Ukisikia uonevu Serikali hufanya, ni huu hapa kwa Wakulima. Haiwezekani!

Ukisikia uonevu Serikali hufanya, ni huu hapa kwa Wakulima. Haiwezekani!

Paulsylvester

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2021
Posts
1,464
Reaction score
3,379
Serikali inamipango mibovu sana juu ya wakulima wa nchi hii

Ni uonevu juu ya uonevu!! Haya mambo ifike mahali tuone aibu kwa kuwanyonya kiasi hiki wakulima

Wakulima wa nchi hii, ni wao tu ndio wanaojua mateso wanayoyapitia, kwenye jua Kali na mvua za radi na Mawe, wao na shamba,

Kwenye mvua kubwa na haba, wao na shamba, wamebeba msalaba mzito huku wakiwa na matumaini ya kuendeleza familia zao, lakini wanakwamishwa na mipango mibovu ya serikali yao masikini ya Mungu!!

Kila mtu ukimuuliza, atatoa takwimu kusema, nchi yetu hutegemea kilimo kwa zaidi ya 70℅ na wananchi wengi ndio hutegemea kilimo kwa ajili ya kujikimu maisha yao, kusomesha na kuendeleza familia zao

Sera ya nchi yetu inasema, Nchi yetu ni ya wakulima na wafanya kazi!!

Serikali ituambie, kwa nini bunge letu halima MTU wa kuwasemea wakulima? Badala yake wanawekewa mawaziri ambao hata shamba hawana, hawajui kulima na hawaujui uchungu wa wakulima wanaoupitia...?

Serikali na waajiriwa wake, kila mwaka wafanya kazi wa serikali hulia kuongezewa mishahara, posho na fedha sijui za kujikimu kwenda safari za kuwatazama wanavyolima n.k

Lakini ukirudi kwa wakulima, hayupo hata mmoja anayefikiria kuweka mfumo wa angalau wa kuwapatia ruzuku wakulima hawa, Hiii wagosha

Wakitaka kuuza mazao yao wenyewe waliyoyalima wao wenyewe kwa jasho lao na kwa damu, utasikia mtu anasema, niskie mtu akipandisha bei ya vyakula! sijui niskikie mtu akifungua mipaka ya kuuza mazao nje!!! mbona tunavunana kiasi hiki?? Yaani hatuoni kwamba kuna mtu anakula jasho la mtu bila lidhaa yake?

Huu ni uonevu wa hali ya juu kwa serikali, na haiwezekani,

Inakuwaje kwenu nyinyi wafanya kazi mjiongezee mishahara na maposho yasiyo na maelezo, na muone ni halali kwenu, ila kwa wakulima kuuza kwa bei wanayoitaka iwe ni haramu.....?

Ni kwa sababu mawaziri wote wanaopewa wizara hiyo, si wakulima ndiyo maana! hawajui hata jembe linashikwaje, hawajui madhila yoote wayapatayo wakulima..?

Mambo wanayofanyiwa wakulima ni kwa sababu hawana wa kuwasemea bungeni??

Leo hii wanalia mbolea hakuna, na kama zipo, bei zake zimewashinda, lakini wanalima hivyohivyo, wakija kupata tumazao twao, mnawazuia wasiuze kwa bei waitakayo,

Je, wakulima wa nchi hii wataendelea lini?? Ni lini wataondokana na umasikini..?

Wapelekeni basi angalau mabwawa tuu ili wawe wanalima Mara kwa Mara muone kama wengi wenu hamtahamia kwenye kilimo, napo hamtaki!!! Hii wagoshaa ujue inauma eeeh!!

Mijini ndiko kwenye viwanda, na vitu Bei ya chini kwa vitu vitokanavyo na malighafi zilezile za mkulima, na ndiko huko ambako wakulima hawakai, malighafi zilezile zikirudi kwa mkulima, mama yangu, anauziwa kwa kukomolewa ili tu aendelee kuwa masikini!!

Hivi serikali mnajua kwamba, umasikini wa wakulima wa nchi hii mmewasababishia nyinyi??

Ingelikuwa ni heri sasa, Serikali ichukue hatua kuliona hili na kulifanyia kazi haraka Kabla ya wakulima hawajaamka na kusababisha sntofahamu!!

Tusitengenezee umasikini, unafanya kazi serikalini, fanya na ule kwa urefu wa kamba yako, kwa nini mkulima hamtaki ale kwa urefu wa kama yake na badala yake mnamfanya awe adui mazao yake yanapokuwa tayari kwa kuuzwa?


Mungu Ibariki Tanzania
 
Taarifa kama hii wakiiona wakulima wa Kagera waliopigwa stop na serikali wasiuze kahawa kwa mtu yeyote hadi siku ya mnada ndo unawaongezea msongo wa mawazo.
Maana yake kuna mapapa yapo na calculator yanapanga genge kwamba yakomee bei gani.
Bado hatujagusa unyonyaji kwenye pamba, korosho, tumbaku n.k muda si mrefu wataingilia biashara ya parachichi.
 
Ukiona nchi karibia 70% ya wananchi wake wanategemea kilimo..meanwhile kilimo kinachangiaa chini ya 20% ya uchumi wa nchi...tambua kabisa hiyo nchi nia masikini wakutupwa.

Nahili ccm ndio furaha yao..kuendelea kumdidimiza mkulima..haiwezekani miaka zaidi ya 60 ya uhuru mkulima bado anatumia jembe la mkono na ndio mtu masikini wa kutupa.

Sijawahi waelewa viongozi wa hii nchi..they are not serious kabisa na kumkomboa mwanachi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kama mnataka mali, mtazipata shambani.
 
Taarifa kama hii wakiiona wakulima wa Kagera waliopigwa stop na serikali wasiuze kahawa kwa mtu yeyote hadi siku ya mnada ndo unawaongezea msongo wa mawazo.
Maana yake kuna mapapa yapo na calculator yanapanga genge kwamba yakomee bei gani.
Bado hatujagusa unyonyaji kwenye pamba, korosho, tumbaku n.k muda si mrefu wataingilia biashara ya parachichi.
Sasa nakubali, mabadiriko hayaepukiki tena, katiba inahitajika kwa njia zote!

Wakulima ni mhimu wapate msemaji wao anayotokana na wakulima wenyewe!
 
Serikali inamipango mibovu sana juu ya wakulima wa nchi hii

In uonevu juu ya uonevu!! Haya mambo ifike mahali tuone aibu kwa kuwanyonya kiasi hiki wakulima

Wakulima wa nchi hii, ni wao tu ndio wanayojua mateso wanayoyapitia, kwenye jua Kali na mvua za radi na Mawe, wao na shamba,

Kwenye mvua kubwa na haba, wao na shamba, wamebeba msalaba mzito na matumaini ya kuendeleza familia zao, lakini wanakwamishwa na mipango mibovu ya serikali yao

Kila mtu ukimuuliza, atatoa takwimu kusema, nchi yetu hutegemea kilimo kwa zaidi ya 70℅ na wananchi wengi ndio hutegemea kilimo kwa ajili ya kujikimu maisha yao, kusomesha na kuendeleza familia zao

Sera ya nchi yetu inasema, Nchi yetu ni ya wakulima na wafanya kazi!!

Serikali ituambie, kwa nini bunge letu halima MTU wa kuwasemea wakulima? Badala yake wanawekewa mawaziri ambao hata shamba hawana, hawajui kulima na hawaujui uchungu wa wakulima wanaoupitia...?

Serikali na wanaoajiriwa na serikali, kila mwaka wafanya kazi hulia kuongezewa mishahara, posho na fedha sijui za kujikimu kwenye safari za kuwatembelea wakulima n.k

Lakini ukirudi kwa wakulima, hayupo hata mmoja anayefikiria kuweka mfumo angalau wa kutoa ruzuku kwa wakulima wa nchi hii!!

Wakitaka kuuza mazao yao wenyewe waliyoyalima wao wenyewe kwa jasho lao na kwa damu, utasikia, niskie mtu akipandisha mazao, sijui niskikie mtu akifungua mipaka ya kuuza mazao nje!!!

Huu ni uonevu wa hali ya juu kwa serikali, na haiwezekani, inakuwaje kwenu nyinyi wafanya kazi mjiongezee mishahara na muone ni halali kwenu, ila kwa wakulima kuuza kwa bei wanayoitaka uwe ni haramu.....? Ni kwa sababu mawaziri wote wanaopewa wizara hiyo, siyo wakulima, hawajui hata jembe linashikwaje, hawajui madhila yoote yanayompata mkulima, Mambo wanayofanyiwa wakulima ni kwa sababu hawana wa kuwasemea bungeni??

Leo hii wanalia mbolea hakuna na kama zipo, bei zake zimewashinda, lakini wanalima hivyohivyo, wakija kupata tumazao yao, mnawazuia wasiuze kwa bei waitakayo,

Je, wakulima wa nchi hii wataendelea lini??

Mijini ndiko kwenye viwanda, na vitu Bei ya chini ni hukohuko ambako wakulima hawakai, zikifika kwa wakulima, ndio kabisaaa mnawanyonga na kuwadidimiza kwa bei za ajabu ajabu, Serikali, mnawatakia nini wakulima wa nchi hii!!..?

Ingelikuwa ni heri sasa, Serikali ichukue hatua kuliona hili na kulifanyia kazi haraka Kabla ya wakulima kuamka na kusababisha sntofahamu


Mungu Ibariki Tanzania
Kuna mdau kajadili humu kuwa umaskini nchini unalindwa Kikatiba..
Kwa kuwa bado hatutaki Katiba Mpya, hakuna namna, wacha umaskini utamalaki tu hadi akili zikae sawa!
 
Back
Top Bottom