewe au wa karibu yako. MAJINI NI WATUMISHI WA SHETANI KAMA MALAIKA WALIVYO WATUMISHI WA MUNGU. na haya majini watu wanafaidika nayo.
 
Elimu hii umeipata katika kitabu gani ?
Ninavyojua mimi, hakuna Jini zuri au jema hata moja, yote ni maovu na hayamsadii binadamu zaidi ya kumharibu.
Umejuaje kama hakuna jini mwema ?
 
Mkuu Kudo naweza pewa ushahidi mwingine kua Mungu alianza kuumba majini kabla ya binaadamu?
Usitumie Quran
Atumie nini embu msaidie pia katika hilo,yaani atumie akili,sayansi,Biblia au kitu gani ?
 
Sawa ahsante kwa elimu yako pia
 
Sawa Sawa na ahsante kwa nondo hii hakika tunaendelea kujifunza sote
 
Sio kweli mzee.
 
Unasema binadamu ni bora kuliko malaika au majini ?
 
SERIKALI YA MAJINI
Majini wana Utawala wao ambao ni Majini Wakuu na Majini wa Kawaida wanaopewa Kazi za kufanya na Wakuu wao, Katika Serikali yao kuna Wakuu wa Serikali, Wakuu wa Majeshi, Wakuu wa Mahakama na wengineo wengi.

Utawala katika Serikali yao umegawanyika katika sehemu Kuu mbili (2);
1. Utawala katika Ulimwengu wa Kijini.
2. Utawala katika Ulimwengu huu wetu wa Kibinadamu.


Majini Wakuu kabisa wapo Watatu (3) ambao Majina yao ni;
1.
2. Lucifer.................ambae ndio Mfalme wao (Emperor),
3. Beelzebuth.......... ambae ni Mtoto wa Mfalme (Prince),
4. Astaroth ..............ambae ni Mtawala Mkuu wa Majimbo (Grand Duke).


Hawa Watawala Wakuu kabisa watatu, iwapo Binadamu anataka kuwaita na kuwatumia inambidi atumie njia Maalum;

Mtu anayewaita anatakiwa achore alama zao kwa kutumia Damu yake mwenyewe, au anaweza pia kutumia Damu ya Kobe wa Baharini (Kasa) katika kuandikia.
Iwapo atashindwa haya yote basi anaweza pia kuwaita kwa kuchora alama za Majini hao kwenye Kito cha Ruby au

Emarald; kwani vito hivi vinaendana sana na Majini hasa wale wa Ukoo wa Jua, ambao huwa na Busara, wazuri na Marafiki zaidi kuliko aina nyingine ya Majini.

Alama hizi za Majini zinatakiwa zivaliwe na Mtu ambae anataka kuwaita. Ikiwa muitaji ni Mwanamme, anatakiwa aiweke kwenye Mfuko wake wa Kulia na iwapo ni Mwanamke, anatakiwa aiweke katikati ya Matiti yake ikielekea upande wa Kushoto.

Alama hizi zinatakiwa ziandikwe katika siku ya Jumanne saa Kumi na mbili (12) mpaka saa moja asubuhi au saa saba mchana mpaka saa nane kwa majini wote.

Majini hawa watatu wana uwezo wa kufanya mambo yote, na kwa Mtu ambae anawaita hawa anatakiwa aheshimu wale tu ambao watamheshimu kwani Majini hawa Wakuu wanawaheshimu wale tu ambao ni Marafiki wao Wakuu na wa karibu, hivyo mtu anaeamua kuwaita anatakiwa ajihadhari kwa lolote ambalo linaweza kutokea.

Utawala wa hawa umegawanyika baina yao wote kwani kila mmoja ana Wasaidizi wake wakuu Wawili ambao nao huwa wanawatuma Majini wengine kuhusu mambo ambayo Mfalme wao Lucifa ameagiza yafanyike Duniani kote.

Wasaidizi walio chini ya Lucifa ni;
Put Satanachia na
Agaliarept;.............Ambao wanaishi Bara la ULAYA na ASIA.
Wasaidizi walio chini ya Beelzebuth ni;
Tarchimache na
Fleurety...................Amb ao wanaishi Bara la AFRIKA.
Wasaidizi walio chini ya Astaroth ni;
Sargatanas na
Nebiros.............Ambao wanaishi Bara la AMERIKA.
{mospagebreak}

Majini katika Serikali yao kulingana na Kazi zao ni kama ifuatavyo;
1.
2. LUCIFUGE ROFOCALE....ambae ni Waziri Mkuu (Prime Minister)
3. SATANACHIA.........ambae ni Amiri Jeshi Mkuu (Commander-in-Chief)
4. AGALIAREPT......ambae ni Kamanda wa Majeshi
5. FLEURETY.........ambae ni Luteni Jenerali (Lieutenant-General).
6. SARGATANAS.....ambae ni Brigedia Meja (Brigadier-Major)
7. NEBIROS....ambae ni Jemedari Mkuu na ni Inspekta Jenerali (Field-Marshal and Inspector-General).


Kama jinsi ilivyoonekana hapa ya kuwa Utawala wao katika Ulimwengu wao wa Kijini umekaa KIJESHI lakini Utawala wao hapa Duniani sio wa Kijeshi kwani;

1. LUCIFUGE ROFOCALE; ana Mamlaka ambayo amepewa na LUCIFA ya kudhibiti Mali na Hazina zote za hapa Duniani.
Wasaidizi wake ni Baal, Agares na Marbas.

2. SATANACHIA ana Mamlaka juu ya Wake, Wanawake, na Wasichana wote ambapo ana uwezo wa kuwafanyia kama jinsi atakavyopenda yeye.
Wasaidizi wake ni Pruslas, Aamon na Barbatos.

3. AGALIAREPT
Ana Mamlaka na Uwezo wa kugundua Siri zote zilizopo katika Mabaraza na Mahakama zote hapa Duniani.
Anavumbua Siri za hali ya juu sana.
Anaamuru Kikosi cha Pili cha Majini wasiopungua 3,000).
Wasaidizi wake ni Buer, Gusoyn, na Botis.

4. FLEURETY
Ana Mamlaka na Nguvu za Kufanya Kazi yeyote Usiku na anasababisha mvua ya Mawe katika sehemu yeyote ile itakayoitajika.
Anaongoza na Kudhibiti Jeshi kubwa la Majini.
Wasaidizi wake ni Bathsin (au Bathim), Pursan, na Eligor.

5. SARGATANAS ana Nguvu na Mamlaka ya;
Kumfanya Mtu yeyote asionekane.
Anasafirisha Mtu yeyote kwenda sehemu yeyote ile.
Kufungua Loki na Kufuli zote Duniani,
Kuonyesha na kuweka wazi mambo yote yanayofanyika ndani ya Nyumba za Watu binafsi.
Anafundisha mbinu zote za Uchungaji wa Wanyama.
Anadhibiti na Kuamuru Vikosi Kadhaa vya Majini wasiopungua 5,000 kwa kila kikosi.
Wasaidizi wake ni Zoray, Valefar na Faraii.
{mospagebreak}

6. NEBIROS ana uwezo wa;

Kushurutisha Uovu kwa Mtu yeyote amtakaye.
Ana uwezo wa Kumletea Mtu Fahari Kuu.

Ana uwezo wa Kumuonyesha Mtu vitu Bora kama vile; Madini, Mawe, Mboga, na Wanyama.
Ana uwezo Mkubwa wa Kutabiri vitu vitakavyotokea hapo baadae; kwani Huyu ndiye Mkuu wa Utabiri katika Ulimwengu wa Kijini.

Anazunguka zunguka huko na huko kila sehemu kwa ajili ya Kuangalia, kuchunguza na Kukagua aina zote za Maangamizi.
Wasaidizi wake ni Ayperos, Naberrs na Glassyalabolas.

Kuna Mamilioni ya Majini wengine ambao nao wapo chini ya hao waliotajwa hapo juu na hutumika tu pale inapoonekana ya kuwa kuna Kazi ya kufanya kutoka kwa Wakuu wao, kwani wao hutumiwa na Wakuu wao kama Wafanyakazi au Watumwa.

Hata hivyo kuna Majini Wasaidizi Muhimu Kumi na Saba (17) ambao wao hufanya Kazi kama Mawaziri wa Wale Majini Wakuu Sita (6), Majini hao pamoja na Kazi zao ni kama ifuatavyo;

1. CLAUNECK;

Ana Nguvu na Mamlaka juu ya Vitu na Utajiri,
Anaweza Kuvumbua Hazina iliyofichwa, kwa yeyote atakayeweka Mkataba nae,
Ana uwezo wa Kumzawadia Mtu Utajiri mkubwa kwani yeye anapendwa sana na Lucifer,
Ana uwezo wa kukuletea Pesa kutoka mbali;
Mtii naye atakutii!

2. MUSISIN;
Ana Nguvu juu ya Mabwana Wakuu, anawapa Maelekezo kuhusu yale yanayotokea na kupitishwa katika Serikali zao na za Washirika wao.

3. BECHARD;
Ana Nguvu na Mamlaka juu ya Upepo, Dhoruba (Tufani), Radi, Umeme, Mvua na Mvua ya Mawe, kwa kutumia uchawi wa Chura na Vitu vingine vya namna hii.

4. FRIMOST
Ana uwezo juu ya Wake na Wanawali na ana uwezo wa kukusaidia kuwafurahia.
5. KHIL ....Husababisha Mtetemeko wa Ardhi.

6. MERSILDE: Ana uwezo wa kukusafirisha mara moja sehemu yeyote uitakayo.

7. CLISTHERET: Ana uwezo wa kukugeuzia usiku na mchana kwa kupenda kwako.
{mospagebreak}

8. SIRCHADE: Ana uwezo wa kukuonyesha wewe aina zote zile za wanyama katika umbo lolote lile walilonalo.

9. SEGAL: Ana uwezo wa kukuonyesha dhahiri miujiza yeyote iwe ya kawaida au ya kimazingaombwe.

10. HIEPATCH: Ana uwezo wa kukuletea mtu aliye mbali papo hapo.

11. HUMOTS: Ana uwezo wa kusafirisha aina zote za vitabu kwa starehe yake.

12. FRUCIESSEIERE: Ana uwezo wa kuwafufua wafu.

13. GULAND: Ana uwezo wa kusababisha aina yote ya maradhi.

14. SURGAT: Ana uwezo wa kufungua aina zote za Loki.

15. MORAIL: Ana uwezo wa kufanya vitu vyote Duniani visionekane.

16. FRUTIMIERE: Ana uwezo wa kukupa kila aina ya sherehe.

17. HUICTIIGARA: Ana uwezo wa kusababisha kutembea usingizini na kwa wengine kuwakosesha usingizi kabisa.

Satanachia na Satanisie wanawatawala majini 45 au 50 wanne katika hao ni Surgutthy, Heramael, Trimasel na

Sustugriel. Wawili wa hawa ni machifu na waliosalia hawana umuhimu wowote.

Hawa ni Majini watumikao kwa binadamu kwa urahisi na haraka lau ikiwa wanaelewana na anaemuita,

Serguthy ana uwezo juu ya wake za watu na wanawali

Heramael anafundisha elimu ya madawa na anatoa na ujuzi kamili wa magonjwa yote, tiba zake sahihi, anafundisha

aina ya mimea yote, sehemu mimea hiyo inapatikana, nyakati nzuri ya kuipata, umuhimu wa mimea hiyo na namna ya kuchanganya mimea hiyo ili kupata dawa sahihi kwa maradhi ya aina yeyote ile.

Trimasel na Sustugriel hawa wawili ni Machifu na wanatoa elimu ya kichawi kwa wale wanaowapenda.

Agalierept na Tarihimal wanamtawala Elelogap, ambae nguvu zake zipo juu ya Maji.

Nebirots Wawili wawatawala Hael na Sergulath.

Hael anatoa maelezo juu ya Usanii wa kuandika kila aina ya Barua, anampa Mtu uwezo wa kuongea mara moja kila

aina ya Lugha na anaelezea na kufumbua vitu vyote vya siri.
Sergulath ana uwezo wa Kufundisha Mtu njia mbalimbali za kuvunja pande ambazo hazielewani.

Hawa wana Wasaidizi wao Wanane (8) wenye nguvu

1. Proculo ambae ana uwezo wa kumpatia Mtu usingizi kwa muda wa masaa manane huku akiwa anafahamu yanayotokea usingizini.

2. Haristum ambae anampa Mtu uwezo wa Kupita kwenye Moto bila ya kuungua.

3. Brulefer, ambae ana uwezo wa Kumfanya Mtu apendwe na Wanawake.

4. Pentagnony, ambae anawapa Watu uwezo wa Kutokuonekana (Invisible), pia anapendwa sana na Watawala Wakuu

5. Aglasis, ana uwezo wa Kumsafirisha Mtu kwenda sehemu yeyote ile Duniani.

6. Sidragrosam, anawafanya Wanawake wacheze Uchi.

7. Minoson, ana uwezo wa Kumhakikishia Mtu kushinda katika Michezo yeyote ukiwepo wa Kamari.

8. Bucon ambae ana Uwezo wa kuanzisha Chuki na Wivu kati ya Jinsia mbili (Wanaume na Wanawake).



Naishia hapa ila nipatapo muda nitajaribu kuleta mada nyingine kuhusu uwepo wao juu ya ulimwengu kabla ya mwanadamu na kwanini mungu aliwaumba,himaya zao na chimbuko lao la usaliti juu yao wenyewe na muumba

zitto junior

Asalaam kudo
 
Hayo Maasi ambayo hutafanya upande wa Mashariki ni Maasi gani...!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…