Ukishaanza biashara achana na kutunza pesa VICCOBA na uweke nguvu zaidi kwenye kukuza biashara

Ukishaanza biashara achana na kutunza pesa VICCOBA na uweke nguvu zaidi kwenye kukuza biashara

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Mimi sipingi uwepo wa VICCOBA kwasababu kwa mtu ambaye hana mtaji anaweza kujiunga na kusevu kidogo kidogo na baada ya mwaka akapata mtaji wakati wa kuvunja kiccoba. Ni njia nzuri ya kufikia malengo yako. Ila leo nitashauri watu ambao wanateseka na maisha kisa VICCOBA.

Mtu ukishaanzisha Biashara unapaswa uwekeze nguvu, pesa na akil yako yote kwenye kuikuza. Ile faida kidogo utakayoanza kuipata unatakiwa uirudishe kwenye biashara kuongezea mtaji. Biashara hadi uanze kuifaidi ina hatua nyingi ila kwa pale mwanzoni pambana sana mtaji ukue.

Itachukua muda ila ndo uhalisia. Ninapinga sana mtu ana biashara ndogo lakini hela hiyohiyo badala ya kuizungusha ikue utakuta ndo kila wiki au mwezi anaenda kupeleka kiasi kuhifadhi kwenye VICCOBA. Huo ni UPUMBAVU.

Unatunza hela ili nini wakati biashara bado changa? Wafanyabiashara wote makini hutumia benki kukopa na kulipa & kulipwa. Hakuna mfanyabiashara makini ataanza kuweka hela benki zikae tu akisubiri labda riba ya 10% kwa mwaka wakati akiweka juhudi anaweza zalisha hata 300% ya hiyo hela kwa muda huo.

Nimeandika huu uzi baada ya siku za karibuni kusumbuliwa na kina dada wengi kuhusu kuwasaidia pesa za VICCOBA. Mimi ni mtenda dhambi mstaafu kwahiyo hata kamà hawa kina dada wako tayari wanipe tamu siwezi kubaliana nao. Wafuate huu ushauri wangu. Wengi wao huishia kukopa kwingine na kujikuta kwenye mabalaa zaidi.
 
20240725_080029.jpg
 
Pole kwa kukutana na mizinga kutoka kikosi cha mizinga aka single mamaz ila ni bora wakikufuata uwashauri hapo hapo huku hawapo
 
VICOBA au VSLAs idea yake ilianzia kule West Africa nchini Niger na hivi vikundi ni special kwa watu walio tengwa na huduma rasimi za kifesha hasa Vijijini.

Kwa mjiji vicoba havitakiwi na pia ni specila kwa ajili ya watu wanao ishi Commubal model of Productions yaani wanajuana kwa tabia, na pia wanaishi kwa upendo.

Kwa mijini VICOBA haifai kuwepo ni kuforce na kutafuta matatizo
 
Umenena vyema sana mkuu. Wenzetu wanaliwa tunda kimasihara sababu ya marejesho ya VICCOBA kila wiki.
Idea ya VICOBA ni kwa jamii ya vijijini ilio tengwa na huduma za kifedha na ambao wana shughuri ndogo sana za biasbara kiasi kwamba hata mikopo yao ni midogo midogo sana.

Idea ya mwanzo ilikuwa sahihi sema sasa imeingiliwa sana na kinacho tokea ni kwa sababu ya kukiuka ile misingi yake.
 
Back
Top Bottom