Zee la kitaa
JF-Expert Member
- Oct 25, 2017
- 403
- 211
Nimekuwa nikifuatiliia watia nia wengi walioanza kujitokeza na kufanya tathmini kidogo nimegundua wengi hawana mipango madhubuti ya kuwakomboa wananchi katika changamoto nyingi wanazokumbana nazo.
Wengine wanaona kama urais, ubunge na udiwani kama njia nyepesi ya kujipatia vipato. Wananchi wengi wamepata uelewa kuhusu nini wanataka na kiongozi wa aina gani wanamtaka.
Wananchi wanataka kiongozi atakayejibidiisha katika kutatua changamoto zinazowakabili regardless chama anachotoka. Kiongozi mwenye maono kwa taifa na jamii inayomzunguka.
Kiongozi asiyekuwa na makandokando ya kibepari na kiongozi anayetambua Tanzania ndio taifa lake na yuko tayari kupoteza uhai wake kwa ajili ya taifa lake.
Hivyo kwa kuangalia hayo utatambua wengi wanaotia nia wanashida na kukosa vigezo vya msingi. Vigezo vingine unaweza kuongeza wewe.
Naomba kuwasilisha
Wengine wanaona kama urais, ubunge na udiwani kama njia nyepesi ya kujipatia vipato. Wananchi wengi wamepata uelewa kuhusu nini wanataka na kiongozi wa aina gani wanamtaka.
Wananchi wanataka kiongozi atakayejibidiisha katika kutatua changamoto zinazowakabili regardless chama anachotoka. Kiongozi mwenye maono kwa taifa na jamii inayomzunguka.
Kiongozi asiyekuwa na makandokando ya kibepari na kiongozi anayetambua Tanzania ndio taifa lake na yuko tayari kupoteza uhai wake kwa ajili ya taifa lake.
Hivyo kwa kuangalia hayo utatambua wengi wanaotia nia wanashida na kukosa vigezo vya msingi. Vigezo vingine unaweza kuongeza wewe.
Naomba kuwasilisha