Ukombozi kwa wanaofuga kuku kwa kutumia taa za joto

Transistor

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2013
Posts
1,061
Reaction score
1,637
Katika mtiririko wangu wa kudesign vifaa mbalimbali vya electronics,leo nawaletea kifaa ambacho ni mkombozi kwa wanao fuga kuku kwa kutumia taa za filament.

Teknolojia hii ni maalumu kwa ajili ya wale wanao tumia taa za filament(filament bulb) almaarufu zinajulikana kama vitunguu,kwa ajili ya kufugia kuku wa mayai.

Lengo la teknolojia hii ni kupunguza matumizi makubwa ya umeme yanayo tokana na matumizi ya taa aina hii kwa wafugaji wa kuku.

Teknolojia hii haivunji sheria yoyote ya TANESCO kwani haiingilii mfumo wowote wa utendaji kazi wa meter ya umeme.

Kifaa hiki kinaweza kusaidia kupunguza gharama za umeme kwa kiwango kikubwa.
Tuanze kwa kujua bei ya umeme.

GHARAMA RASMI ZA UMEME KWA MUJIBU WA TANESCO KWA UNIT MOJA

Kwenye mstari mwekundu nyumba nyingi zenye shughuli za kibiashara zinazo tumia umeme huangukia hapo kwa mtazamo wangu gharama ya UNIT 1 itakuwa ni Tsh 273.


MATUMIZI YA UMEME YA TAA MOJA YA WATT 100 BILA KUFUNGA ENERGY SAVER

Data
-Taa moja ya watt 100
-Masaa ya kufanya kazi = 24hrs
-Bulb ya watt 100 ikiwaka kwa masaa 24 itatumia kwh 2.4(kwa siku moja) sawa na 72kwh(kwa mwezi) sawa na 876kwh (kwa mwaka)

Gharama za matumizi hayo itakuwa.
Kwa siku =kwh2.4 x Tsh273 = Tsh 655.2/=

Kwa mwezi =kwh72 x Tsh273 = Tsh 19656/=

Kwa mwaka = kwh876 x Tsh273 = Tsh239,148/=

NB;Gharama hizi ni kwa taa moja ya watt 100 inayo waka masaa 24,hivyo unaweza kuzidishia

gharama hizi na idadi ya taa ulizonazo katika banda lako kujua kiasi sahihi unacho lipa kwa
siku,mwezi au mwaka.
MATUMIZI YA UMEME YA TAA MOJA YA WATT 100 BAADA YA KUFUNGA KIFAA CHA ENERGY SAVER

Baada ya kufunga kifaa cha energy saver taa ya watt 100 itatumia Kwh 1.92 kwa masaa 24


Gharama za matumizi hayo itakuwa.

Kwa siku =kwh1.92 x Tsh273 = Tsh 524.16/=

Kwa mwezi =kwh57.6 x Tsh273 = Tsh 15724.8/=

Kwa mwaka = kwh700.8 x Tsh273 = Tsh 191318.4/=

NB:Gharama hizi ni kwa taa moja ya watt 100 inayo waka masaa 24,hivyo unaweza kuzidishia gharama hizi na idadi ya taa ulizonazo katika banda lako kujua kiasi sahihi unacho lipa kwa siku,mwezi au mwaka.

Kiasi utakacho SAVE baada ya kufunga kifaa cha energy saver kwa taa moja
Kwa siku uta-save= Tsh 131/=

Kwa mwezi uta-save = Tsh 3931.2/=

Kwa mwaka uta-save = Tsh 47829.6/=

NB:Gharama hizi ni kwa taa moja ya watt 100 inayo waka masaa 24,hivyo unaweza kuzidishia gharama hizi na idadi ya taa ulizonazo katika banda lako kujua kiasi sahihi unachokuwa ume SAVE kwa siku,mwezi au mwaka.

HIVI NDIVYO KIFAA HIKI KITAKAVYOFUNGWA KATIKA MFUMO WAKO WA UMEME



Kifaa hiki kinafungwa bila malipo ya awali hadi ndani ya masaa 48 ya uchunguzi wa utendaji wake wa kazi.
Kifaa hiki Nimeki-design mimi mwenyewe bila ya kuwa na ushirikiano na kampuni yeyote au mtu yeyote.


Bonyeza hapa kwa maelezo zaidi ya kifaa hiki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…