Ukitupwa kama jiwe wapo watao kuokota kama dhahabu

Mwanasayansi Kalivubha

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2024
Posts
344
Reaction score
926
Ukichukua watu kumi uwapeleke msituni kisha utafute mti mmoja mkubwa na uwaambie wanaona nini?

# Wapo watasema wanaona mti

#Wapo wataosema wanaona kuni.

#Wapo wataosema wameona Mbao.

#Wapo wataosema wameona mlingoti wa umeme

# Wapo wataosema wameona nguzo ya nyumba.

WOTE WAPO SAHIHI, NA HIVYO NDIVYO ILIVYO KWENYE MAISHA YA KAWAIDA.

Wapo wataokuona kama ulivyo na kuna ambao wataenda zaidi ya ulivyo ndio maana unayemkataa leo kwa matusi na dharau anaweza kubaliwa pengine tena akaonekana MTU MUHIMU SANA.

Utavyoonekana machoni pao itategemea tafasiri zao jumlisha ufahamu wao.

#Mwanasayansi Saul kalivubha
Fikia Ndoto Zako.
 
Naunga mkonoo hojaa za uzii huu. [emoji106][emoji106]
 
Ujajuaaa dhahabu lazima iungueee ikae sawa
 
Kweli kabisa yaani kama Wema kwa Diamond, halafu Zari kwa Diamond
 
Kama past yako ni chafu kubali tu ulikosea, badilika na uende kuishi sehemu ambayo haujulikani.

Kama hauna thamani, pambana kupandisha thamani yako, thamani yako inavyopanda na watu watakuthamini.

Tusijidanganye ili tu kukubaliana na comfortable zone yetu
 
Kwenye hili eneo huwa hukoseagi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…